uchumi2018
JF-Expert Member
- Mar 4, 2018
- 1,657
- 2,406
Rabbon, Rabonn ,rabon, yupi kati ya hao ulimaanisha.Wakuu hili suala la muungano linaumiza sana hisia za watu hasa ukizingatia vifungu vilivyochambuliwa na wadau hapo juuπ na kina NGURUVI, Nguruvi3.
Kiukweli hizi kasoro zinachoma, more painful kwa sisi watu wa bara huku, yaani hapa kifua kinafurukuta kwa gadhabu ile mbaya! Ila hii hali naitafsiri kama hisia(emotions) tu, ni kweli vitu kwa ground vipo hivyo lakini tusichukue maamuzi magumu kwa msisimko wa hisia kwa ambavyo vinarekabisika. Hili dude linahitaji strategic plans makini sana & in a diverse way zitakazo angazia hatima ya vizazi vijavyo.
Intelligence will... katika hili naona itakua positive na ita-make sense kama itachagua kudumisha muungano, na pengine muungano upo hadi leo kwa sababu ya hihi intelligence... waliona ni busara zaidi kuriko usiwepo.
Pendekezo langu ni kwamba tusijikite kuuvunja bali tujikite kuuimarisha huu muungano kwa;
1) Kuboresha vifungu vinavyotafrika kama kero za muungano kuendana na hali halisi ili muundo wa serikari mbili ama tutu uweze kua na afya zaidi pande zote. Haya mabadiliko yaanzie kwenye sheria mama na yasomane mpaka kwenye sheria za serikali zote.
3) Muundo wa serikali mbili uondolewe uletwe muundo wa serikari moja usio na MAKANDOMAKANDO/KONAKONA WALA (MBA)3 = MBAMBAMBA, yaani nchi inakua ya serikali moja JMT, harafu Kagera Kigoma Mtwara Tanga Zanzibar Dar es salaam nk... Inakua mikoa na mapato yatagawanywa kulingana na potential iliyopo mkoa husika.
Huu upande wa pili wa shilingi ni fikra zangu binafsi usizingatie saana.πππ
Kuna watu wanaishi kwenye familia mambo safi mahitaji yanapatikana kwa wakati wazazi wao wananguvu ya kiutawala na uchumi yaani wanaheshimika mtaani kwao, sasa hawa watoto ama wajukuu wanawaona walala hoi kama wazembe hivi, hawana plan wanahisi mambo yao yako poa kwasababu mikakati, elimu waliyokua nayo (wanazani ni uwezo wao binafsi).
Wanafikia hatua wanaamini uchawi haupo wengine wanasema hakuna Mungu(Nguvu ya Mungu), yaani wanaamini completely kua waganga na watumishi wa MUNGU ni matapeli wanatuigizia tu. Kumbe wasijue watangulizi (ancestors) wao kuna harakati walifanya zinazowaweka salama hadi leo kiasi kwamba wasione changamoto yoyote duniani hapa, hata wakikutana na changamoto siku moja wanaona ni coincidence tu, kiufupi duniani kuna sarakasi nyingi sana ukiona unautulivu wa kiafya kiuchumi tambua sio bule kuna nguvu ipo nyuma yako. Hili suala sio lahisi kulielezea/kuthibitisha mtu akaelewa/akaamini ni mpaka limtokee yeye mwenyewe, ali-experience by direct observation, tafauti na hapo mtu wa namna hii atakuona wewe ni mjinga unaeshindwa kufikilia mambo kwa kina, au una ufinyu wa akili.
Nachotaka kulielezea hapa ni kwamba mambo mengine ni ya kiroho haijalishi niππβ―οΈ. Nguvu ya kiutawala. Rabonn.
Na ndio maana mataifa makubwa migongano yao mikubwa asilimia kubwa hua inahusisha territories zilizozungukwa na maji bahari kwa kiasi kikubwa kama visiwa(Taiwan, Hong-Kong, Hawai).... peninsula(Korea zote).
Ivi marekani na urusi huku Middle East & far east hua wanatafuta nini? hasa marekani na wakati yeye ni bara lingine kabisa.
Kuna nukuu ya Baba wa Taifa ile nukuu ukii- listen between the pitches utapata kitu, kua "watakao watenge/wabagua wenzao ile zambi ya ubaguzi haitaishia pale inaendelea... .. ." siikumbuki vizuri nukuu. Ila sizanzi kama alizungumza kwa bahati mbaya.
Kuna habari kuwa mwenda zake alikuwa amesha set kuwa katika uongozi wake ataunganisha serikali mbili na kuwa moja, na Zanzibar ikiunganisha visiwa vya pemba, unguja na mafia itakuwa mkoa mmoja wenye wilaya 4, moja pemba, unguja wilaya mbili na ya nne mafia.
Hizi habari, amewahi kuzisema Maalim, tena hadharan. Akasema atapambana kwa hali na Mali kuhakikisha hilo halitokei,
Lakin pia habari za ndan zinasema move ilikuwa kumchukua rais wa Zanzibar kumfanya kuwa ndie mgombea urais wa 2025 ili kuwatuliza Wazanzibar. Bahati mbaya hatuko nae. Mungu ailaze roho yake mahali pema pepon.
Habari za ndan zinasema Leo lilikuwa kui neutralize kabisa, mipango ilikuwa tayar, kuhakikisha wafanyakazi wote wa serikali za miji ya zanzibar kuletwa Tanganyika na kule kupelekwa watanganyika. Wanafunzi wengi kuletwa bara na wa bara kupelekwa kule.
Bahat mbaya mwamba wa kufanya mambo makubwa hayupo.
