Daraja la jp magufuli (kigongo-busisi ) lafikia asilimia 96.3, kukamilika februari 2025

Daraja la jp magufuli (kigongo-busisi ) lafikia asilimia 96.3, kukamilika februari 2025

Venus Star

JF-Expert Member
Joined
Dec 6, 2018
Posts
26,519
Reaction score
78,311
Waziri wa Ujenzi Abdallah Ulega amesema Daraja la JP MAGUFULI (Kigongo-Busisi), linalounganisha mkoa wa Mwanza na Geita, linatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Februari mwaka huu.Akikagua Ujenzi wa Daraja hilo leo tarehe 24 Januari 2025 mkoani Mwanza, Waziri Ulega amemshukuru na kumpongeza Rais wa Jamhuri ya

Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa zaidi ya shilingi bilion 611 kugharamia daraja hilo hadi sasa.


View: https://youtu.be/2X2mAhcsi0I?si=bFR7smY17nKI01dE

Mradi wa kihistoria wa ujenzi wa Daraja la JP Magufuli (Kigongo-Busisi) unaendelea kusonga mbele kwa kasi kubwa, ambapo hadi sasa umefikia asilimia 96.3 ya utekelezaji wake. Daraja hili linatarajiwa kukamilika ifikapo Februari 2025.

Daraja hili, ambalo litakuwa refu zaidi katika Ukanda wa Afrika Mashariki likiwa na urefu wa kilomita 3.2, limekuwa mkombozi mkubwa kwa wakazi wa mikoa ya Mwanza na Geita na maeneo ya jirani. Kwa sasa, wananchi wanategemea huduma za kivuko ambazo zimekuwa changamoto kubwa hasa wakati wa msongamano wa magari na mizigo.

Lengo kuu la mradi huu ni kuhakikisha kuwa mawasiliano kati ya mikoa ya Kanda ya Ziwa yanaboreshwa, kupunguza gharama za usafirishaji, na kuongeza kasi ya maendeleo ya kiuchumi kwa maeneo yanayohusika.
 
Faida za Daraja la JP Magufuli:

  1. Kupunguza muda wa kuvuka kutoka Kigongo hadi Busisi kwa dakika chache tu badala ya kutumia kivuko.
  2. Kuimarisha biashara na uwekezaji kwa kurahisisha usafirishaji wa bidhaa.
  3. Kukuza utalii, hususan katika Hifadhi ya Serengeti na maeneo ya Kanda ya Ziwa.
  4. Kuboresha maisha ya wananchi kwa kuondoa changamoto za usafiri wa kivuko.
Mradi huu unaendelea kuwa kielelezo cha maono makubwa ya marehemu Dkt. John Pombe Magufuli, ambaye alisisitiza ujenzi wa miradi mikubwa ya maendeleo inayowanufaisha wananchi moja kwa moja.

Wananchi wanaendelea kushuhudia hatua kwa hatua maendeleo haya makubwa, huku wakisubiri kwa hamu kuona daraja hili likikamilika na kuanza kutumika rasmi.

#DarajaLaKigongoBusisi
#MiradiYaKimkakati
#MaendeleoKwaVitendo
 
RIP JPM, maono na uthubutu wako vimefungua macho watanzania kujua haya mambo ni mepesi na yanaweza kufanyika Kwa haraka sana kama watu wataacha wizi, rushwa na kuwafikiria watanzania zaidi kuliko matumbo yao, familia zao na circle zao.
 
Napinga wafuasi wa Chadema kupita kwenye hilo daraja
 
daraja lina urefu wa KM 3.2 ..hivi wakuu pale toka Kigamboni hadi magogoni pana KM ngapi hadi kunashindikana kuweka daraja kama la Busisi.! au ndio viongozi hawana dira wala maono kama JPM wanaangalia matumbo yao
 
Tunachotaka ni Tume huru na Katiba mpya kabla ya Uchaguzi wowote.

Tukipata hayo, madaraka yatauwa kama New York vile, Si hili Moja pekee.
 
Tunachotaka ni Tume huru na Katiba mpya kabla ya Uchaguzi wowote.

Tukipata hayo, madaraka yatauwa kama New York vile, Si hili Moja pekee.
Mnataka wewe na nani? 🤣 🤣 🤣 Na Lisu au?
 
daraja lina urefu wa KM 3.2 ..hivi wakuu pale toka Kigamboni hadi magogoni pana KM ngapi hadi kunashindikana kuweka daraja kama la Busisi.! au ndio viongozi hawana dira wala maono kama JPM wanaangalia matumbo yao
Hapo Meli zinapita kijana wangu kuelekea bandarini. Au hujui hilo?
 
