KERO Danadana malipo ya fidia Kipunguni

KERO Danadana malipo ya fidia Kipunguni

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Insidious

JF-Expert Member
Joined
Oct 28, 2020
Posts
654
Reaction score
895
Napenda kutoa malalamiko yangu makali na kero kuhusu kucheleweshwa kwa malipo ya fidia kwa ardhi tuliyotoa KIPUNGUNI kwa ajili ya upanuzi wa uwanja wa ndege wa serikali. Taarifa ya tathmini ya ardhi ilifanywa tangu jana, na hata miaka ya nyuma (1997), lakini hadi leo hatujaona malipo yoyote.

Yalishatolewa matamko kutoka kwa mawaziri wawili (Mwigulu na Mbarawa) tena wakiwa bungeni, waliotoa ahadi hewa pamoja na mbunge wa segerea (bonnah kamoli) kuwa malipo yatafanyika mwaka huu, wakihakikisha yatafanyika mwezi huu wa nane ambao bado siku sita tu uishe.

Naomba malipo yafanyike mara moja ili tuweze kuhama kwenda maeneo bora zaidi, kwani haturuhusiwi kuendeleza chochote kattika maeneo haya ambayo sasa yamekuwa vichaka.

Aidha, tunasisitiza kwamba malipo haya yawe na riba kama ilivyoainishwa katika sheria za upatikanaji wa ardhi.

Tunahitaji hatua za haraka kuchukuliwa ili kuhakikisha tunapata haki yetu.

Pia soma:Mbunge Bonna Kamoli atishia bungeni sakata la wananchi Kipunguni kupisha Airport, hawajalipwa fidia miaka 27 sasa
 
Nadhani last month rais alisema malipo ya fidia yasubiri kwanza maendeleo yapatikane ndio wadai fidia waweze kulipwa.. Kama hiyo kauli haitatenguliwa danadana zitaendelea
 
Napenda kutoa malalamiko yangu makali na kero kuhusu kucheleweshwa kwa malipo ya fidia kwa ardhi tuliyotoa KIPUNGUNI kwa ajili ya upanuzi wa uwanja wa ndege wa serikali. Taarifa ya tathmini ya ardhi ilifanywa tangu jana, na hata miaka ya nyuma (1997), lakini hadi leo hatujaona malipo yoyote.

Yalishatolewa matamko kutoka kwa mawaziri wawili tena wakiwa bungeni, waliotoa ahadi hewa pamoja na mbunge wa segerea kuwa malipo yatafanyika mwaka huu, wakihakikisha yatafanyika mwezi huu wa nane ambao bado siku sita tu uishe.

Naomba malipo yafanyike mara moja ili tuweze kuhama kwenda maeneo bora zaidi, kwani haturuhusiwi kuendeleza chochote kattika maeneo haya ambayo sasa yamekuwa vichaka.

Aidha, tunasisitiza kwamba malipo haya yawe na riba kama ilivyoainishwa katika sheria za upatikanaji wa ardhi.

Tunahitaji hatua za haraka kuchukuliwa ili kuhakikisha tunapata haki yetu.

Pia soma:Mbunge Bonna Kamoli atishia bungeni sakata la wananchi Kipunguni kupisha Airport, hawajalipwa fidia miaka 27 sasa
Toka niko std 1 mpaka namaliza chuo na leo nna mke na watoto ni mwendo wa dana dana tu.

Wameishia kuchora chora nyumba za watu dah maisha haya na wengine mpaka wamehama
 
Unyama wa ccm kwa watu wa kipunguni, Mungu asipoingilia kati nitashangaa sana!
 
Toka mwaka 2022 kulipita zoezi la upimaji pale kipunguni. Wakiambiwa wananchi serikali inataka kuongeza uwanja wa ndege.

Watu wakasimamishwa hakuna kujenga, wapangaji wakapewa notice wahame muda wowote wanavunja.

Wananchi wakapewa makaratasi kuonyeshwa stahiki chao. Leo ni sept 2024, miaka miwili sasa wananchi wanateseka watoto wanashindwa kulipiwa ada. Wapangaji wamekimbia wotee hataa ukiwaita tena hawataki kusikiaaaa.

Swali kwa wahusika pls wekeni msimamo wazi kwa maandishi kama hio project imeshindikana na wananchi waendelee kujengaa na kupangisha.

Yaani wale wananchi wanaishi kama yatima wasio na wazazi. Ukweli kila anaeguswa anaongea uongo toka 2022 subirin match 23..subirn sept 2023. Ikaja 2024 Jan subirin bajeti.....wananchi wamo. Bajeti imepitaaaa mbunge anasumbuliwa mpaka hana hamu na simu.

Tunaomba wananchi wapewee msimamoo wa ujenzi wa kipungun kama haupoo waendeleze kujenga na kupanga

Wanatesekaa sana, sana...

Mungu wabariki kipungun na watoto zaoooo...

Amen
 
Kipunguni
Kipunguni
Kipunguni
Machozi yananitoka
Kama kijana nmesimama ujenzi miaka inasonga nguvu zinaisha hakuna kuendelea

Wapangaji wameondoka
Wazee wamekosa Kodi wanaishi maisha magumu
Ni wakati serikali iseme jambo moja inalipa ilipe watu wahame


Kama hakuna bomoa bomoa waseme tuendelee na mambo mengine

Ishu hii ina zaidi ya miaka 27
Kila kukicha ahadi zisizo fika ukomo.
 
Kipunguni
Kipunguni
Kipunguni
Machozi yananitoka
Kama kijana nmesimama ujenzi miaka inasonga nguvu zinaisha hakuna kuendelea

Wapangaji wameondoka
Wazee wamekosa Kodi wanaishi maisha magumu
Ni wakati serikali iseme jambo moja inalipa ilipe watu wahame


Kama hakuna bomoa bomoa waseme tuendelee na mambo mengine

Ishu hii ina zaidi ya miaka 27
Kila kukicha ahadi zisizo fika ukomo.
Tapeli Mwigulu Nchemba ndio mnategemea awalipe?

Halafu utashangaa hapohapo ccm inapata kura na kuna wajumbe wa ccm.
 
Back
Top Bottom