Mazee habari,nauliza kama naweza kwenda Mbeya toka Dar na ka gari kangu haka kadogo ka toyota Passo nina dharula kidogo,na kwa wazoefu mafuta ya kiasi gani naweza tumia,ka passo kenyewe ni kale kadogo ka pistoni 3....kwa mzoefu naomba anidaidie!
Katika siku nimesoma jibu sahihi ktk uendeshaji wa gari ni leo, ubarikiwe sana mkuu. Watu wengi wanajifunza kuendesha gari lakini hawajifunzi gari ni nini na ndio maana ukimuuliza dereva kwanini gari inapata moto mpaka maji kurushwa juu atakwambia hii gari nilia mbiwa nisiinunuwe engine zake sio nzuri, kikubwa wao nikuweka D nakukanyaga mafuta songa mbele.Kama umeamua kuipumzisha gari izime kabisa. Usiweke silence. Gari ukiiweka silence (idle) hujaipumzisha bado, engine bado inaendelea kuwa moto na tena kama umepiga nayo safari ndio kabisa inaendelea kuwa moto haipoi. Kumbuka, unapokuwa njiani, sio maji tu ndio yanapoza mashine, ule upepo unaopiga kwenye radiator na engine kwa ujumla unasaidia sana tena sana kupoza mashine ndio maana ukikaa silence mda mrefu unaona feni zinazunguka. ila kama upo kwenye mwendo, hutozisikia zikizunguka kwa sababu tayari upepo wa kutosha upo
Kwanini ipasue radiator?Hakikisha kabla haujapanda Mlima Kitonga unapumzisha gari hata Dk 10 ili usije ukapasua radiator,
Saa nne ya asubuhi?hakikisha macho yako yanaona vzr kutoka iringa mpaka makambako kuna ukungu sana hasa kipindi hiki cha baridi....beba debe mbili kuipa gari uzito kidogo upepo njiani hasa unapokutana na malori...me nilitusua dar to mza na IST nilitoka dsm saa tisa usiku saa nne nipo mwanza ila nipumzika 30min singida na 20min dodoma kwa kuzima gari kabisa
Ukiwaona kina majinjah na new force na dar lux wanakimbizana usiwafwate
Hasa majinjah mkorofi hatari
asante mkuu na wewe pia ubarikiwe.Katika siku nimesoma jibu sahihi ktk uendeshaji wa gari ni leo, ubarikiwe sana mkuu. Watu wengi wanajifunza kuendesha gari lakini hawajifunzi gari ni nini na ndio maana ukimuuliza dereva kwanini gari inapata moto mpaka maji kurushwa juu atakwambia hii gari nilia mbiwa nisiinunuwe engine zake sio nzuri, kikubwa wao nikuweka D nakukanyaga mafuta songa mbele.
Mkuu uko sawa kabisa hii nchi ina watu wajinga sana ,tena wenye mentality za kimasikini kabisa. Utakuta huyu naye eti ni msomi.Ndio akili yako ilipoishia,...ndio nyinyi mpaka leo mnaona kuwa na gari ni ufahari....wakati nowadays gari ni basic need,na unaamua kuwa na gari ili ikurahisishie maisha,....ubovu watanzania tunaona sifa kuwa masikini.....,sasa ka gari kama haka ka passo ambako mtu yeyote akijipanga ananunua wewe kichwani mwako unawaza ufahari.,....tujifunze kuficha upumbavu wetu kwa kukaa kimya....!
Kwa hoja hii na uzi ufungwe...ambaye hajaelewa hatakaa aelewe....gari kama ni nzima unaenda popote..Mkuu uko sawa kabisa hii nchi ina watu wajinga sana ,tena wenye mentality za kimasikini kabisa. Utakuta huyu naye eti ni msomi.
Back to the point . Hiyo gari unaenda popote kama barabara ni lami.Mimi nimeendesha gari hiyo kutoka Dar mpaka Mwanza bila hata kupumzika. Hao wanaokuambia sijui Kila baada 120KM upumzishe gari huo ni uswahili tupu wala hawana technical factor.
Mkuu nenda safari yako na ninaamini utafika salama kabisa. Achana na waswahili.
Wenye prado zao watakuja hapa wakukatalie...mkuu juzi nimetoka kagera bukoba mpaka Kilimanjaro moshi lakin nililala arusha yaan passo ni gari moja tamu sana na pia nilikuwa peke yangu tu na speed mwisho 1000