Dar Village Project in Dar es Salaam


kigamboni kuna tamko ganilimetolewa tuna Ardhi zetu huko hatujui kinachoendelea
 

una tangible evidence gani kwa kweli kafulia, au maneno ya mitaani. jengo anajenga mkopo na yuko na washirika wake wa south africa
 
mkuu huko sahihi kabisa, tatizo serikali yetu haitaki kusikiliza wataalamu hasa wasomi ndio maana miradi mingi inaratibiwa tu kwa miinajili na matakwa ya wachache na wasio na ufahamu katika masuala husika.
 
kaka pesa za kumalizia ujenzi bado zinazungushwa kwenye uchaguzi, baada ya uchaguzi ndo litamaliziwa. Lakini hii ni siri usimwambie mtu nimewaonea huruma tu kuwaambia.

Teh teh teh teh!
 
du jamani kama na sisi wa huku bara tunasikia wanataka kuanzisha na Blue zone kwa kuwafukuza watu wote kigamboni na Project itachukua miaka 30 kweli hatujaliwa,
naomba mwenye data zozote za mradi huo wa kigamboni atumegee, maana nasikia itakuwa City ya kwanza Africa ikifuatiwa na Casablanca.
kule Dom UNIVERSITY(UDOM) nsikia amefanikiwa lakini haijulikani hizo pesa ni za Mifuko ya jamii wazee wetu waliokuwa wakikatwa na kina Mkullo billa ya riba au ni Bill Gate au ni huyo mwarabu.
mlioko jikoni mtueleze ni kweli kinaiva kwa ajili ya wote au kimeshaibiwa na moto kumwagiwa maji! hizi Project zitawafikia wajukuu wetu miaka ya hapo baadaye?
 
nadhani ameamua abaqne kwanza aangalie upepo wa uchaguzi. kwa pesa ipo si unaona mabango ya mgombea kila pahali - lazima atakuwa na mifedha mingi kutokana na haya mabango.
 
Labda kwa vile kuna watu humu (akiwemo GT) wanadai kuwa Tanzania ikijiunga na jumuiya ya kiislam itapata misaada kibao na umaskini utakwilia mbali.

Think Big?!!?

Uganda, mozambique +pakistani ni members wa oic; mbona juzi pakistan imepiga magoti kwa jumuiya za kimagharibi (imf, wb, eu, paris club) zisaidie kupambana na madhara ya mafuriko?, sina uhakika kama oic wako kiuchumi, nadhani wako ki imani zaidi.
 
Zadock anjipanga, iliamalizie project yake, kwa kawaida huwa hakubali kushindwa kwa urahisi.
 
Nashauri warudishie TTCL eneo lao basi , hapo hakuna kitu tena
 
Basi watakuwa wazembe kama wanaacha saiti wanaenda kwa mama nitilie, halafu wote kwa mara moja.
 
Zadock anajipanga, ili amalizie project yake, kwa kawaida huwa hakubali kushindwa kwa urahisi.

Tatizo ni roho mbaya ya viongozi walioko serikalini. Wakimwona Mwafrika ametajirika - bila kuiba - wanachanganyikiwa. Kama Zadock angekuwa Mhindi au Mzungu au Mwarabu haingekuwa na tatizo. Hii nchi ndivyo ilivyokuwa. Miafrika iliyoko Serikalini inaendeleza ubaguzi wa rangi DHIDI ya Waafrika wenzao na kupendelea wenye rangi nyeupe. Wewe ingia ofisi ya serikali halafu nyuma yako aje Mzungu au Mhindi au Mwarabu uone jinsi wanavyokudharau na kukuruka na kukimbilia yule wa ngozi nyeupe aliyeko nyuma yako. Hii nchi imekuwa miguu juu kichwa chini, yaani upside down, kwa muda mrefu na hiyo ni moja ya sababu kuu zinazokwamisha maendeleo yetu.

Hii project ya Rose Garden alianza kuipiga vita Magufuli hasa kwa sababu hiyo - kwamba ni Mwafrika alitaka kujenga shopping mall. Eh, yaani huyu Zadok, mtoto wa baba na mama wa Kiafrika anataka kulingana na wazungu, wahindi, waarabu wa Mlimani City, Shoppers Plaza au Haidari Plaza? Na Chuo Kikuu kikamtunukia digree ya heshima, inaelekea kwa kazi nzuri anayofanya ya kubomolea watu nyumba zao za kulala au za biashara huku akiwazulumu fidia zao na kuwazibia Waafrika wenzake wasitajirike - isipokuwa kwa kuiba - lakini kwa Wahindi, Wazungu na Waarabu, kutajirika ni halali yao. Yeye mwenyewe nasikia kajenga Kanisa huko kwao. Kwa hela aliyobana kwenye mshahara wake au?
 
nawasalimuni wakubwa, naomba kujulishwa juu ya hili:

Kwa wale wakazi wa Dar es Salaam na hasa maeneo ya Bagamoyo rd na mikocheni tulitangaziwa juu ya mradi wa mall ya DAR VILLAGE pale karibu na bar maarufu ya Rose Garden. Miongoni mwa wapangaji (kama sikosei) ilikuwa ni chain ya supermarkets moja kutoka Kenya.

  • Je, yupo anayejua mustababali (fate) ya hiyo project? Maana nimeona kama umesimama!
  • Je, inaweza ika justify "Is Tanzania 'almost' impossible to do business!??"

Nawakilisha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…