Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,267
Ni mechi ya kupindua matokeo na kufuzu hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika, leo Disemba 23, 2018 kwa wawakilishi wa Tanzania, Simba SC watakapokuwa wakikwaruzana na Nkana FC kutoka nchini Zambia katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Kaa pamoja na Timu ya JF kukuletea mtanange huu wa kukata na shoka kuanzia saa 10: 00 jioni. Usikose Ukaambiwa.
Wakati wowote mpira utaanza uwanja wa Taifa ni dakika 90 za mchezo Ligi ya Mabingwa Afrika
Naam mpira umeanza uwanja wa Taifa
Simba wameanza kwa kulishambulia lango la Nkana FC..ambapo shuti la Bocco linadakwa na golikipa wa Nkana FC
10' Ligi ya Mabingwa Afrika hakuna timu imepata bao
Simba 0-0 Nkana FC
17' Gooooooooaaal Walter Bwalya anaipatia Nkana FC bao la kwanza kwa kichwa kufuatia krosi iliyopigwa.
Simba imeamka inaamua kutumia mashuti ya mbali sasa
Simba SC 0-1 Nkana FC
Nyoni anajaribu kupiga shuti kali goo laaaa..Mpira unagonga mwamba na kurudi uwanjani.
Pamoja na kuwa nyuma ya bao moja bado Simba wanaliandama lango la Nkana FC
29' Gooooooooooaaal Gooooooooooaaal..Jonas Mkude anaisawazishia Simba bao kwa shuti la umbali mrefu na kwenda moja kwa moja wavuni na kumuacha golikipa wa Nkana Chibwe, akiruka bila mafanikio, kumbuka ni pasi safi kutoka kwa Cleoutus Chama
Simba SC 1-1 Nkana FC
Nkana wanajaribu kutumia mashambulizi ya kushtukiza hapa uwanja wa Taifa.
40' Ligi ya mabingwa Afrika uwanja wa Taifa, Simba wanapanga mashambulizi ya mara kwa mara langoni mwa Nkana
Simba 1-1 Nkana FC
45+2 kuelekea kuwa mapumziko Simba wanaliandama lango la Nkana huku Nkana wakijaribu kuzuia
45+1' Gooooooooooaaal Gooooooooooaaal Mk14 Mfumba Jicho Meddie Kagere anaipatia Simba bao la pili kwa kichwa safi kufuatia mpira wa Krosi ya Nicholas Gyan iliyotokana na kona fupi iliyopigwa na Cleoutus Chama
Simba SC 2-1 Nkana FC
Naaaaaaaam mpira ni mapumziko ambapo Simba wanatoka uwanjani wakiwa mbele ya mabao mawili dhidi Ya bao moja la Nkana FC
Kipindi cha pili kimeanza uwanja wa Taifa na hakuna mabadilko kwa pande zote mbili
Simba SC 2-1 Nkana FC
49' Simba wanapanga mashambulizi kuelekea lango la Nkana FC
Wanachukua Nkana sasa..Lakini wanapoteza anachukua Wawa upande wa Simba
Kona kuelekea lango la Nkana FC..Bocco gooo laaa, ilikuwa hatari lango la Nkana
53' Anatoka Nicholas Gyan anaingia Juuko upande wa Simba
57' mpira ni mkali kwa pande zote mbili..huku Simba wakihitaji goli moja tu kuweza kufuzu michuano hii ya mabingwa afrika.
87' Simba wanapoteza nafasi nzuri ya kufunga..ilikuwa ni hatari sana
88' Gooooooooooaaal Gooooooooooaaal
Mwamba wa Lusaka Cleoutus Chota Chama, Triple C, anaipatia Simba bao la tatu akipiga kwa kisigino kufutia pasi safi Hassan Dilunga hivyo kuihakikishia Simba inafuzu michuano hii Ligi ya Mabingwa ya Afrika
89' Ligi ya Mabingwa Afrika uwanja wa Taifa kuelekea kumalizika mchezo huu
Simba SC 3-1 Nkana FC
(Agg) 4-3
90+3' Naaaaaaaam mpira umekwisha uwanja wa Taifa. Simba wanaibuka kwa ushindi wa mabao matatu dhidi ya moja la Nkana FC
Kwa matokeo hayo Simba imefuzu hatua ya makundi katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwa jumla ya mabao manne kwa matatu kufuatia mechi ya kwanza iliyochezwa nchini Zambia ambapo Nkana FC waliibuka na ushindi wa mabao mawili kwa moja dhidi ya Simba SC
Simba SC 4-3 Nkana FC
Asante sana wote mlioshiriki hapa JF
Ghazwat...
