Dar es Salaam Bookshop

Dar es Salaam Bookshop

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
Picha hii kwangu inanikumbusha miaka yangu ya mwanzo udogoni naanza kujitambua na kuingia kwenye duka la vitabu kununua vitabu.

Nimenunua vitabu vingi duka hili kuanzia mwaka wa 1963 nikiwa na umri wa miaka 11.
Safari ya kutoka nyumbani kuja "Picha ya Bismini," (Askari Monument) ilikuwa safari makhsusi.

Nitaoga na kuvaa, "Sunday Best," nguo zangu nzuri nizipendazo.
Kwa miaka ile Dar es Salaam Bookshop ilikuwa ikiongoza kama duka bora la vitabu mji mzima.

Nilikuwa nikiingia ndani ya duka hili nilikuwa naingia katika dunia ambayo mimi peke yangu nilikuwa naielewa.
Nakuwa sipo Dar es Salaam niko angani na hakuna viumbe vingine ila mimi na vitabu.

Nitatembea ndani mle kutoka shubaka moja hadi lingine, shubaka lingine hadi lile na lile hadi lingine.

Nachukua kitabu kimoja natazama picha kwenye cover na jina la kitabu, "Adili na Nduguze," Shaaban Robert, "Machimbo ya Mfalme Suleiman," Rider Haggard, Alif Lela Ulela orodha ndefu.

Itachukua muda kuamua ninunue kitabu kipi.
Nikitoka kwenye vitabu naingia kwenye sehemu ya zana za uchoraji kwani nilikuwa artist.

Water colours gani zimeingia na brush zipi.
Penseli za Staedtler na vifutio vyake.

Siku zile zilikuwa siku za neema kila ukiingia Dar-es-Salaam Bookshop wana vitabu vipya haba jana.
Namkumbuka dada mmoja alikuwa pale counter.

Baada ya miaka mingi dada huyu nikaja kumuona sasa si msichana tena ni mama mke wa marehemu Mbaruku Mwandoro na mimi si mvulana mdogo ni kijana mkubwa.

Hakuna kitu kilichokuwa kinanipa furaha kama kuweka vitu vyangu kwenye kaunta nikalipa kisha nikafungiwa na kutiliwa kwenye mfuko nadhifu wa kuvutia.

Miaka mingi sana ikapita.
Iko siku nimepita Dar-es-Salaam Bookshop ikanijia hamu na fikra niingie ndani.

Sikustahamili.
Nilitoka nje haraka.

Ningelia wapita njia wenzangu wasingeniacha wangenikimbiza haraka hospitali.
Labda kachanganyikiwa ghafla.

Msongo wa mawazo.
Sijapata ujasiri wa kurejea mahali pale tena.

Nikawa najiuliza nini kimeisibu nchi yangu?

1652905759835.png
 
Kweli humo ndani Mzee Mo Said ndio ulipokutana na Atlas ya Dunia...
Ukaamua kuigagaraza nchi hadi nchi, mji hadi mji,,,
Kama ninavyokumbuka somo la Geography, shule ya msingi, Mwalimu wa somo akiingia na Atlas na kuifungua... huku akisema leo tunaenda uwanja wa ndege wa kimataifa wa Dar es Salaam (DIA 1980's) na kupanda ndege ya shirika la ndege la Uswiss na kuenda kuitembelea milima ya Alps..
Kwa kweli nilikuwa nina "daydreaming" darasani kwa ufundishaji wa Mwalimu huyu...
 
Vipi hao wazee wako ndio waliomiliki hiyo bookshop.?

#MaendeleoHayanaChama
 
Nchi yako imekuwa genge kubwa la mabishano ya mpira na vijiwe vya kubeti.
 
Hivi yule muhindi na mke wake bado wanauza vitabu. Mara ya mwisho kuingia hapo ilikuwa mwaka 2017. Hilo chimbo langu la NOVELS za JAMES HADLEY CHASE.
 
Hivi yule muhindi na mke wake bado wanauza vitabu. Mara ya mwisho kuingia hapo ilikuwa mwaka 2017. Hilo chimbo langu la NOVELS za JAMES HADLEY CHASE.
Mura...
Dar es Salaam Bookshop haikuwa ya Wahindi.

Bila shaka unazungumzia duka lingine.
 
Hivi yule muhindi na mke wake bado wanauza vitabu. Mara ya mwisho kuingia hapo ilikuwa mwaka 2017. Hilo chimbo langu la NOVELS za JAMES HADLEY CHASE.
Tuliokuwa hatujui KIMOMBO, novels zetu, zilikuwa ni za akina MUSIBA, SIMBAMWENE, HAMMIE RAJAB, KASSAM MUSA, NICO YE MBAJO, na gazeti la SANI nk!
FB_IMG_1652665379368.jpg
 
Pole Kiongozi, Vijana sikuizi wanawaza Pono na PlayStation . Japo hatuwezi kuacha kuwaelimiaha na kuwapa vitabu.

Binafsi natoa huduma ya vitabu kwa mawasiliano tutafutane kwa no: 0787 728422 nitakusaidia.
 
Kweli humo ndani Mzee Mo Said ndio ulipokutana na Atlas ya Dunia...
Ukaamua kuigagaraza nchi hadi nchi, mji hadi mji,,,
Kama ninavyokumbuka somo la Geography, shule ya msingi, Mwalimu wa somo akiingia na Atlas na kuifungua... huku akisema leo tunaenda uwanja wa ndege wa kimataifa wa Dar es Salaam (DIA 1980's) na kupanda ndege ya shirika la ndege la Uswiss na kuenda kuitembelea milima ya Alps..
Kwa kweli nilikuwa nina "daydreaming" darasani kwa ufundishaji wa Mwalimu huyu...
Kusoma Atlas ni raha sana. Na unapokuwa mkubwa unaepuka ushamba na aibu ndogondogo.
 
Back
Top Bottom