DART watenge mabasi maalum kwa ajili ya wanafunzi, asubuhi wakati wa kwenda shule na jioni wakati wa kutoka shule

DART watenge mabasi maalum kwa ajili ya wanafunzi, asubuhi wakati wa kwenda shule na jioni wakati wa kutoka shule

Mkoba wa Mama

JF-Expert Member
Joined
May 5, 2021
Posts
208
Reaction score
91
Wanafunzi wa shule za kutwa jijini Dar es salaam wanakumbana na changamoto kubwa sana ya usafiri, hii inapunguza morali ya watoto kupenda shule, pia ni moja ya sababu ya matokeo mabaya kitaaluma yanayochangiwa na kuchelewa vipindi, kuchoka sana na hivyo kupunguza umakini wakati wa vipindi na pia kukosa mda wa kutosha kujisomea kwa sababu mda mwingi wanautumia wakiwa barabarani, kubwa zaidi wanafunzi wananyanyasika sana.

Mbali na athari hizo;, hali hii pia inachangia mmomonyoko wa maadili, kwa sababu wakati mwingine wanafunzi wanalazimika kupambana na watu wazima au kurushiana maneno kutokana na kashkash ya kugambonia usafiri, lakini pia hali hii wakati wwingine hupelekea unyanyasaji wa kijinsia/kimaumbile hasa kwa watoto wa kike kwa kujikuta wakishikwa ama kupapaswa sehemu ambazo sio sahihi.

Soma Pia: Mabasi ya mwendokasi yawe suluhisho kwa wanafunzi mikoani

Ninashauri mamlaka zinazohusika kwa maeneo ambayo tayari kuna usafiri wa mabasi yaendayo haraka, yatengwe mabasi maalum kuwasaidia wanafunzi wakati wa kwenda na kutoka shule, hii itasaidia sana kuwapunguzia ghadhabu na usumbufu mkubwa wanaopitia ukilinganisha na umri wao, maana wakati mwingine wanalazimika kutumia nguvu kushindana na watu wazima wakigombania kupata nafasi ya kuingia kwenye gari. Lakini pia itasaidia kuwakutanisha pamoja wanafunzi kutoka shule tofauti na kuweza kubadilishana mawazo na maarifa wakati wa safari.
 
Wazo zuri sana hili.

Unaona jinsi Watanzania tulivyo?? Akili kubwa.

Ilihali ingekuwa wale mamluki wa CHADEMA na magenge yao ya Ugaidi wa Mtandaoni, badala ya kuja na "Idea" kama hii, wangetukana.

Naunga mkono hoja.
 
Wanafunzi wa shule za kutwa jijini Dar es salaam wanakumbana na changamoto kubwa sana ya usafiri, hii inapunguza morali ya watoto kupenda shule, pia ni moja ya sababu ya matokeo mabaya kitaaluma yanayochangiwa na kuchelewa vipindi, kuchoka sana na hivyo kupunguza umakini wakati wa vipindi na pia kukosa mda wa kutosha kujisomea kwa sababu mda mwingi wanautumia wakiwa barabarani, kubwa zaidi wanafunzi wananyanyasika sana.

Mbali na athari hizo;, hali hii pia inachangia mmomonyoko wa maadili, kwa sababu wakati mwingine wanafunzi wanalazimika kupambana na watu wazima au kurushiana maneno kutokana na kashkash ya kugambonia usafiri, lakini pia hali hii wakati wwingine hupelekea unyanyasaji wa kijinsia/kimaumbile hasa kwa watoto wa kike kwa kujikuta wakishikwa ama kupapaswa sehemu ambazo sio sahihi.

Soma Pia: Mabasi ya mwendokasi yawe suluhisho kwa wanafunzi mikoani

Ninashauri mamlaka zinazohusika kwa maeneo ambayo tayari kuna usafiri wa mabasi yaendayo haraka, yatengwe mabasi maalum kuwasaidia wanafunzi wakati wa kwenda na kutoka shule, hii itasaidia sana kuwapunguzia ghadhabu na usumbufu mkubwa wanaopitia ukilinganisha na umri wao, maana wakati mwingine wanalazimika kutumia nguvu kushindana na watu wazima wakigombania kupata nafasi ya kuingia kwenye gari. Lakini pia itasaidia kuwakutanisha pamoja wanafunzi kutoka shule tofauti na kuweza kubadilishana mawazo na maarifa wakati wa safari.
Ni wazo zuri kama serikali wataona inafaa,. Walifanyie kazi
 
Hili ni moja ya mawazo mazuri sana. Na hili si jambo geni hapa Darisalama. Kulikuwako Mabasi kwa huduma hii hii huko nyuma. Watoto wanateseka sana na usafiri.

Swala la kujiuliza ni je, itakuwaje kwa wanafunzi wanaopita njia ambazo DART hawapiti? Au tuwashauri UDA wafanye huduma hiyo?
 
Hili ni moja ya mawazo mazuri sana. Na hili si jambo geni hapa Darisalama. Kulikuwako Mabasi kwa huduma hii hii huko nyuma. Watoto wanateseka sana na usafiri.

Swala la kujiuliza ni je, itakuwaje kwa wanafunzi wanaopita njia ambazo DART hawapiti? Au tuwashauri UDA wafanye huduma hiyo?
Kila kitu kinawezekana ni maamuzi ya wenye mamlaka tu.
 
Ngoja tuonee kwamba kuwe na school bus aaah sawa 🤗🤗🤣🤣
 
Back
Top Bottom