1. Kikohozi kikavu ambacho hakisikii antibiotic mfululizo kwa zaidi ya wiki mbili.
2. Kutoka jasho usiku, ambalo linalowanisha hadi nguo ulizolalia.
3. Homa hasa usiku
4. Kukonda
5. Ukipima makohozi yataonyeha uwepo wa bacteria ingawa si wakati wote.
Wakti mwingine unaweza kukohoa damu.
TB au Kifua Kikuu ni ugonjwa wa kuambukiza ambao husababishwa na viini viitavyo tubercle bacilli. Wengi wetu tuna viini vya TB mapafuni mwetu lakini hii sikumaanisha kwamba tutauguza huu ugonjwa. TB hushika wale ambao wana ukosefu wa kinga mwilini unao sababishwa na kutokula chakula kizuri, matumizi ya madawa ya kulevya au wanaouguza magonjwa mengine.
TB ya mapafu ndio imeenea zaidi. Hata hivyo, viini vya TB vinaweza kusafirishwa kutoka mapafuni kupitia kwa damu hadi sehemu zingine za mwili na kusababisha hivyo viungo viathiriwe na TB.
Viini vya TB hupatikana kwa mate ya muuguzi. Wakati mgonjwa anakohoa, kupiga chafya au kutema mate kiholela, viini vya TB husambazwa kwa hewa. Mwenye afya akiipumuwa hewa hiyo anaambukizwa na mapafu yake inaanza kuwa na vijidonda.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.