Ni wazi kuwa aliyetunyang'anya JPM mapema alitukatili sana. Alitunyima mabadiliko makubwa sana.
yoga usiku wa deni haukawii.. nasubiri kwa hamu ujio wa uzi mpya kiongozi.. [emoji847]
Kafanyaje? naona anatamba sana tudai.Daaaaa Mpango kawa mpango
Kwani Mpango ni team ipi kati ya hizi tatu?Daaaaa Mpango kawa mpango
Jibu ni kwamba Mtanganyika alikubali Utanzania. Fahamu kwamba Utanzania unahusu Uzanzibar pia, ndiyo maana Wazanzibar wakitaka kutumia fursa za Tanganyika wanajiita Watanzania. Tunaambiwa Waziri Mbarawa ambaye ni Mzanzibar anafanya kazi ya Uwaziri katika Wizara isiyo ya Muungano kwasababu ni Mtanzania.ulisha wahi kusikia mtanganyika anajitambulisha kuwa ni mtanganyika? unajua ni kwa nin?
Ikiwa muundo wa sasa ni mzuri , malalamiko yanatoka wapi? Wazanzibar wasiobeba gharama zozote wanalalamika. Watanganyika wamechoshwa kubeba Mzigo wao na wa Zanzibar.mkuu muundo wa sasa wa serikali ndyo Bora x1000 kuliko muundo mwingine wowote utakao pendekezwa, kama huu haukubariki maana yake Muungano ufe! na ukifa atakae athirika zaidi ni Zanzibar kwa kuwa atalazimika kuwa mkimbinzi kwenye ardhi yake mwenyewe..
Hakuna anayekuja kujifunza huu ujinga. Tutajie nchi moja tu iliyokuja kujifunza hapa na kama ipo pengine wanajifunza kwamba Muungano wa aina hii una watu wenye akili za kiwango gani!nlisema hapo juu narudia tena hii ndyo ndoa(muungano) pekee duniani ambayo watu wanakuja kujifunza kwetu, kwamba nchi inakuwa na Marais wawili lkn mkuu wa majeshi1,
Si kweli, Mkuu wa Majeshi si Amri Jeshi Mkuu. Kwa nchi moja kuwa na ''Amir Jeshi'' wawili bila kujua ni yupi mkubwa na kwa wakati gani, inashangaza.hapo ndipo upekee unapokuja kwamba mkuu wa majeshi wa Tanzania ndyo anapokea order kutoka Kwa mtu 1 tu bila kujari hyo event imetokea Zanzibar au Tanzania!
ila rais wa Zanzibar anayo mamlaka kwake TU na kwa baadhi ya mambo, mengine nae anayaona na kuyaacha yafanyike hawezi kuyabadili, Wala kuyasemea na huo ndio muungano,
umependa imeze hujapenda imeze hvyo hivyo.
Dawa ya hii ni kuvunjwa muunganoDawa ya hili ni serikali 3.
Vipi kwenye kulipa..? Au analipa aliyekopa sio aliyetumia..?Tanzania ikikopa dola bilioni 100, dola Bilioni 4.5 zinapelekwa Zanzibar!.
πππVipi wenzangu unaona shida yoyote kumlipia deni mkeo?.
Duh!!!..Tena sana, nimesikia akimaliza ujenzi wa barabara ya Benjamin Mkapa ya Mtoni Darajabovu, ataifumua barabara ya bububu hadi Malindi kisha Itafumuliwa ya Malindi hadi Mnazi mmoja,
Bado miradi mingine tusiyoijua,
Na ile ya Tunguu to Kizimkazi nasikia nayo inajengwa.
Ukiwasikiliza Wazanzibari baadhi yao utasikia "Samia afanye haraka amalize miradi kabla ya 2025 maana wabara hawatampa tena"
Kuna mikopo ya Zanzibar, Zanzibar wanakopa wenyewe kwa udhamini wa JMT, ni Zanzibar wenyewe watalipa mikopo hii, ila ikitokea mkopaji akashindwa kulipa, hapa ndipo mdhamini anamlipia.Vipi kwenye kulipa..? Au analipa aliyekopa sio aliyetumia..?
Na ni kama yuko kimya sana siku hizi. TumainiEl na Tumia Akili hawapost chochote siku hiziNadhani mdau huyo ni TumainiEl
Mwaka huu kimetokea kituko kingine cha Muungano
Waziri wa Madini wa JMT ametiiliana saini mktaba (MoU) na Waziri wa Madini wa Zanzibar.
1Katika nchi moja, MoU inakuwaje na kwa sababu gani? Hivi ''Tanzania'' inaweza kuwa na MoU na Mtwara?
Huyu Waziri wa Madini wa JMT ni wa nchi gani? Anawakailisha serikali ya Rais yupi na wa nchi gani?
Hii Tanzania ni nchi gani tofauti na ile iliyoundwa na Tangayika na Zanzibar?
Kilichotokea, suala la madini si la Muungano. Ili Zanzibar waweze kufaidika nalo lazima washirikishwe kupitia makubaliano (MoU). Tanganyika haina sababu za MoU na Zanzibar kuhusu Madini!
Jambo la kujiuliza, kwanini Wazanzibar waliokimbiza ''gesi na mafuta' leo wanataka MoU ya madini ?
Tangu Muungano uasisiwe hatujawahi kusikia Serikali ya Tanzania ikisaini MoU, kwanini ni kipindi hiki cha SSH?
Utaratbu wa MoU unatoka wapi kikatiba , na kwamba Rais wa JMT ambaye ni mkuu wa nchi ya Tanzania kupitia Waziri wa Madini wa JMT anasaini MoU na Waziri wa Madini wa Zanzibar! Hii ni nchi moja au mbili?
Ni suala gani jingine lenye MoU kati ya ''Tanzania na Zanzibar''?