ASIWAJU
JF-Expert Member
- Nov 18, 2022
- 1,938
- 1,632
- Thread starter
-
- #21
Sawa kabisa mkuu, maelezo yako yame eleweka vizuri kabisa.Mkuu hiyo 1600 MW ni rate ya uzalishaji
Ni kama unavyosikia mradi wa maji Ruvu unazalisha lita 1000 kwa saa, ina maana ili kupata lita zinazozalishwa mwaka mzima inabidi uzidishe kwa idadi ya masaa ya mwaka mzima
So kama Rate ya Tanzania ni 1600 MW ina maana kwa mwaka mzima tutakuwa tunazalisha
1600x365 days x 24 hours= 14,016,000 MWh
ambazo ni 14,016 GWh
Ambazo bado ni ndogo sana kama ilivyo pointi ya mada yako
Watts zinapima rate ya uzalishaji au utumiaji wa umeme, hata ukiambiwa pasi yako ni ya 750W ina maana ili upate umeme utakatumika ndani ya masaa 5 itabidi uzidishe kwa masaa
750watts x 5 hours=3750Wh au 3.7kWh ambazo ni unit 3.7
Lakini je tumefika tumefika kiwango hicho kwa mwaka ?