Dark days 17/03/20...

Yaani kauli za hawa wazee zinatia shaka sana. JK alisema mambo yakiwa kama ilivyo sasa, je maana yake nini? Je kuna mtu kaandaliwa kwa sababu Rais Samia watu kwa sasa hawampendi na wanajua? Akaja Makamba akamaliza kabisa eti Rais Samia akifa Mwenyezi Mungu ataleta mgombe mzuri mwingine. Ila mi Rais Samia pamoja na ulegevu wake kwenye kusimamia Rasimali za nchi ila bora tuendelee naye anayo nafasi ya kujirekebisha kuliko kuanza na mtu mwingine.
 
Yaani mpaka sasa wanajua kabisa Rais Samia keshaharibikiwa, hakuna anayetamani huku mitaani kusikia jina la Rais Samia, na ndiyo maana wazee wamemuonya kishikaji mpaka kumtabiria kifo. Rais Samia angekuwa na uwezo wa kutembelea JF na kusoma nyuzi zetu naamini Makamba asingekuwa waziri, Nape angekuwa keshafukuza na Mwigulu angekuwa Jela na mambo yake Rais Samia yangekuwa bomba. Ila sasa sijui hilo baraza litakuwaje, hatujui kama ata recycle walewale. Natamani kuona kabisa Nape, January na Mwigulu awatoe baraza la Mawaziri, ateue watu makini kwenye hizo nafasi tena wawe na historical background ya utendaji mzuri.
 
Hana uwezo wa kuwatoa hao vijana watatu kwa mpigo.
 
Hao watu ndio wanamchafua? Una uhakika wakitolewa hao "hali" itakuwa kama hivyo unavyofikiria? Je hao "wazee" wanapendelea "hali" ipi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…