Waziri wa Ujenzi Abdallah Ulega amesema Daraja la JP MAGUFULI (Kigongo-Busisi), linalounganisha mkoa wa Mwanza na Geita, linatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Februari mwaka huu.Akikagua Ujenzi wa Daraja hilo leo tarehe 24 Januari 2025 mkoani Mwanza, Waziri Ulega amemshukuru na kumpongeza Rais wa Jamhuri ya

Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa zaidi ya shilingi bilion 611 kugharamia daraja hilo hadi sasa.


View: https://youtu.be/2X2mAhcsi0I?si=bFR7smY17nKI01dE

Mradi wa kihistoria wa ujenzi wa Daraja la JP Magufuli (Kigongo-Busisi) unaendelea kusonga mbele kwa kasi kubwa, ambapo hadi sasa umefikia asilimia 96.3 ya utekelezaji wake. Daraja hili linatarajiwa kukamilika ifikapo Februari 2025.

Daraja hili, ambalo litakuwa refu zaidi katika Ukanda wa Afrika Mashariki likiwa na urefu wa kilomita 3.2, limekuwa mkombozi mkubwa kwa wakazi wa mikoa ya Mwanza na Geita na maeneo ya jirani. Kwa sasa, wananchi wanategemea huduma za kivuko ambazo zimekuwa changamoto kubwa hasa wakati wa msongamano wa magari na mizigo.

Lengo kuu la mradi huu ni kuhakikisha kuwa mawasiliano kati ya mikoa ya Kanda ya Ziwa yanaboreshwa, kupunguza gharama za usafirishaji, na kuongeza kasi ya maendeleo ya kiuchumi kwa maeneo yanayohusika.

Kama wameweza kujenga daraja la km 3.2 wanashindwaje kujenga daraja la kigamboni to magogoni?
 
Hapo Meli zinapita kijana wangu kuelekea bandarini. Au hujui hilo?
ni kweli meli zinapita lakini si lazima daraja likae kati kati linatafutiwa sehemu pembeni eneo lisilo na ubize wa meli au daraja linyanyuliwe juu alafu meli zinapita chini ya daraja au kama vp lijengwe lingine mkabala kwa pembeni yake na lile daraja la kigamboni(tanzanite) kwani jambo kubwa la muhimu ni watu kuvuka tu upande wa pili na kama hawawezi hilo basi serikali iongeze vivuko badala ya hivi viwili chakavu vya sasa watu wanabanana mno viwe angalau vinne..angekuwepo JPM asingekosa solution ya maana hapo kigamboni
 
Waziri wa Ujenzi Abdallah Ulega amesema Daraja la JP MAGUFULI (Kigongo-Busisi), linalounganisha mkoa wa Mwanza na Geita, linatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Februari mwaka huu.Akikagua Ujenzi wa Daraja hilo leo tarehe 24 Januari 2025 mkoani Mwanza, Waziri Ulega amemshukuru na kumpongeza Rais wa Jamhuri ya

Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa zaidi ya shilingi bilion 611 kugharamia daraja hilo hadi sasa.


View: https://youtu.be/2X2mAhcsi0I?si=bFR7smY17nKI01dE

Mradi wa kihistoria wa ujenzi wa Daraja la JP Magufuli (Kigongo-Busisi) unaendelea kusonga mbele kwa kasi kubwa, ambapo hadi sasa umefikia asilimia 96.3 ya utekelezaji wake. Daraja hili linatarajiwa kukamilika ifikapo Februari 2025.

Daraja hili, ambalo litakuwa refu zaidi katika Ukanda wa Afrika Mashariki likiwa na urefu wa kilomita 3.2, limekuwa mkombozi mkubwa kwa wakazi wa mikoa ya Mwanza na Geita na maeneo ya jirani. Kwa sasa, wananchi wanategemea huduma za kivuko ambazo zimekuwa changamoto kubwa hasa wakati wa msongamano wa magari na mizigo.

Lengo kuu la mradi huu ni kuhakikisha kuwa mawasiliano kati ya mikoa ya Kanda ya Ziwa yanaboreshwa, kupunguza gharama za usafirishaji, na kuongeza kasi ya maendeleo ya kiuchumi kwa maeneo yanayohusika.

Hongera kwa Ilani ya uchaguzi ya CCM 2020-2025, hongera JPM, hongera sana SSH kwa utekelezaji wa Ilani ya CCM na kukuza uchumi wa kanda ya ziwa kupitia daraja hili. Watu wa kanda ya ziwa tunashukuru sana na tunadaiwa na CCM.
 
Back
Top Bottom