Dark days 17/03/20...

Wapo wanaouliza 'Kura ya Maoni ' itawezekana vipi ikiwa kikatiba haipo kwa suala la Muungano!
Katiba ya 1977 imefanyiwa mabadiliko mara nyingi kukidhi haja ya wakati. Kwa mfano, kuondoa nafasi ya Makamu wa kwanza na wa pili wa Rais ,wepo wa vyama vingi n.k.

Katiba ya Zanzibar ya 1984 imefanyiwa mabadiliko 2010 na kuondoa baadhi ya vifungu vikiwemo vinavyogusa katiba ya JMT. Kwa mfano, kuondoa nafasi ya Waziri kiongozi na kuweka makamu wawili na uwepo wa serikali ya Kitaifa

Mabadilio ya Katiba ya 1984 ya Zanzibar toleo la 2010 yamefanyika na kuidhalilisha ile ya JMT.
Kwa mfano, Katiba ya Zanzibar inasema , sheria itakayotungwa na bunge la JMT lazima kwanza ipitishwe na Baraza la wawakilishi. Tukumbuke kuna Wabunge wa Zanzibar katika Bunge la JMT na kuna Wabunge 5 kutoka Baraza la wawakilishi ndani ya Bunge la JMT. Ulazima wa kupitisha sheria mara mbili unatoka wapi?

Hoja ni kwamba upo uwezekano wa SMZ kupeleka mswada wa Kura ya Maoni ndani ya Baraza la Wawakilishi kuhusu Muungano na ikakubaliwa , na Wabunge wa Zanzibar kutumia 2/3 ndani ya Bunge la JMT kutaka mabadiliko ya sheria yatakayoruhusu kura ya maoni.

Katiba si vitabu vitakatifu, ni maandiko yanayoweza kubadlilishwa kulingana na nyakati.

Hatuwezi kuepuka kura ya maoni kwasababu Muungano unahitaji stability kama utakuwepo na njia ya lazima ni kura ya maoni Wazanzibar waamue hatma yao. Ikiwa wataamua kuondoka , tutakutana EAC na SADC n.k.
 
Kwa vyovyote vile Zanzibar inabidi iwe na mikoa maalumu ndani ya Tanzania ili kuwavunja nguvu kabisa ya ubinafsi kuwe na mikoa miwili ya Zanzibar na Pemba kabisa ili kuondoa hii hali ya Serikali mbili ndani ya Nchi Moja, kipimo cha Rais bora ni yule atakayeweza kufanya Nchi kuwa Moja yaani serikali Moja kamili bila fikra za uzanzibari tena maana utanganyika ulishakufa Sasa kazi ya kiongozi hodari ni kuua uzanzibari, bila kuua uzanzibari hakuna Utanzania, hivyo kwa maoni yangu, Uzanzibari ni adui mkuu wa taifa la Tanzania kwa sababu umebeba ubinafsi, uchoyo, dharau, kiburi, majivuno na nyodo dhidi ya watanganyika, Sasa Zanzibar lazima waamue either serikali Moja au waende kivyao.
NB: Anayepoteza nafsi yake kwa ajili ya Mungu (Umoja) ataiokoa (Tanganyika), Anayeiokoa nafsi yake kwa ajili ya ubinafsi wake ( Utengano) ataipoteza (Zanzibar).
 
Kabla ya kuungana mwaka 1964 Tanganyika ilikuwa na mipaka yake.
Sijaona hoja hapa labda unifafanulie zaidi tafadhali
Tanganyika ina mipaka yake ya baharini hata kabla ya kuungana na Zanzibar, je gharama za kulinda mipaka ya bahari ya Tanganyika nje ya Muungano na gharama za kuhudumia Muungano ipi gharama zaidi?
 
Tanganyika ina mipaka yake ya baharini hata kabla ya kuungana na Zanzibar, je gharama za kulinda mipaka ya bahari ya Tanganyika nje ya Muungano na gharama za kuhudumia Muungano ipi gharama zaidi?
Hakuna gharama itakayoongezeka au kupungua. Mpaka kabla ya Muungano ulianza Tanga hadi Mtwara ukiwa na visiwa vya Mafya na bahari kuu. Baada ya Muungano ukashirikisha visiwa vya Zanzibar mbele.

Vifaa na askari wanaotumika sasa hivi watapunguza wigo lakini si kifaa au rasilimali watu.
 
