Datsun kurudi sokoni baada ya kutoweka kwa zaidi ya miaka 30

EMT

Platinum Member
Joined
Jan 13, 2010
Posts
14,477
Reaction score
15,325
Baada ya kutoweka kwa zaidi ya miaka 30, Datsun imerudi tena sokoni.

Gari hiyo ambayo iliwafanya carmakers wa Kjapani kuheshimika Marekani na Ulaya miaka 1970 ilikuwa inasifika sana kwa kubana mafuta.

Model mpya ya Datsun ambayo, ilizinduliwa jana nchini India, imekuwa designed kwa ajili ya first-time care owners.

Inatumia lita 1.2, ina viti vitano (hatchback) na itaanza kuuzwa India mwakani kwa dola 6,670 kabala ya kusambazwa Russia na Indonesia.

Datsun ya zamani.



Datsun mpya









 
ngoja wenye hela watumie kwanza then watuletee used tununue
 
Reactions: EMT
Mzee umenikumbusha mbali sanaaa. Miaka ya 94 nliwahi kumiliki Datsun 1200, na baadae Datsun 120Y. hizi gari zilinitoa sana kimaisha sitazisahau kamwe!
 
na mimi nimekumbuka mbali, nilijua gari zao ni pickup tu, kumbe zipo saloon pia.
miaka hiyo mtu mwenye gari pickup aidha ana toyota hilux pickup au datsun pickup.
 
Reactions: EMT
Wachaga wameuvamia uzi huu wakidhani ni mapick up. Wachaga kwa Datsun.
 
Reactions: EMT
na mimi nimekumbuka mbali, nilijua gari zao ni pickup tu, kumbe zipo saloon pia.
miaka hiyo mtu mwenye gari pickup aidha ana toyota hilux pickup au datsun pickup.

Lazima utakua kizazi cha Yooh yoo whats up ma nigga
 
mzee wangu, mzee change anayo mpaka leo anapaki moshi mjini anakula vichwa kwenda mbele, pickup ya dutsan si mchezo
 
Wachaga wameuvamia uzi huu wakidhani ni mapick up. Wachaga kwa Datsun.

mkuu wacha tu tuuvamie huu uzi,kuna gari ambazo mchaga hatakaa azisahau kizazi chake chote
1- bedford- hii ndio kama fuso ya enzi hizo kabla ya isuzu injection tx hazijaingia, bodi yake ilikuwa ya mbao .sijui kizazi cha fuso kinayajua haya
2- pioget pickup na sedan
3- toyota stauti- dume na jike
4- mandolini- landrover ya handeli- hii unashusha injini unafanya mashine ya kusagia kisha unairudisha unaenda kubebea mbege kibosho
 
Dah Umenikumbusha long mkuu Datsun Gari letu la pili mzee alinunua baada ya kuwasota sana na mgongo wa Chura... Datsun 120Y Warejeshe na Morris pia tumezimiss gari niliyokuwa napenda Maishani
 
Umenikumbusha mbali kweli kweli....
 
Dah Umenikumbusha long mkuu Datsun Gari letu la pili mzee alinunua baada ya kuwasota sana na mgongo wa Chura... Datsun 120Y Warejeshe na Morris pia tumezimiss gari niliyokuwa napenda Maishani

mkuu hiki chombo si mchezo ... mshua wangu (R.I.P) alitaka kunyea debe enzi hizo ... late 70's ... kisa alikuwa mtumishi wa umma na alinunua hii mashine tena ilikuwa used toka kwa mhindi ... yale mambo ya uhujumu uchumi yalitesa sana watu!
 
Dash board ya hiyo Datsun ni sawa na ya micra SE.
Wamebadilisha body tu.
 

hapo sema GURUWE, Kitu cha kubebea watalii enzi hizo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…