Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Kauli hiyo ameitoa Wilayani Muleba Mkoani Kagera katika Mkutano wa hadhara wa Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi CCM Balozi Dkt. Emanuel Nchimbi ambapo amewataka kushirikiana na kufanya kazi kwa weledi na uadilifu ili kuwezesha upatikanaji wa Vitambulisho vya Taifa kwa wakati.
"Niwaombe Uhamiaji na NIDA shirikianeni katika suala zima la utambuzi na usajili wa wananchi ili kuharakisha upatikanaji wa vitambulisho vya Taifa kwa Wananchi wenye sifa. Sitegemei kuona jambo lolote kukwamisha Vitambulisho hivyo bila sababu za msingi," amesema Sillo.
Soma Pia: NIDA badilikeni na toeni huduma kwa weledi
Ametoa agizo hilo ikiwa ni maelekezo ya Katibu Mkuu wa Chama akiwa Wilayani Ngara Mkoani Kagera na kuelezwa na Wananchi kuwa bado wanachangamoto ya upatikanaji wa Vitambulisho vya Taifa.
Hata hivyo, amemuelekeza Afisa usajili wa NIDA kuwa katika Mkoa wa Kagera bado kuna Vitambulisho 78,766 havichukuliwa na Wananchi ambapo ametoa wito kwa Wananchi kwenda kuchukua Vitambulisho hivyo katika Wilaya, Kata na Vijiji vilivyopo karibu nao.
Pia soma:
~ Ugawaji wa NIDA wilaya ya Busega unasuasua zaidi ya mwezi. Wanafunzi tunaotegemea namba kuomba mkopo HESLB hatarini kukwama
~ Waziri Masauni: NIDA kuna shida ya usimamizi, Uongozi una shida, Watu wanateseka kupata Vitambulisho