SIMBA YAFUZU KUCHEZA MICHUANO YA KLABU BINGWA AFRIKA
Klabu ya Simba imefuzu kuingia hatua ya makundi michuano ya Klabu Bingwa Afrika baada ya kuifunga klabu ya Nkana FC ya Zambia goli 3-1
Magoli ya Simba yamefungwa na Mkude 29', Kagere 45+1' na Chama 88' huku goli la Nkana likifungwa na Bwalya 17'. Hivyo Simba inasonga kwa jumla ya magli 4-3
Timu kutoka Tanzania inafuzu kucheza Klabu Bingwa Afrika ikiwa ni baada ya miaka 15
Habari zaidi.
Dar es Salaam. Timu ya Simba imetinga hatua ya makundi michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kuifunga Nkana mabao 3-1 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Nkana imetolewa kwa jumla ya mabao ya mabao 4-3 huku ikiangukia kwenye Kombe la Shirikisho.
Licha ya kufunga bao lililoifanya Simba kuwa mbele ya Nkana Red Devels kipindi cha kwanza kwa mabao 2-1, mshambuliaji wa Simba, Meddie Kagere alipiga pasi nne.
Kagere ambaye mara kadhaa alikuwa akipoteza mipira ameifungia Simba bao hilo mwishoni mwa kipindi cha kwanza baada ya kuanzwa kwa kona fupi.
Simba ilianza kutanguliwa kwenye kipindi hicho cha kwanza kabla ya muda mchache baadaye kusawazisha kwa shuti kali la kiungo, Jonas Mkude.
Ndani ya dakika 45 za kipindi cha kwanza aliyrpiga pasi nyingi kwenye safu ya ushambuliaji ya Simba ni Mganda Emmanuel Okwi mwenye pasi 11, John Bocco alipiga sita zilizowafikia walengwa.
Aliyepiga pasi chache zaidi kwenye kikosi cha Simba ni mlinda lango wao, Aishi Manula ambaye ameruhusu nyavu zake kuguswa mara moja.
Kaa pamoja na Timu ya JF kukuletea mtanange huu wa kukata na shoka kuanzia saa 10: 00 jioni. Usikose Ukaambiwa.
Wakati wowote mpira utaanza uwanja wa Taifa ni dakika 90 za mchezo Ligi ya Mabingwa Afrika
Naam mpira umeanza uwanja wa Taifa
Simba wameanza kwa kulishambulia lango la Nkana FC..ambapo shuti la Bocco linadakwa na golikipa wa Nkana FC
10' Ligi ya Mabingwa Afrika hakuna timu imepata bao
Simba 0-0 Nkana FC
17' Gooooooooaaal Walter Bwalya anaipatia Nkana FC bao la kwanza kwa kichwa kufuatia krosi iliyopigwa.
Simba imeamka inaamua kutumia mashuti ya mbali sasa
Simba SC 0-1 Nkana FC
Nyoni anajaribu kupiga shuti kali goo laaaa..Mpira unagonga mwamba na kurudi uwanjani.
Pamoja na kuwa nyuma ya bao moja bado Simba wanaliandama lango la Nkana FC
29' Gooooooooooaaal Gooooooooooaaal..Jonas Mkude anaisawazishia Simba bao kwa shuti la umbali mrefu na kwenda moja kwa moja wavuni na kumuacha golikipa wa Nkana Chibwe, akiruka bila mafanikio, kumbuka ni pasi safi kutoka kwa Cleoutus Chama
Simba SC 1-1 Nkana FC
Nkana wanajaribu kutumia mashambulizi ya kushtukiza hapa uwanja wa Taifa.
