Nyakijooga
JF-Expert Member
- Dec 9, 2018
- 276
- 473
Siku za hivi karibuni eneo la Mbezi Beach Africana kutokea Tegeta mpaka Mataa ya njia panda ya Kawe kumekuwepo na foleni kubwa ambayo imekuwa kero kwa watumiaji wa 'Bagamoyo Road' hasa wanaoelekea Mjini, kupitia njia ya Mwenge au Kawe.
Watumiaji wa njia hiyo kwa muda wa asubuhi tunajikuta tunatumia zaidi saa nzima kutokea Africana hadi Bondeni, hali hii ni kero sana kwa kuwa inasababisha tunashindwa kufika kwa wakati kwenye majukumu.
Suala hili limekuwa likijitokeza kwa nyakati tofauti hata kabla ya kuanza kwa ujenzi wa njia ga Mwendokasi lakini watumiaji wa njia hiyo tunashindwa kuelewa ni shida ambayo imekuwa ikisababisha kero, jana nilidhani labda kuna msafara wa kiongozi wa ngazi za juu Serikalini kama tulivyozoea lakini haikuwa hivyo.
Tunaomba mamlaka husika hasa Traffic wanaosimamia kipande hicho washughulikie hiyo changamoto maana ni chanzo cha kupoteza muda na kuna wakati inaweza kusababisha wataalamu katika nafasi nyeti na muhimu kushindwa kufika kwenye majukumu kwa wakati hali ambayo inaweza kusababisha madhara mbalimbali.
Watumiaji wa njia hiyo kwa muda wa asubuhi tunajikuta tunatumia zaidi saa nzima kutokea Africana hadi Bondeni, hali hii ni kero sana kwa kuwa inasababisha tunashindwa kufika kwa wakati kwenye majukumu.
Suala hili limekuwa likijitokeza kwa nyakati tofauti hata kabla ya kuanza kwa ujenzi wa njia ga Mwendokasi lakini watumiaji wa njia hiyo tunashindwa kuelewa ni shida ambayo imekuwa ikisababisha kero, jana nilidhani labda kuna msafara wa kiongozi wa ngazi za juu Serikalini kama tulivyozoea lakini haikuwa hivyo.
Tunaomba mamlaka husika hasa Traffic wanaosimamia kipande hicho washughulikie hiyo changamoto maana ni chanzo cha kupoteza muda na kuna wakati inaweza kusababisha wataalamu katika nafasi nyeti na muhimu kushindwa kufika kwenye majukumu kwa wakati hali ambayo inaweza kusababisha madhara mbalimbali.