Dar: Polisi yawafungia leseni madereva 30 kati ya 179 waliokamatwa katika kipindi cha sikukuu

Dar: Polisi yawafungia leseni madereva 30 kati ya 179 waliokamatwa katika kipindi cha sikukuu

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limewafungia leseni madereva 30 kati ya 179 waliokamatwa katika kipindi cha sikukuu za Krismasi na Mwaka Mpya 2025.

Madereva hao 30 walikamatwa katika operesheni maalumu na walipopimwa walikutwa na ulevi kwa kiwago cha zaidi ya miligramu 80.

Soma Pia: Mbeya: Madereva wa mabasi ya New Force, Zanuni, Rungwe Express, Super Rojas, Abood Bus Service na Kyela Express wafungiwa leseni kwa muda


Hayo yamesemwa na Kamanda wa Kanda hiyo, Jumanne Murilo leo Alhamisi, Januari 2, 2025 wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu masuala mbalimbali ya usalama jijini Dar es Salaam.

Kamanda Murilo amesema madereva hao walikamatwa na jeshi hilo kabla na baada ya sikukuu ya Krismasi na mwaka mpya 2025.

Snapinsta.app_472409316_808426264750158_4060856391112666808_n_1080.jpg
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limewafungia leseni madereva 30 kati ya 179 waliokamatwa katika kipindi cha sikukuu za Krismasi na Mwaka Mpya 2025...

Ujifanya shughuli yoyote ambayo polisi hawa wana mamlaka juu yako "pole sana ndugu..!"
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limewafungia leseni madereva 30 kati ya 179 waliokamatwa katika kipindi cha sikukuu za Krismasi na Mwaka Mpya 2025.

Madereva hao 30 walikamatwa katika operesheni maalumu na walipopimwa walikutwa na ulevi kwa kiwago cha zaidi ya miligramu 80.

Soma Pia: Mbeya: Madereva wa mabasi ya New Force, Zanuni, Rungwe Express, Super Rojas, Abood Bus Service na Kyela Express wafungiwa leseni kwa muda


Hayo yamesemwa na Kamanda wa Kanda hiyo, Jumanne Murilo leo Alhamisi, Januari 2, 2025 wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu masuala mbalimbali ya usalama jijini Dar es Salaam.

Kamanda Murilo amesema madereva hao walikamatwa na jeshi hilo kabla na baada ya sikukuu ya Krismasi na mwaka mpya 2025.

View attachment 3190790
IGP, Toa maelekezo, ili Jeshi la polisi, Weka orodha ya majina ya madereva waliofungiwa hapa!
Wekeni tarehe waliyoanza kufungiwa na tarehe watakayofunguliwa ili rushwa isije kutumika, kuwafungulia.

Ikiwezekana pia,picha zao ziwekwe kwenye magazeti ,ili iwe mfano na onyo Kwa wengine!
 
Kwani wewe ni dereva wa basi?

Hao ni wasaka dau kubwa - huko Kwa kina katarama, new force, ally's na WA namna hiyo!
Ata hivi vidubwasha walisimamisha ile road ya Haile Sailasse mida ya saa 8-9 New Year eve sema mvua na jam ikawatoa maana njia ilisimama yoote
 
Ata hivi vidubwasha walisimamisha ile road ya Haile Sailasse mida ya saa 8-9 New Year eve sema mvua na jam ikawatoa maana njia ilisimama yoote

Ajali ipi wanazuia hao ndugu?

Nimewasikia wa mswada bungeni kulazimisha mikanda kwa abiria, kofia ngumu, seat belts provisions kwa watoto, fine zaidi nk Ili kudhibiti ajali.

Ajabu na kweli, hakuna neno lolote kuhusu barabara!



Bure kabisa!
 
Ajali ipi wanazuia hao ndugu?

Nimewasikia wa mswada bungeni kulazimisha mikanda kwa abiria, kofia ngumu, seat belts provisions kwa watoto, fine zaidi nk Ili kudhibiti ajali.

Ajabu na kweli, hakuna neno lolote kuhusu barabara!

View attachment 3190826

Bure kabisa!
Mkuu hawa jamaa wanakera sana. Kusema kweli trafiki polisi hawna msaada kwa watumia barabara ila kwa manufaa yao binafsi.

Ata haonwatunga sheria kazi ni kutunga adhabu tu sio kuongelea miundombinu mizuri.
 
Kwani wewe ni dereva wa basi?

Hao ni wasaka dau kubwa - huko Kwa kina katarama, new force, ally's na WA namna hiyo!
Hapo naona mlango mpya wa rushwa ukifunguka,kesi za kubambikia ili mlango huu mpya uwe wazi wakati wote.
 
Alafu kuna watu wanasema hawapendi siasa, siasa ndo inaendesha kila kitu kwenye maisha haya. Haya watuambie na Arusha wangapi walipimwa kilevi kwenye like tamasha la Makonda, maana pale asimilima kubwa walikuwa na vyombo vya usafiri na bia na vilevi vingine viliuzwa malori Kwa malori.
 
Back
Top Bottom