40' Ligi ya mabingwa Afrika uwanja wa Taifa, Simba wanapanga mashambulizi ya mara kwa mara langoni mwa Nkana
Simba 1-1 Nkana FC
45+2 kuelekea kuwa mapumziko Simba wanaliandama lango la Nkana huku Nkana wakijaribu kuzuia
45+1' Gooooooooooaaal Gooooooooooaaal Mk14 Mfumba Jicho Meddie Kagere anaipatia Simba bao la pili kwa kichwa safi kufuatia mpira wa Krosi ya Nicholas Gyan iliyotokana na kona fupi iliyopigwa na Cleoutus Chama
Simba SC 2-1 Nkana FC
Naaaaaaaam mpira ni mapumziko ambapo Simba wanatoka uwanjani wakiwa mbele ya mabao mawili dhidi Ya bao moja la Nkana FC
Kipindi cha pili kimeanza uwanja wa Taifa na hakuna mabadilko kwa pande zote mbili
Simba SC 2-1 Nkana FC
49' Simba wanapanga mashambulizi kuelekea lango la Nkana FC
Wanachukua Nkana sasa..Lakini wanapoteza anachukua Wawa upande wa Simba
Kona kuelekea lango la Nkana FC..Bocco gooo laaa, ilikuwa hatari lango la Nkana
53' Anatoka Nicholas Gyan anaingia Juuko upande wa Simba
57' mpira ni mkali kwa pande zote mbili..huku Simba wakihitaji goli moja tu kuweza kufuzu michuano hii ya mabingwa afrika.
87' Simba wanapoteza nafasi nzuri ya kufunga..ilikuwa ni hatari sana
88' Gooooooooooaaal Gooooooooooaaal
Mwamba wa Lusaka Cleoutus Chota Chama, Triple C, anaipatia Simba bao la tatu akipiga kwa kisigino kufutia pasi safi Hassan Dilunga hivyo kuihakikishia Simba inafuzu michuano hii Ligi ya Mabingwa ya Afrika
89' Ligi ya Mabingwa Afrika uwanja wa Taifa kuelekea kumalizika mchezo huu
Simba SC 3-1 Nkana FC
(Agg) 4-3
90+3' Naaaaaaaam mpira umekwisha uwanja wa Taifa. Simba wanaibuka kwa ushindi wa mabao matatu dhidi ya moja la Nkana FC
Kwa matokeo hayo Simba imefuzu hatua ya makundi katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwa jumla ya mabao manne kwa matatu kufuatia mechi ya kwanza iliyochezwa nchini Zambia ambapo Nkana FC waliibuka na ushindi wa mabao mawili kwa moja dhidi ya Simba SC
Simba SC 4-3 Nkana FC
Asante sana wote mlioshiriki hapa JF
Ghazwat...
SIMBA YAFUZU KUCHEZA MICHUANO YA KLABU BINGWA AFRIKA
Klabu ya Simba imefuzu kuingia hatua ya makundi michuano ya Klabu Bingwa Afrika baada ya kuifunga klabu ya Nkana FC ya Zambia goli 3-1
Magoli ya Simba yamefungwa na Mkude 29', Kagere 45+1' na Chama 88' huku goli la Nkana likifungwa na Bwalya 17'. Hivyo Simba inasonga kwa jumla ya magli 4-3
Timu kutoka Tanzania inafuzu kucheza Klabu Bingwa Afrika ikiwa ni baada ya miaka 15
Habari zaidi.
Dar es Salaam. Timu ya Simba imetinga hatua ya makundi michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kuifunga Nkana mabao 3-1 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Nkana imetolewa kwa jumla ya mabao ya mabao 4-3 huku ikiangukia kwenye Kombe la Shirikisho.
Licha ya kufunga bao lililoifanya Simba kuwa mbele ya Nkana Red Devels kipindi cha kwanza kwa mabao 2-1, mshambuliaji wa Simba, Meddie Kagere alipiga pasi nne.
Kagere ambaye mara kadhaa alikuwa akipoteza mipira ameifungia Simba bao hilo mwishoni mwa kipindi cha kwanza baada ya kuanzwa kwa kona fupi.
Simba ilianza kutanguliwa kwenye kipindi hicho cha kwanza kabla ya muda mchache baadaye kusawazisha kwa shuti kali la kiungo, Jonas Mkude.
Ndani ya dakika 45 za kipindi cha kwanza aliyrpiga pasi nyingi kwenye safu ya ushambuliaji ya Simba ni Mganda Emmanuel Okwi mwenye pasi 11, John Bocco alipiga sita zilizowafikia walengwa.
Aliyepiga pasi chache zaidi kwenye kikosi cha Simba ni mlinda lango wao, Aishi Manula ambaye ameruhusu nyavu zake kuguswa mara moja.