Sawa kiongozi shukurani, maana niliwahi kumsikia Zitto akisema "kuwa kwenye muungano ni nafuu kuliko kuwa nje ya muungano, gharama za kulinda mipaka ni kubwa"
Kwamba itabidi uwe na Submarine, nyaya za baharini na nyenzo nyinginezo
 
mkuu nadhani hoja hapa si ghalama au nani ananufaika au anapoteza hzo ni hoja za nje tu kiini chenyewe kabisa kabisa Cha Zanzibar kuwa sehem ya Tanganyika ni USALAMA,

Kwa nini ni usalama

mwalim hakuishia kuona tu wapi alipo ila aliona mbali Sana kwamba ikiwa visiwa Vya Zanzibar vitakuwa chini yake yenyewe Kwa mamlaka kamili ya kiutendaji na kiuendeshaji, basi kunasiku sisi tutakuwa mateka mchana kweupeee

maana adui atatumia Rafiki alie karibu nawe kukupiga, tizama vizri kijoografia angalia, mafia, Pemba na unguja nenda mpka juu Pale ramu kama sikosei hivi ni visiwa Vya kimkakati, kwa hyo mwl alipotengeneza hesabu akaona kabisa ili niitawale nchi vzr visiwa vyote hvi viwe chini yake

isivyo bahati akakikosa hicho cha juu kabisa, sasa ikawa si kesi, kesi yake kubwa ikawa nawezaje kuvitawala?

mwalim alikuwa very interrigent akamsoma vzr karume akaenda na proposal yake akatengeneza ndoa Tena isiyovunjika na mwisho mkataba ukawa Siri Tena uko UN

Kwa hyo kilichobaki ni Tanganyika kuihudumia Zanzibar na visiwa vyake wether wametaka au hajataka, au wanaumia au hawaimii ni ndo ya kikiristo Mke na mme1 mpka kifo kiwatenganishe..

haya mambo yanazagazaga mengi ndipo yakaibuka mambo ya mwenge WA uhuru sijui rais kuchaguliwa kutoka Dodoma, na kuanzia hapo Zanzibar hawajawahi kuwa huru kabisa, hawawezi kujiamulia wao Nan awe rais wao, au wanatumia Pesa yao, au wawe na keshi lao haitiwezekana..

Kwa hyo watabaki kuwa Rais wa kupitishwa na NEC, watabaki kuwa mawazr, na makamu wa rais, wakipata nafasi kuwa Rais, ila hawawezi kubadili chochote hyo imeisha hapo..

msingi ni kuwa mfumo wa ujamaa uliopo na mixed economy unawaziba masikio na meno, maana wanajikuta wananyumba Masaki, au eneo lolote tz hao viongozi wote wa juu...

mambo ni mengi ila tu serikal 3 haziwezekani Wala 1 ila huu muundo wa sasa ndyo suluhisho, tumetaka au hatujataka.

B

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sawa kiongozi shukurani, maana niliwahi kumsikia Zitto akisema "kuwa kwenye muungano ni nafuu kuliko kuwa nje ya muungano, gharama za kulinda mipaka ni kubwa"
Kwamba itabidi uwe na Submarine, nyaya za baharini na nyenzo nyinginezo
Ni maneno tu ya watu katika kubabaisha Umma. Hata sasa hivi tuna vitu hivyo kwasababu bahari ipo na wala haihami asilani. Kitakachotokea ni kwamba Tanganyika italinda mipaka yake kama ilivyo sasa kuanzia kaskazini hadi kusini na bahari kuu na visiwa vyake. Zanzibar ambayo haina gharama za Ulinzi ndio itabidi iwe na vitu hivyo, hapo ndipo watu wanaficha ukweli. Kwamba, Tanganyika haina gharama hata senti tano wala haitapunguza gharama nukta.

Zanzibar itakuwa na mipaka , jeshi na vifaa jambo ambalo sasa hawana ndio maana wanaweza kulipa Wazee pensheni hata kama hawakuwahi kufanya kazi.
 
Sawa mkuu shukurani sana.
 
mkuu nadhani hoja hapa si ghalama au nani ananufaika au anapoteza hzo ni hoja za nje tu kiini chenyewe kabisa kabisa Cha Zanzibar kuwa sehem ya Tanganyika ni USALAMA,
Kwa wakati huo lakini si usalama wa Tanganyika tu bali pia usalama wa Zanzibar kama tutakavyoona baadaye
Si kweli kwasababu adui huyo angetumia Rwanda, Burundi , Malawai n.k. Kumbuka Tanganyika ina mipaka na nchi 8
mwalim alikuwa very interrigent akamsoma vzr karume akaenda na proposal yake akatengeneza ndoa Tena isiyovunjika na mwisho mkataba ukawa Siri Tena uko UN
Hapana! unakosa point, ni kinyume chake. Kwamba Karume alikuwa under pressure ya Umma Party ya Abraham Babu. Kuna wakati Tanganyika ilibidi ipeleke askari 300 na Karume alipoleta jeuri Nyerere akatishia kuondoa majeshi.
Hii ni kwa ufupi , ni kisa kikubwa lakini elewa kwamba aliyeomba Muungano ni Karume '' Wewe ni Rais mimi ni Makamu' alisema Karume
mambo ni mengi ila tu serikal 3 haziwezekani Wala 1 ila huu muundo wa sasa ndyo suluhisho, tumetaka au hatujataka.
Kwanini Serikali 3 haiwezekani? Hapa ndipo tunahitaji utusaidie. Kwanini Muundo wa sasa unaosema ni suluhisho bado una matatizo tunayoyaon!
 
