KERO Dar: Baadhi ya watoza ushuru Stendi ya Magufuli sio waadilifu, wanatengeneza mazingira ya kutorejesha chenji

KERO Dar: Baadhi ya watoza ushuru Stendi ya Magufuli sio waadilifu, wanatengeneza mazingira ya kutorejesha chenji

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
photo_2024-11-10_23-10-37.jpg

photo_2024-11-10_23-10-40.jpg

Naomba nitumie jukwaa hili kuwasilisha dukuduku yangu nikiwa naamini ujumbe utawafikia wahusika kama ambavyo tumekuwa tukiona kwenye baadhi ya kero ambazo zimekuwa ziibuliwa hapa jukwaani.

Ni kwa mara kadhaa nimekuwa nikienda Stendi ya Mbezi Magufuli (Magufuli Bus terminal) nikiwa nasafiri au kupokea ndugu na jamaa zangu, lakini kuna jambo sio rafiki kabisa linafanywa na baadhi ya wahudumu wanaotoa kadi kwa ajili ya kuingia ndani ya stendi hiyo linatakiwa kukemewa.

Kwa kawaida utaratibu uliopo unamtaka Mwananchi kulipia kiasi cha Tsh. 300 kuingia ndani, lakini baadhi ya wahudumu hawarejeshi chenji hasa ya Tsh.200 wanataka wakate Shilingi 500, wanapoulizwa wanasema hawana chenji wakati mwingine wanachagua Mtu gani wamrejeshee cheji yote kwa kumuangalia jinsi alivyo.

Ikitokea Mtu amewakazia wanamrejeshea hela yake wanamwambia kama anataka akatwe Shilingi 300 basi atafute chenji awapelekee kiasi kamili, wanafanya hivyo huku wakiwa wanatoa majibu na lugha zisizo rafiki kwa wapokea huduma jambo ambalo wakati mwingine linaibua mizozo.

Mazingira hayo nimeyashuhudia mwenyewe mara kwa mara watu wakikatwa shilingi 500 huku wengine wakisimamishwa pembeni kwa muda mrefu na kuambiwa kwamba wangojee chenji hata kama wanayo, lakini wanatumia mbinu hiyo ili kuwakatisha tamaa baadhi ya watu waweze kuacha chenji hiyo kwa kuwa wanajua wengi wanakuwa na haraka.

Nitoe wito wangu kwa mamlaka zinazosimamia stendi hiyo kufuatilia na kuwachukulia hatua wahudumu wanaobainika kukosa uadilifu na kama kuna upungufu wa cheji suala hilo lishughuliwe ipasavyo ili kuondoa kero na usumbufu.

photo_2024-11-10_23-10-10.jpg

photo_2024-11-10_23-10-33.jpg

photo_2024-11-10_23-10-29.jpg
 
Wahuni hao kama wale wa mwendokasi tu!
 
Mtanzania asipokuwa na kazi ulia lia sanaa, ila akipata kazi ugeuka kuwa na dharau na kauli chafu sanaaa
 
Hao ni washenzi sana mimi kuna siku nilimkazia hadi alitoa chenji baada ya kuona watu wawili wa mbele yangu hawakurudishiwa mia mbili zao. Hao wameshafanya hayo ndio marupurupu yao.
 

Naomba nitumie jukwaa hili kuwasilisha dukuduku yangu nikiwa naamini ujumbe utawafikia wahusika kama ambavyo tumekuwa tukiona kwenye baadhi ya kero ambazo zimekuwa ziibuliwa hapa jukwaani.

Ni kwa mara kadhaa nimekuwa nikienda Stendi ya Mbezi Magufuli (Magufuli Bus terminal) nikiwa nasafiri au kupokea ndugu na jamaa zangu, lakini kuna jambo sio rafiki kabisa linafanywa na baadhi ya wahudumu wanaotoa kadi kwa ajili ya kuingia ndani ya stendi hiyo linatakiwa kukemewa.

Kwa kawaida utaratibu uliopo unamtaka Mwananchi kulipia kiasi cha Tsh. 300 kuingia ndani, lakini baadhi ya wahudumu hawarejeshi chenji hasa ya Tsh.200 wanataka wakate Shilingi 500, wanapoulizwa wanasema hawana chenji wakati mwingine wanachagua Mtu gani wamrejeshee cheji yote kwa kumuangalia jinsi alivyo.

