Dangote anavyopata wakati mgumu kuendesha kiwanda chake che Sementi Ethiopia

The Mongolian Savage

JF-Expert Member
Joined
Jul 5, 2018
Posts
8,082
Reaction score
17,838
Nadhani Aliko Alhaj Dangote hakuwafahamu vizuri kabila la Oromo ambalo wa Ethiopia wengine wanawaita barbaric kwa kuenda kujenga kiwanda chake cha Sementi kwenye ardhi yao ya Oromia.

Yeye alikula deal na watu wa Serikali lakini wa Oromo wakamuwekea masharti jinsi ya kukiendesha hicho kiwanda wakitaka wakurugenzi na mameneja wote wawe wa oromo pamoja na asilimia 80% ya wafanyakazi.

Dangote hakufanya hivyo akawaleta wahindi. Tayari hao wahindi wakurugenzi watatu walishauliwa kwa kupigwa risasi wakiwa kwenye gari kuelekea Addis Ababa.

Wafanyakazi wageni wote wanaishi kwa hofu na kujificha. Magari ya kampuni yanachomwa moto mara kwa mara.

Anataka kukukifunga hicho kiwanda.
 
huwa nikiangalia movie ya black hawk down naimagine Ethiopia ni nchi hatari zaidi,by the way sijawahi kusikia ata mtu anaomba muongozo wa kuzamia huko
 
Wahabeshi wabishi sana. Sema ubishi wao umewasaidia kiasi flani kumiliki uchumi wao..
 
Oromo ni kabila kubwa Ethiopia haiwezekani wasiwe na wasomi wa kuweza kushika hizo nafasi.

Dangote aangalie upya sera yake ya ajira kama anataka afaidi matunda ya uwekezaji wake. Hiyo sera hata ingekuwa India wasingeikubali. Lazima uangalie maslahi ya wenyeji kwanza.
 
Hawa nimewakubali...wanajielewa. hawezikani upo hapa nchini kwetu alafu top managerial positions unawapa wahindi...wats the point ya wewe kuwekeza hapa kwetu?
 
Safi, ale mikwaju tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…