Dart, Udart zapewa siku 90 mabasi Mwendokasi Mbezi Mbagala yapatikane

Dart, Udart zapewa siku 90 mabasi Mwendokasi Mbezi Mbagala yapatikane

jjackline

Senior Member
Joined
Jul 25, 2024
Posts
111
Reaction score
274
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mohammed Mchengerwa amezitaka Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (Dart) na Kampuni ya Mabasi Yaendayo Haraka (Udart) kuhakikisha ifikapo Desemba 2024, mabasi ya mwendokasi yanayotakiwa katika barabara ya Morogoro na ya Mbagala yawe yamepatikana.

Mchengerwa ametoa maagizo hayo Jumatatu Septemba 2, 2024, alipozindua mageti janja na kadi janja kwa ajili ya usafiri wa mabasi ya mwendokasi, jijini Dar es Salaam.

Katika kufanikisha hilo, Mchengerwa amesema hakuna haja ya kuwasubiri wawekezaji kutoka nje ya nchi kwa kuwa wapo Watanzania wengi wanaweza na kutaka wapewe nafasi, wakiwemo wamiliki wa mabasi ya mikoani.

Soma Pia: Amos Makalla: Mabasi ya Mwendokasi yataanza kazi Mbagala Desemba 2024

"Watanzania wamesubiri kwa muda mrefu kupatikana kwa mabasi hayo na sasa inatosha, hatutaki tena kusikia changamoto hii wizarani,” amesema.

Snapinsta.app_458079582_335360669571063_6862794888952628722_n_1080.jpg
 
Nchi ya matamko.. ili aonekane anapower .
Kwani taratibu zinasemaje?
 
Ujinga mtupu sasa siku 90 mmewapa fedha za kununua hayo mabasi? Mnatenga kila mwaka 580B kujinunulia LC300 na kushindwa kusupport huduma za kijamaii.....Misafara magari ya maana zaidi ya 150.
 
Hivi kwani hiyo tenda mkampa mtu kama Shabbiby au Abood si wili 2 tu hayo mabasi yanafika hapo na kuanza kazi? Huyo mwekezaji wa nie ana nini hasa ambacho sisi hatuna?!
 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mohammed Mchengerwa amezitaka Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (Dart) na Kampuni ya Mabasi Yaendayo Haraka (Udart) kuhakikisha ifikapo Desemba 2024, mabasi ya mwendokasi yanayotakiwa katika barabara ya Morogoro na ya Mbagala yawe yamepatikana.

Mchengerwa ametoa maagizo hayo Jumatatu Septemba 2, 2024, alipozindua mageti janja na kadi janja kwa ajili ya usafiri wa mabasi ya mwendokasi, jijini Dar es Salaam.

Katika kufanikisha hilo, Mchengerwa amesema hakuna haja ya kuwasubiri wawekezaji kutoka nje ya nchi kwa kuwa wapo Watanzania wengi wanaweza na kutaka wapewe nafasi, wakiwemo wamiliki wa mabasi ya mikoani.

Soma Pia: Amos Makalla: Mabasi ya Mwendokasi yataanza kazi Mbagala Desemba 2024

"Watanzania wamesubiri kwa muda mrefu kupatikana kwa mabasi hayo na sasa inatosha, hatutaki tena kusikia changamoto hii wizarani,” amesema.

Hii project ni disaster. Posta to gongo la mboto imekuwa kero. yaani saa hizi, usije posta na gari lako. Utakwama masaa 2.
 
Back
Top Bottom