Ikitokea Mtu amewakazia wanamrejeshea hela yake wanamwambia kama anataka akatwe Shilingi 300 basi atafute chenji awapelekee kiasi kamili, wanafanya hivyo huku wakiwa wanatoa majibu na lugha zisizo rafiki kwa wapokea huduma jambo ambalo wakati mwingine linaibua mizozo.

Mazingira hayo nimeyashuhudia mwenyewe mara kwa mara watu wakikatwa shilingi 500 huku wengine wakisimamishwa pembeni kwa muda mrefu na kuambiwa kwamba wangojee chenji hata kama wanayo, lakini wanatumia mbinu hiyo ili kuwakatisha tamaa baadhi ya watu waweze kuacha chenji hiyo kwa kuwa wanajua wengi wanakuwa na haraka.

Nitoe wito wangu kwa mamlaka zinazosimamia stendi hiyo kufuatilia na kuwachukulia hatua wahudumu wanaobainika kukosa uadilifu na kama kuna upungufu wa cheji suala hilo lishughuliwe ipasavyo ili kuondoa kero na usumbufu.

Hivi sasa kutokana na tabianchi dunia ina uhaba wa chenji.
 
Hii ni kero kweli

Naomba nitumie jukwaa hili kuwasilisha dukuduku yangu nikiwa naamini ujumbe utawafikia wahusika kama ambavyo tumekuwa tukiona kwenye baadhi ya kero ambazo zimekuwa ziibuliwa hapa jukwaani.

Ni kwa mara kadhaa nimekuwa nikienda Stendi ya Mbezi Magufuli (Magufuli Bus terminal) nikiwa nasafiri au kupokea ndugu na jamaa zangu, lakini kuna jambo sio rafiki kabisa linafanywa na baadhi ya wahudumu wanaotoa kadi kwa ajili ya kuingia ndani ya stendi hiyo linatakiwa kukemewa.

Kwa kawaida utaratibu uliopo unamtaka Mwananchi kulipia kiasi cha Tsh. 300 kuingia ndani, lakini baadhi ya wahudumu hawarejeshi chenji hasa ya Tsh.200 wanataka wakate Shilingi 500, wanapoulizwa wanasema hawana chenji wakati mwingine wanachagua Mtu gani wamrejeshee cheji yote kwa kumuangalia jinsi alivyo.

Ikitokea Mtu amewakazia wanamrejeshea hela yake wanamwambia kama anataka akatwe Shilingi 300 basi atafute chenji awapelekee kiasi kamili, wanafanya hivyo huku wakiwa wanatoa majibu na lugha zisizo rafiki kwa wapokea huduma jambo ambalo wakati mwingine linaibua mizozo.

Mazingira hayo nimeyashuhudia mwenyewe mara kwa mara watu wakikatwa shilingi 500 huku wengine wakisimamishwa pembeni kwa muda mrefu na kuambiwa kwamba wangojee chenji hata kama wanayo, lakini wanatumia mbinu hiyo ili kuwakatisha tamaa baadhi ya watu waweze kuacha chenji hiyo kwa kuwa wanajua wengi wanakuwa na haraka.

Nitoe wito wangu kwa mamlaka zinazosimamia stendi hiyo kufuatilia na kuwachukulia hatua wahudumu wanaobainika kukosa uadilifu na kama kuna upungufu wa cheji suala hilo lishughuliwe ipasavyo ili kuondoa kero na usumbufu.

View attachment 3149165
View attachment 3149166
View attachment 3149169Hii ni kero kubwa kweli. Sehemu kama hiyo inayohudumia wananchi wengi haiwezi kukosa chenji. Na hawa watu wanafanya makusudi tena wanakuwa wakali sana hata kama unaziona chenji mezani; wakitegemea mtu ukate tamaa. Kumbuka hiyo 200 inaweza kumvusha mtu feri au inaweza kununulia maji ya kupima hapo hapo magufuli ya lita moja yakamsaidia siku nzima. Mamlaka ziliangalie hili kwa ukaribu na wahusika wawajibishwe.​
 
Back
Top Bottom