Dangote Cement penetrates giant Kenyan Cement Market

Mimi yangu macho na masikio.Lakini Nina imani kuna jambo kubwa kuliko anayosema waziri na Dangote hadharani .Hapo lazima mikono ya mafisadi Wa bongo IPO tu.

The game has just changed!!! golini yupo Juma Ponda Mali
 


Bila kusahau ukiwa na mashine ya kunyolea nywele nacho pia ni kiwanda yatupasa tujivunie viwonder vyetu
 
Hivi nyinyi ambao mnapenda kurukia mambo ambayo hamuyafahmu kwa kina na ku-draw conclusion ni watu wa aina gani?
Hivi unafahamu makubaliano ya uwekezaji kati ya kampuni hiyo na serikali???
Hivi unafahamu pia kitu ambacho dangote anakihitaji?
Humu jamvini ni nyinyi ambao huwa mnapenda kulalamika kuwa wawekezaji wa nje wanapewa mikataba ya 'carte blanche' na mwisho wa siku nchi ikiwa haimbulii kitu? siyo ninyi mliotaka mikataba ambayo inaweka maslahi ya nchi kwanza?
Siku zote ninawaambia fanyeni kautafiti kabla ya kuanza kuponda. Naona utafiti wenu wote unaishia kwenye magazeti tu. na wengi wao kwa sasa kazi ni kuandika hisia ya wahariri wao badala ya kufanya utafiti, kuuliza wataalamu na mwishowe kuandika. Kwa spidi hii, mtaishia kuwa wataalam wa kulalamika tu.
 
Mi nataka tu kujua,kabla ya Dangote kuwepo...hali ilikuwaje ambayo huenda ilihatarisha maisha ya watanzania..?
Na ni watz wangapi hali hiyo iliwagharimu?
Akiondoka ni nini madhara yake.?
 
Kama una macho mazuri utakubaliana na mimi ya kuwa:-

Ukimuangalia mkulu kwa makini hasa anapohutubia anafanana sana na shetani.









.















.










.













.





















.








.









.






Mjombaake na shempasi wa gologolo kule lushoto.
 
nilichogundua tatizo ni GESI. Huyu Dangote anahitaji gesi yetu kwa gharama yoyote. Hizo cement ni njia tu ya kuchukua gesi. Naipongeza serikali kwa kushtukia hila zake na kumkazia. Serikali ikikubaliana nae basi itakuwa tu sawa na mikataba ya kilaghai kama ya madini na umeme. Mnaoponda serikali ni wavivu wa kufuatilia mambo na kuishia kupiga stori za vijiweni kwenu.
 
Dah....sasa ndio nn hii...je kwenye mikataba mliweka anunuwe makaa ya mawe Ng'aka?...

Makaa hayana ubora kama ya South....jiulize kwann aende south wakati hapo jiran na kiwanda yapo? Mtawakimbiza wawekezaji wote..na mtabakia kuwa koloni la kenya kibiashara!
 
Una maandishi - yanayothibitisha kuwa serikali imeshindwa kutekeleza makubaliano na Dangote?

Acha aende tu Kenya
 
Kugombana na Dangote ni kosa litakalotugharimu sana.Tajiri aina ya Dangote sio wa kufanyia mzaha hata kidogo.
Hatutaki matajiri wa kubembelezwa , tunaviwanda vya simenti
1. Nyati
2. Twiga
3. Simba
4. Tembo
5. Kifaru / rhino
6. Camel/ ngamia

Ukiona viwanda vyote vina majina ya wanyama, hivi Dangote ni mnyama gani? Inawezekana ndio sababu ya mkwamo wake, mwambie aje na mzaha wake tuone
 

Dangote alikuwa anampango toka siku nyingi wakufungua kiwanda cha cement Kenya licha ya kuwa na Tanzania amefungua, Hivi nyie mnazani ni rahisi sana ku pull out investment, tena ya kiwanda kikubwa kama kile.
 

Sawa lakini kumbuka bado miaka mitatu na miezi kadhaa kampeni za uchaguzi wa 2020 zianza ambapo tutahoji kuhusu uchumi wa viwanda tulioahidiwa.
 
Kweli kabisa mkuu,tumekuwa na utaratibu wa ajabu sana tangia tupate uhuru au tangia mwl nyerere alivyotuacha.Rais huyu anakuja anafanya hiki,yule anakuja ana haribu kila kitu,tunachagua kiongozi anaenda pale ikulu kwenda kufanya majaribio ya ubongo wake, akifeli tu Watanzania wote hoi yaaani tupo tupo tu, Tumekuwa ni nchi ya majaribio ndiyo maaana tuliona october 2015 idadi ya waliochukua form ya kugombea Urais ilikuwa kubwa sana,kumbe watu wanajua kwamba unaweza kwenda pale ikulu kufanya sarakasi na mambo yako siyo kuwapigania wananchi masikini waliokuchagua.Nchi hii haina utaratibu ni kama kijiwe.
 
Viongozi wetu wana upeo finyu sana..
Sasa tatizo kama hilo wamelishindwa ..?
Wasidhani kuwa kuitwa profesa ndio umeshakuwa problem solver na kwamba eti unaweza kila kitu. La hasha.
Sasa wewe ambaye huna akili finyu umeishia JF khe khe kheeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee JF na vituko vyake.
 
Asnte Yesu endelea kutenda miujiza
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…