AWESO AIPANGUA DAWASA, AIWEKA CHINI YA UANGALIZI MAALUM
Your browser is not able to display this video.
Waziri wa Maji, Jumaa Aweso amemtaka Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira (DAWASA), Kiula Kingu akae pembeni kwa muda, pia amemsimamisha kazi, Mkurugenzi wa Uzalishaji na Usambazaji Maji-DAWASA, Shaban Mkwanywe na kuanzia leo June 30,2024 ameiweka DAWASA chini ya uangalizi Wizara ili kuboresha utendaji wake kufuatia uzembe uliopelekea visima kukosa maji na kufanya Wakazi wa Dar es salaam kukosa maji.
Aweso ametangaza uamuzi huo leo baada ya kufanya ziara ya kimkakati na ya kushtukiza katika Ofisi za DAWASA zilizopo Ubungo Dar es salaam ili kupata maelezo ya Watendaji ya sababu za Watu kukosa maji na baada ya kushindwa kuridhishwa na majibu aliamua kuzungukia matanki ya maji katika maeneo manne tofauti ikiwemo la Ardhi UDSM na Kibamba huku akituma Timu nyingine kwenda kukagua matanki ya Kigamboni ambapo matanki hayana maji huku mengine yakiwa na maji kidogo ukilinganisha na mahitaji ya Wananchi huku Watendaji wa DAWASA wakishindwa kueleza sababu iliyopelekea uhaba huo wa maji.
Aweso amesema “Mwanzoni kulipokuwa kunakosekana maji tulikuwa tunasema shida ni vyanzo vya maji vimekauka hakuna maji, TANESCO umeme hamna lakini leo vyanzo vyote vina maji, umeme upo, niambieni kwanini hatuna maji kwenye matenki?, kwanini Wananchi wanateseka, wanalalamika wanapiga kelele kwenye Serikali?”
Ziara ya Aweso leo imekuja baada ya ziara ya Katibu Mkuu wa Maji aliyoifanya kwa siku mbili kujionea utendaji kazi wa DAWASA na hali ya upatikanaji wa maji ambapo amebaini uzembe aliouwasilisha kwa Waziri Aweso leo ikiwemo miundombinu ya maji kuwa chakavu, maji kupotea bila usimamizi, Watendaji wa DAWASA wa ngazi za chini kutopewa stahiki zao muhimu na kupelekea kufanya kazi bila hamasa nzuri na hata kupelekea kuwajibu vibaya Wateja, ziara hiyo ya Aweso na Katibu Mkuu itaendelea katika maeneo mbalimbali ya Nchi ili kuboresha upatikanaji wa maji.
Hii siyo dawa, dawa ni kujua chanzo cha tatizo tanzania haijawahi kuwa na proper water supply tangu na tangu miradi kibao inaletwa lakini dar kinachosaidia wananchi kuwa na uhakika wa maji ni visima
Mzizi wa tatizo haujang'olewa ambao ni kuruhusu sekta binafsi kuwekeza kwenye hii miradi inayogusa huduma muhimu za jamii moja kwa moja kama maji na umeme, hakuna nchi yoyote ambako serikali inafanya vizuri kwenye miradi inayoiendesha yenyewe.
Maji na umeme nimesema kwenye andiko langu la #STORIEOFCHANGE2024 kuwa "serikali iruhusu sekata binafsi kuwekeza kwenye sekta ya umeme na maji ili kuleta ushindani wa kihuduma"
ukisoma pale utaelewa nchi kama botswana ni jangwa lakini hujawahi kusikia kilio cha maji nchi kama misri wanatoa maji yao mto nile ambao kwa asilimia kubwa uko tanzania hakuna shida ya maji nchi kama dubai n.k hakuna shida ya maji kwasababu sekta binafsi zimepewa dhamana ya kuzalisha na kusambaza serikali ni mbia kupitia PPP lakini hii nchi sijui haya mashirika mawili kuna nini?
Leo nasikia tena wameongeza 500 kwenye kodi ya jengo kupitia luku yani kila mwaka wa fedha wanaongeza 500 ilianza 1000 ikaja 1500, leo 2000 🤣
MWANGALIENI USON ANASUTWA. HUYU WAZIR NI MWIZI NA MSANII NA TAPELI. KUNA MREJESHO ALIUTAKA HUKU DAWAS HAKUPEWA NDIO MAANA ANAJIDAI KUSHUGHULIKIA WATENDAJI
Akitoka kupumzika, kama soo ni kubwa sana, anahamishiwa kwingine. Mwanaharamu akishapita kombe linafunuliwa tena.
HAKUNA mtumishi wa umma hufukuzwa kazi kwa incompetence, utaratibu huo haupo vitabuni. Utumishi wa Umma ni ajira ya kudumu. Hii ndio misingi inayounda na ku define hizi Banana Republic zetu.
Ningetawala Banana Republic kama Tanzania ningefuta sheria moja tu, na ingetutoa: Permanence of public employment.
Akitoka kupumzika, kama soo ni kubwa sana, anahamishiwa kwingine. Mwanaharamu akishapita kombe linafunuliwa tena.
HAKUNA mtumishi wa umma hufukuzwa kazi kwa incompetence, utaratibu huo haupo vitabuni. Utumishi wa Umma ni ajira ya kudumu. Hii ndio misingi inayounda na ku define hizi Banana Republic zetu.
Ningetawala Banana Republic kama Tanzania ningefuta sheria moja, na ingetutoa tulipokwamia: Permanence of public employement.
MWANGALIENI USON ANASUTWA. HUYU WAZIR NI MWIZI NA MSANII NA TAPELI. KUNA MREJESHO ALIUTAKA HUKU DAWAS HAKUPEWA NDIO MAANA ANAJIDAI KUSHUGHULIKIA WATENDAJI
MWANGALIENI USON ANASUTWA. HUYU WAZIR NI MWIZI NA MSANII NA TAPELI. KUNA MREJESHO ALIUTAKA HUKU DAWAS HAKUPEWA NDIO MAANA ANAJIDAI KUSHUGHULIKIA WATENDAJI
Tangu huyu jamaa amesimamishwa maji yamekuwa bwerere kabisa mshikamano!
Huyu jamaa alikuwa na magari 2 ya maji na wenye malori walimtumia sana vibaya! Hongera Aweso, safi sana Mkuu
NIMESHANGAA sana kuwa makao makuu ya Dawasa yapo ubungo halafu wilaya ya ubungo ndiyo wilaya pekee mkoa wa Dar es salaam ambao haijaungwa na huduma ya maji.Huko misumi,mpiji, mbezi msakuzi ,makabe n.k hakuna hata bomba Moja la Dawasa.Halafu Kuna wapuuzi wanasema mama anaupiga mwingi.wananchi wa wilaya ya ubungo kunyweshwa maji ya mabowser ya magari yaliyochotwa mtoni ndiyo kuupiga mwingi?
Huyu Eng. angeswekwa ndani tu , kwa kuhujumu wananchi na kupokea mshahara bila kujua majukumu yake😡😡 pia tujue elimu yake maana anaonekana hajui hata majukumu yake.inasikitisha sana,hata bodi inatakiwa uvunjwe, tanki la ltrs milioni 40 halina hata tone la maji👹