Daraja linalounganisha Kata ya Lemara na Sinoni ni miaka minne sasa hakuna mawasiliano

Daraja linalounganisha Kata ya Lemara na Sinoni ni miaka minne sasa hakuna mawasiliano

Bushmamy

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2019
Posts
9,140
Reaction score
15,963
Wananchi wa kata ya Lemara na Sinoni mkoani Arusha katika wilaya ya Arusha wamekosa mawasiliano kwa kipindi cha miaka minne tangu daraja linalounganisha Kata ya Themi Lemara na Sinoni lisombwe na mvua.

Kwa muda wote huo wananchi wamekuwa wakilalamika wawekewe daraja lakini viongozi kutoka serikali za mitaa walikuja mara moja kuangalia na hawakurudi tena na wananchi hawajui kinachoendelea hadi sasa.

Kipindi cha mvua ambako maji ni Mengi kuna watu hujitolea na kuweka daraja la mianzi na hivyo wananchi hao hulipia sh mbili( 200) kuvuka,hivyo basi kwenda na kurudi hutumia Mina nne(400) .
Na kipindi ambacho sio cha mvua basi wananchi hulazimika kuruka juu ya mawe ili kuvuka ng'ambo ya pili.


Daraja hili ni kiunganishi muhimu sana kutokana na kwamba kata ya Themi na Lemara ndiko kuliko na idadi kubwa ya shughuli za Kiuchumi kama vile viwanda hivyo hivyo basi idadi ya wananchi wanaovuka kutoka Sinoni kuelekea katika Kata za Themi na Lemara.

IMG-20211113-WA0054.jpg
mmoja wa wananchi akikatiza katika mto huo kutokea kata ya Lemara kuelekea kata ya sinoni
IMG-20211113-WA0063.jpg
IMG-20211113-WA0061.jpg


DSC_0799.JPG


DSC_0789.JPG


IMG-20211113-WA0055.jpg
 
Haya wakazi wa Lemara na Sinoni mje huku.

Sisi ambao sio wakazi wa huko tumenyimwa hata haki ya kupajua hiyo Sinoni na Lemara ipo Mkoa gani na Nchi gani
 
Bahati yako, Don nimefungua huu uzi na ku-comment, imeisha hiyo, wiki tu daraja mtaliona hapo.
 
Technically huwezi kuliita hilo daraja..., Sema lililokuwa Daraja miaka minne iliyopita...
 
Haya wakazi wa Lemara na Sinoni mje huku.

Sisi ambao sio wakazi wa huko tumenyimwa hata haki ya kupajua hiyo Sinoni na Lemara ipo Mkoa gani na Nchi gani
Arusha mkuu
 
Wananchi wa kata ya Lemara na Sinoni mkoani Arusha katika wilaya ya Arusha wamekosa mawasiliano kwa kipindi cha miaka minne tangu daraja linalounganisha Kata ya Themi Lemara na Sinoni lisombwe na mvua.

Kwa muda wote huo wananchi wamekuwa wakilalamika wawekewe daraja lakini viongozi kutoka serikali za mitaa walikuja mara moja kuangalia na hawakurudi tena na wananchi hawajui kinachoendelea hadi sasa.

Kipindi cha mvua ambako maji ni Mengi kuna watu hujitolea na kuweka daraja la mianzi na hivyo wananchi hao hulipia sh mbili( 200) kuvuka,hivyo basi kwenda na kurudi hutumia Mina nne(400) .
Na kipindi ambacho sio cha mvua basi wananchi hulazimika kuruka juu ya mawe ili kuvuka ng'ambo ya pili.



Daraja hili ni kiunganishi muhimu sana kutokana na kwamba kata ya Themi na Lemara ndiko kuliko na idadi kubwa ya shughuli za Kiuchumi kama vile viwanda hivyo hivyo basi idadi ya wananchi wanaovuka kutoka Sinoni kuelekea katika Kata za Themi na Lemara ni kubwa.

712447EE-42AF-4334-B0BD-A52718280D3B.jpeg
 
Niliwahi kukaa hapo lemara nikiwa nasoma chuo cha uhasibu pale njiro IAA, vituko vya wanga usiku vilinikimbiza, sikutegemea ntakutana na hizi ishu Arusha
 
Back
Top Bottom