DOKEZO Dampo lisilo rasmi ni hatari kwa afya zetu Wananchi wa Chamazi Dovya, viongozi wa Mtaa hawatusikilizi

DOKEZO Dampo lisilo rasmi ni hatari kwa afya zetu Wananchi wa Chamazi Dovya, viongozi wa Mtaa hawatusikilizi

  • Thread starter Thread starter Anonymous
  • Start date Start date
Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
87aaa17a-d3cb-4455-92e7-0bc81dbd1b2d.jpeg
Mtaani kwetu maeneo ya Chamazi Dovya kwa Nzala jirani na Shule ya JB (Dar es Salaam) kuna dampo ambalo sio rasmi, limekuwa kero kwa muda mrefu kwa sisi wakazi wa maeneo hayo, pia lina athari nyingi kiafya na uchafuzi wa Mazingira kwa sisi tuliojenga karibu na eneo hilo.

Tumepeleka malalamiko yetu kwa Mwenyekiti wa Mtaa mara nyingi tu lakini hatuoni utekelezaji wowote wa kusitisha. Huu ni mwaka wa pili tangu dampo hilo lianzishwe, kuna muda tukipiga kelele wanasimama kidogo kisha baada ya muda wanaendelea kama kawaida.

Malalamiko hayo tumeshafikisha hadi kwa Mbunge wetu lakini hakuna alichofanya.

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) fikeni eneo hilo, wakazi wa maeneo hayo tuna hali mbaya, tunapoelekea kuna uwezekano wa kuibuka kwa mlipuko wa magonjwa mbalimbali kutokana na uchafu uliopo.

89d05e63-4564-473a-afb1-9bde72b4c4c2.jpeg

bfe4866f-dca8-4c37-8d2c-79a257cc1476.jpeg

136bc605-ec98-4af9-815a-4638fbf0fb99.jpeg
 
Tukiwaambia DSM imejaa maskini tupu asilimia 85% mnakataa angalia hayo makazi ya Vibwengo, kunguni na majini endeleeni kupauka DSM hovyo kabisa.
 
Tukiwaambia DSM imejaa maskini tupu asilimia 85% mnakataa angalia hayo makazi ya Vibwengo, kunguni na majini endeleeni kupauka DSM hovyo kabisa
Watu wa vijijini wananuka njaa kwa asilimia zaidi ya Dar. Wewe kama unaishi huko na umefanikiwa kuwa na kipato, relax fanya yako. Watu wa Dar hutuwezi tuache.
 
Back
Top Bottom