DOKEZO DAR: Vituo vya daladala Morogoro Road hakuna sehemu ya abiria kupumzikia

DOKEZO DAR: Vituo vya daladala Morogoro Road hakuna sehemu ya abiria kupumzikia

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Boran Jakutay

Senior Member
Joined
Apr 8, 2023
Posts
110
Reaction score
259
photo1689799092 (1).jpeg
photo1689799092.jpeg
NIMEKUWA nikiliona hili jambo kwa muda mrefu, nikaamua leo niliweke hapa pengine na wewe uliwahi kuliona lakini kama ukaona freshi tu.

Ukipita Morogoro Road, njia ambayo mabasi ya mwendokasi ndiyo yalianza kufanya kazi zake hapa Dar es Salaam, utagundua kwamba vituo vya daladala za kawaida ukiachana na mwendo kasi, hakuna sehemu ambayo abiria anaweza kusubiri daladala akiwa sehemu tulivu.

Vituo vyote katika barabara hiyo, hakuna sehemu ya abiria kupumzika kama ilivyo kwa vituo vingine vya Mandela Road, Nyerere Road, Kawawa Road, Bagamoyo Road.

Mvua ikinyesha, jua likiwaka, vyote vinaishia mwilini mwa abiria wakiwa wanasubiri gari.

Tunaomba mamlaka husika, liliangalie suala hili kwa sababu imekuwa kero ya muda mrefu.
 
Mtu unasafiri na usafiri bado unataka kituo cha kupumzika kama unatembea kwa mguu
 
Hii ni kweli kabisa alafu siyo kila mtu anapanda mwendokasi, kwanza sidhani kama zinatosha, ambacho hakijafanyika morogoro rd ni daladala za kawaida kujengewa stendi
 
MKUU KWANI HUJAJIONGEZA TU KUWA DALADALA ZA KAWAIDA HAZITAKIWI? NDIO MAANA UKIENDA KUOMBA NJIA UWEKE GARI WANAKATAA
 
Hata huku mikoani hakuna kabisa afadhari yenu mnavyo hata hivyo vichache
 
NIMEKUWA nikiliona hili jambo kwa muda mrefu, nikaamua leo niliweke hapa pengine na wewe uliwahi kuliona lakini kama ukaona freshi tu.

Ukipita Morogoro Road, njia ambayo mabasi ya mwendokasi ndiyo yalianza kufanya kazi zake hapa Dar es Salaam, utagundua kwamba vituo vya daladala za kawaida ukiachana na mwendo kasi, hakuna sehemu ambayo abiria anaweza kusubiri daladala akiwa sehemu tulivu.

Vituo vyote katika barabara hiyo, hakuna sehemu ya abiria kupumzika kama ilivyo kwa vituo vingine vya Mandela Road, Nyerere Road, Kawawa Road, Bagamoyo Road.

Mvua ikinyesha, jua likiwaka, vyote vinaishia mwilini mwa abiria wakiwa wanasubiri gari.

Tunaomba mamlaka husika, liliangalie suala hili kwa sababu imekuwa kero ya muda mrefu.
Tunakwenda kuondoa kabisa Daladala hizo barabara ndiyo maana hakujawekwa kwenye miradi.Hizo Daladala zimechelewa tu kuondolewa Morogoro road. Zamani vilikuwepo ila vilivunjwa .
 
Mtu unasafiri na usafiri bado unataka kituo cha kupumzika kama unatembea kwa mguu
kuna wagonjwa, kuna walemavu na wazee, kumbuka sio kila ukifika kituoni unapanda daladala hapohapo, kuna kusubiri ikitokea kuna shida ya usafiri.
 
Back
Top Bottom