TFF isiwababaishe watu kwa kutibu dalili badala ya maradhi yenyewe. Ijielekeze kwenye swala la msingi. Ndumbaru afungiwe asifungiwe, vilabu vimtume visimtume, haviko tayari kukatwa asilimia tano ya udhamini. TFF ilichoagizwa na Serikali sio kutafuta mchawi, ni kukaa na vilabu na kukubaliana juu ya swala la 5%. Inachotakiwa kutoa taarifa TFF sio nani kafungiwa au miaka mingapi. Swala ni: (a) wameshakubaliana na vilabu? (b) makubaliano hayo yanasemaje?
Hata mimi nashangaa kwann huyu NDUMBA hakufungiwa maisha kabisa kutoshiriki mambo ya soka!!! alipindisha sheria huyu kwenye usajil wa okwi kutoka yanga kwenda simba, safi sana tff.alimuidhinisha okwi kucheza simba kimagumashi..malinzi ungemfungia maisha kabisa..pumbav!
Hata mimi nashangaa kwann huyu NDUMBA hakufungiwa maisha kabisa kutoshiriki mambo ya soka!!! alipindisha sheria huyu kwenye usajil wa okwi kutoka yanga kwenda simba, safi sana tff.
Hata hiyo miaka saba ni sawa na kufungiwa maisha tu, kuwa na amani dudu limetolewa; asante TFF kwa maamuzi hayo mazuri aende huko kwenye mahakama za kawaida akabishane na washenzi wenzake.
Ndo hivo mkuu yahoo,nilitaka kushangaa tangu lini yanga ikashindwa kwnye ishu ya kisheria..kumbe sorce ni hili jambazi la sheria
Yah! Simchezo, naona povu tu.Hata hiyo miaka saba ni sawa na kufungiwa maisha tu, kuwa na amani dudu limetolewa; asante TFF kwa maamuzi hayo mazuri aende huko kwenye mahakama za kawaida akabishane na washenzi wenzake.
Malipo hapa hapa duniani, huyu si ndio alikuwa kinara kumhujumu Wambura
Yah! Simchezo, naona povu tu.
ππππ Malinzi alizungukwa na watu hatari sana bila kufahamuKamati ya nidhamu ya Shirikisho la soka nchi TFF, imemfungia wakili Damas Ndumbaro kujihusisha na mambo ya soka kwa muda wa miaka saba na faini ya kiasi cha pesa. Ndumbaro ambaye aliingia katika mzozo mkubwa na rais wa TFF, Ndugu, Jamal Malinzi wiki iliyopita baada ya TFF kuagiza kila klabu kukatwa asilimia tano za mapato yatokanayo na udhamini wa klabu hizo wanaoupata kutoka kwa Vodacom, wadhamini wakuu wa ligi kuu ya Tanzania Bara, na Azam Tv.
Ndumbaro alikimbilia katika vyombo vya habari na kusema wazi kuwa, klabu zimemuagiza kuwaambia TFF kuwa havipo tayari na havitakubali jambo hilo litokee, huku akijiamini na kuchambua baadhi ya vipengele na mambo ya sheria, Ndumbaro alivuka mipaka pale aliposema kuwa wanatafuta wastani wa wajumbe wa mkutano mkuu wa TFF na kupiga kura ya kutokuwa na imani na rais wa Shirikisho, Malinzi.
Kikao cha juzi cha kamati ya nidhamu kimefikia uamuzi wa kumfungia, Ndumbaro na kumlilipisha faini kwa sababu. Ndumbaro ambaye alizungumza kama wakili wa klabu za ligi kuu kupitia, Bodi ya Ligi amekanwa hadharani na vilabu huku vikisema kuwa havikumtuma kuzungumza yale ambayo alisema mbele ya vyombo vya habari. Klabu zimesema alizungumza kwa utashi wake mwenyewe, na si wao walimtuma.
Kilichomuhuku ni yeye kutaka kubadilisha maamuzi ya kamati ya utendaji ya TFF bila kuthibitishwa na wajumbe wa Bodi ya Ligi na kukubaliana. Kupingana maamuzi ya kamati ya utendaji ni kosa la kinidhamu. Ndumbaro amehukumiwa kutokana na makosa hayo na kama angezungumza kwa niaba ya klabu basi adhabu hiyo ingekwenda kwa kwao, lakini yeye alijizungumzia tu kama vile alivyotaka iwe.
ShaffihDauda
Malinzi yupo wapi na Ndumbaro yupo wapi?ππππ Malinzi alizungukwa na watu hatari sana bila kufahamu
Na za Al Ahly, anafanya soka kama uadui[emoji1787][emoji1787]ndio huyu anakataza jezi za Mamelodi
Tokea lini uvaaji wa nguo ukahitaji ruhusa ama uhakiki wa uraia?