Dar Es salaam: CG Mwenda , Desemba ni mwezi wa kuwashukuru walipakodi na kuwasikiliza

Dar Es salaam: CG Mwenda , Desemba ni mwezi wa kuwashukuru walipakodi na kuwasikiliza

TRA Tanzania

Senior Member
Joined
Jul 16, 2022
Posts
128
Reaction score
370
1000513221.jpg

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imesema mwezi huuu wa Disemba ni mwezi wa kuwashukuru na kuwasikiliza walipakodi wote nchini.

hayo yamebainishwa na Kamishna Mkuu wa Mamlaka hiyo Bw. Yusuph Juma Mwenda leo tarehe 11/12/2024 ofisini kwake jijini Dar es Salaam alipokutana na Umoja wa Mabenki Tanzania (TBA) kwa lengo la kuwasikiliza na kuwashukuru kwa kuendelea kulipa kodi na kuwezesha walipokodi wengine kufanyabiashara.

Aidha, Kamishna Mkuu amesema yeye pamoja na menejimenti ya TRA hawatakaa ofisini mwezi huu bali watatoka kwenda kuwafuata na kuwasikiliza walipakodi.
" Desemba ni mwezi wa kuwashukuru walipakodi wote nchini ...lakini huuu mwezi wa kusikiliza walipakodi wote Tanzania... tumeambizana Makamishna wote, wakurugenzi wote, mameneja wote hawatakaa ofisni bali wataenda kuwasikiliza walipakodi"

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti mwenyekiti wa Umoja wa Mabenki Tanzania, Bw. Geofrey Mchangila ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa Citibank ameshukuru kukutana na kufanya mazungumzo na Kamishna Mkuu na wameweza kujadiliana mambo mbalimbali ambayo yataendelea kuboresha sekta ya fedha na kutoa mchango katika ukuaji wa uchumi wa nchi.

Naye Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB Bi. Ruth Zaipuna amesema TBA itaendelea kushirikiana na TRA kuhakikisha kwamba mabenki yataendelea kulipakodi sahihi na kwa wakati kwa manufaa ya nchi.
 
View attachment 3174675
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imesema mwezi huuu wa Disemba ni mwezi wa kuwashukuru na kuwasikiliza walipakodi wote nchini.

hayo yamebainishwa na Kamishna Mkuu wa Mamlaka hiyo Bw. Yusuph Juma Mwenda leo tarehe 11/12/2024 ofisini kwake jijini Dar es Salaam alipokutana na Umoja wa Mabenki Tanzania (TBA) kwa lengo la kuwasikiliza na kuwashukuru kwa kuendelea kulipa kodi na kuwezesha walipokodi wengine kufanyabiashara.

Aidha, Kamishna Mkuu amesema yeye pamoja na menejimenti ya TRA hawatakaa ofisini mwezi huu bali watatoka kwenda kuwafuata na kuwasikiliza walipakodi.
" Desemba ni mwezi wa kuwashukuru walipakodi wote nchini ...lakini huuu mwezi wa kusikiliza walipakodi wote Tanzania... tumeambizana Makamishna wote, wakurugenzi wote, mameneja wote hawatakaa ofisni bali wataenda kuwasikiliza walipakodi"

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti mwenyekiti wa Umoja wa Mabenki Tanzania, Bw. Geofrey Mchangila ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa Citibank ameshukuru kukutana na kufanya mazungumzo na Kamishna Mkuu na wameweza kujadiliana mambo mbalimbali ambayo yataendelea kuboresha sekta ya fedha na kutoa mchango katika ukuaji wa uchumi wa nchi.

Naye Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB Bi. Ruth Zaipuna amesema TBA itaendelea kushirikiana na TRA kuhakikisha kwamba mabenki yataendelea kulipakodi sahihi na kwa wakati kwa manufaa ya nchi.
Kwa nini tukiuliza maswali hamjibu?
 
Okay nadhani kama mtatoka maofisini na umepata muda wa kuanzisha huu uzi basi huwezi kukosa muda wa kujibu maswali ya watu humu.....

 
Okay nadhani kama mtatoka maofisini na umepata muda wa kuanzisha huu uzi basi huwezi kukosa muda wa kujibu maswali ya watu humu.....

Chief tra wao wanapelekewa sheria na malengo.Ndiyo kila mwaka unaona bungeni utasikia hiki kipande hivi hiki kipande vile.Hawana meno ya kupunguza au kuongeza sababu tayari ni sheria wamepewa kuzisimamia.Ni muda muafaka kuwauliza wawakilishi wetu.Ni kweli nakubaliana nawe kodi ni muhimu ila nami nashauri serikali ingeangalia namna gani sote tulips ili tulips kiasi kidogo kuliko sasa wachache tunaolipa.
 
Pendekezo langu kwenu TRA Tanzania kila mwisho wa mwaka kuwepo na usamehevu wa kodi kwa wadaiwa tsh 5M kushuka chini.


Alafu muwe mnatoa Elimu ni mfanyabiashara yupi anastahili kukataa leseni na kulipia mapato hasa vijijini.


WAKATI HUO SERIKALI BORESHENI BARABARA KUTOKANA NA MNACHOVUNA.


KARIBUNI RUNGWE TUKUYU🙏
 
Chief tra wao wanapelekewa sheria na malengo.Ndiyo kila mwaka unaona bungeni utasikia hiki kipande hivi hiki kipande vile.Hawana meno ya kupunguza au kuongeza sababu tayari ni sheria wamepewa kuzisimamia.
Sababu hakuna aliyeweza kujibu maswali yangu na nahisi wao ni wataalamu wa haya mambo na nimewaona sidhani kama nimefanya kosa kuwauliza tija ya hayo makamuzi. Pia siku nyingine wakiwa wanatumwa wapeleke habari kwamba watu kitaa tunawakamua kwa sasa tunakamua mpaka damu tena bila kuwalisha
Ni muda muafaka kuwauliza wawakilishi wetu.Ni kweli nakubaliana nawe kodi ni muhimu ila nami nashauri serikali ingeangalia namna gani sote tulips ili tulips kiasi kidogo kuliko sasa wachache tunaolipa.
Issue sio makusanyo..., makusanyo ni mengi na kwa nchi ambayo ina utalii na mpaka madini mengine yanayopatikana hapa tu nchini utaona kwamba shida ni matumizi, ufujaji na ulaji


By the way na kama Serikali inaona imeshindwa kutoa huduma kwa watu kitaa basi ipunguze kutukamua

 
Back
Top Bottom