Si kweli kwasababu adui huyo angetumia Rwanda, Burundi , Malawai n.k. Kumbuka Tanganyika ina mipaka na nchi 8

Mkuu kijiografia zanzibar imekaa vibaya zaidi ukilinganisha na majirani wengine. Naona huu muungano waliangalia sababu kadhaa ila shabaha kubwa ilikua ni usalama.

Kuhusu Rwanda mimi nadhani ni suala la muda tu, inawezekana maadui kwa wakati huu hawajaona potential yoyote kwetu, kuna nyakati kama tutapishana saana ideology na ki-maslahi na wakubwa wetu, kunauwezekano zengwe likatokea.

Rwanda mimi hua nahisi ni monitor wa wakubwa kwa ukanda wetu huu wa A. Mashariki na kati, kama ambavyo hua nahisi Israel na Middle East pale.
 
Smartkahn kuhusu Rwanda kama kuna ukweli fulani, namna ambavyo anaipelekesha Congo hadi unashangaa kabisa.
 
Sawa kiongozi shukurani, maana niliwahi kumsikia Zitto akisema "kuwa kwenye muungano ni nafuu kuliko kuwa nje ya muungano, gharama za kulinda mipaka ni kubwa"
Kwamba itabidi uwe na Submarine, nyaya za baharini na nyenzo nyinginezo
Ukizingatia hiyo hoja ya zitto ni nzito imejikita kwenye athari zitakazojitokeza baada yakuwa nje ya muungano,,
 
Mkuu kijiografia zanzibar imekaa vibaya zaidi ukilinganisha na majirani wengine. Naona huu muungano waliangalia sababu kadhaa ila shabaha kubwa ilikua ni usalama.
Tuna mpaka mrefu sana na Kenya katika nchi tunazopakana. Tuna mpaka na Msumbiji, Congo, na nchi nyingine
Tushawishi kwanini unadhani Zanzibar imekaa vibaya. Ni kwa usalama upi
Kuhusu Rwanda mimi nadhani ni suala la muda tu, inawezekana maadui kwa wakati huu hawajaona potential yoyote kwetu, kuna nyakati kama tutapishana saana ideology na ki-maslahi na wakubwa wetu, kunauwezekano zengwe likatokea.
Tulioishi wakati wa ' frontline states' na mapigano ya kudai Uhuru kwa nchi za kusini mwa Africa hatuoni tishio lolote la nchi jirani. Hata hivyo nakubaliana nawe kwamba 'Intelligence' tuliokuwa nayo si hii ya sasa hivyo kuwa vulnerable na nchi yoyote ni kitu possible. Hapa si suala la mipaka ni suala la 'Intelligence'
Rwanda mimi hua nahisi ni monitor wa wakubwa kwa ukanda wetu huu wa A. Mashariki na kati, kama ambavyo hua nahisi Israel na Middle East pale.
You never know! Mbona kuna Marine base kubwa sana pale Lamu Kenya? Kwanini usiwe suspicious
Kuna Embassy Kubwa Sub sahara pale Dar es Salaam , kwanini usiwe suspicious kama unavyohisi Rwanda

Hoja ya ulinzi na usalama kama sababu za Muungano, ilikuwepo, HAIPO kwasasa. Dunia imebadilika sana
Ni kama hoja ya kuwa na makao Makuu Dodoma kwasababu za usalama, si kweli!

Kama wapiganaji wa Houth wakiwa Yemen wanaweza kutuma kitu Tel Aviv, wewe hapo Dodoma una nini cha kuzuia? Mizabibu!
 
Ukizingatia hiyo hoja ya zitto ni nzito imejikita kwenye athari zitakazojitokeza baada yakuwa nje ya muungano,,
Mbona hamuelezi athari hizo? Tusaidieni sisi tuisoona uzito wa hoja.

Tunatishana tishana tu bila hoja, tafadhalini njooni tuzungumze

1. Muundo wa Serikali ya sasa ni 'mzuri'. Tuelezeni malalamiko yanatoka wapi ikiwa ni mzuri?
2. Serikali 3 zina gharama, tuonyesheni wapi gharama zinaongezeka , kwa eneo gani na watu gani!
3. Kuna suala la Usalama, tuelezeni kwa lipi na kwanini isiwe nchi 8 tulizo na mpaka nazo bila bahari
 
Kwa nini isiwe serikali moja?.

Kero zitakuwepo tu hata pawe na serikali saba

Taifa la Afrika limegawanywa vipande vipande huku kila kipande kikiwa na serikali yake iliyo tofauti na kipande kingine.

Ikiwa ni moja wote tukaongea lugha moja, tukaelewana ule umoja ambao ndio nguvu ya kushinda ujinga, magonjwa na umasikini utaleta matokeo.

AFRIKA UNITE (You Night)
 
Daaah! Umesoma maandiko yote Nguruvi aliyo andika juu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…