David Kafulila: Hali ya uchumi wa kati wa Tanzania na rekodi saba za kimataifa zilizowekwa chini ya uongozi wa Rais Magufuli

David Kafulila: Hali ya uchumi wa kati wa Tanzania na rekodi saba za kimataifa zilizowekwa chini ya uongozi wa Rais Magufuli

Mfalme wa Genge

Senior Member
Joined
Mar 30, 2018
Posts
190
Reaction score
224
~Na David KAFULILA.
email: davidkafulila0@gmail.com

02 Septemba 2020.

Julai 1, 2020, ni tarehe itakayokumbukwa katika historia ya Tanzania. Ilikuwa tarehe ya kwanza ya utekelezaji wa Bajeti ya mwisho ya Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Utawala wa Rais JOHN MAGUFULI; na muhimu zaidi, ni siku ambayo Benki ya Dunia ilitambua na kuitangaza Tanzania kama Nchi ya kipato cha kati kabla ya matarajio iliyojiwekea kufikia 2025.

Katika kujadili mafanikio hayo, ningependa kuongelea mambo saba (7) muhimu yaliotekelezwa ndani ya miaka mitano na kuvunja rekodi kimataifa.

Kwanza, tunapaswa kuzingatia kwamba wakati watu wengi walipokuwa wanawasiwasi na kujiuliza kwamba Rais Magufuli anajenga Taifa la namna gani, mnamo Julai 1, 2020, Benki ya Dunia ilijibu Kuwa Rais Magufuli alikuwa anajenga Taifa la kipato cha kati.

Pili, katika uchambuzi wa 2017 wa Bi Christine Legarde alipohojiwa nchini Ethiopia na Jarida la Quartz, alipokuwa Mkurugenzi wa Shirika la Fedha Duniani (IMF), alipongeza kwa moyo mkunjufu mafanikio yaTanzania yaliyofikiwa waikati huo chini ya uongozi wa Rais Magufuli.
Mbali na Ethiopia, Nigeria na Kenya, aliitaja Tanzania kama Nchi iliyokuwa imeonesha dalili za wazi kuelekea safari ya mapinduzi ya viwanda kama Vietnam.

Tatu, kama ilivyoelezwa katika mkutano wa jukwaa la uchumi wa Dunia 2018, Tanzania ilishika nafasi ya kwanza katika Nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara kwa uchumi jumuishi. Rekodi hiyo imedhibitisha kwamba utawala wa Magufuli ni serikali inayowajali masikini

Hata hivyo Tanzania ilitajwa kuwa ni nchi inayoongoza katika mapambano dhidi ya Rushwa kati ya nchi 37 zilizofanyiwa utafiti Barani Afrika mwaka 2019 hii ni kwa mujibu wa Shirika la the Africans Global Options Survey.

Watanzania wametambua jitihada za mafanikio za muda yaliyofikiwa kutoka, kukodisha Ndege kwa dollar za kimarekani 43 million ikifanya kazi kwa miezi 6 tu na miezi 37 ikiwa haifanyika hii ni kwa mujibu wa ripoti Mkaguzi wa hesabu za serikali ya April,2020

Hivi karibuni jukwaa la uchumi wa Dunia liliitangazaSerikali ya Tanzania kushika nafasi ya 28 kati nchi 136 Duniani kwa matumizi Bora ya fedha za Umma. Ikumbukwe kuwa katika jumuia ya Afrika Mashariki naJumuia ya maendeleo ya kusini mwa afrika, Nchi zilikuwa kama ifuatavyo, Botswana nafai 37,Kenya nafasi ya 70 , Uganda nafasi ya 100, Malawi 106, Msumbiji 118. Rekodi hiyo inathibitisha kuwa Rais Magufuli anajenga Serikali yenye nidhamu ya matumizi ya fedha za umma.

Rekodi ya sita inatokana na Utafiti uliofanywa na African Global Opinion Survey 2019 ambayo inaonyesha kwamba imani ya Watanzania kwa Serikali yao imeongezeka sana. Ripoti imesema kwamba 72% walikuwa na imani na Serikali yao katika kupambana na ufisadi, ikilinganishwa na 13% ya ripoti ya 2015. Hii ni moja ya rekodi za mapinduzi makubwa ulimwenguni.

Rekodi ya Saba inatoka kwa Wakala nambari moja wa Ukadiriaji wa Mikopo, MOODYS ambayo inamiliki asilimia 45 ya hisa ya soko la kimataifa, ilikadiria Tanzania kuwa katika kiwango cha uchumi wa B1 katika ripoti yake ya 2017 ambacho ni kiwango cha juu kuliko nchi yoyote katika Afrika Mashariki (ambayo ilipewa B2). Tathmini hii ni ya kwanza nchini Tanzania tangu uhuru.

# Hizi ni rekodi za ulimwengu na zitabaki kuwa kitambulisho cha Rais Magufuli kimataifa, sembuse diplomasia kubwaⁿ aliyotumia kukabili COVID-19 na kuwaacha wengine ulimwenguni wakishangaa inawezekanaje janga la Corona ambalo lilikuwa likitetemesha ulimwengu wote kweli imeshindwa nchini Tanzania.

Msisitizo wangu hapa ni kwamba umiliki wa Magufuli katika urais wa Tanzania unaonyeshwa na mafanikio makubwa yanayostahili rekodi kubwa ya kimataifa. Ikumbukwe, hata hivyo, kwamba aliingia madarakani mnamo 2015 wakati serikali ilikuwa imekata tamaa sana na haiwezi hata kusimamia muswada wa mshahara wa Utumishi wake wa Umma!
 
Rudi ukamwambie alete takwimu za ukuaji wa pato la Mtanzania kwa kila awamu kuanzia Mkapa. Mwambie asituletee habari za kuungaunga kama Abbas.
 
Kafulila endelea kulamba viatu,Raisi kasema anazo nafasi nyingi za uteuzi,lakini wakulaumiwa ni WAJUMBE.
 
Unapozungumzia maendeleo ya nchi zungumzia na maendeleo ya wananchi wake, alafu tambua tumeshushwa hatupo tena ktk uchumi wa kati baada ya kuona ule utafiti ulikuwa wa kupikwa hauna uhalisia,

Sent from my itel S11 using JamiiForums mobile app
 
Mwambie kaka yako hizi ndio nondo zitto junior
Uchumi jumuishi una indicator nane

Yeye amechukua tu Miundombinu basi ndio imetupandisha. Ila regional disparity vipi? Unajua hta doing business ina indicator 9 ssa kma indicator moja imekubeba ikakufanya uwe #10 ilihali variable 8 zingine zipo chini unataka tueleweje?

Uchumi hauchambuliwi kwa face value bali components
 
Msitulazimishe na propaganda, sisi sio wajinga tunaelewa hali halisi ikoje. Hadithi za rekodi wakati miaka mitano watumishi maslahi hayaboreshwi, wakulima wanalia, sekta binafsi zinaangamia? Wafanya biashara wanaumia wengine biashara zao wanafunga.
 
Uchumi jumuishi una indicator nane

Yeye amechukua tu Miundombinu basi ndio imetupandisha. Ila regional disparity vipi? Unajua hta doing business ina indicator 9 ssa kma indicator moja imekubeba ikakufanya uwe #10 ilihali variable 8 zingine zipo chini unataka tueleweje?....
Ni aibu sana ninyi wapinzani kuwa mnakataa ukweli. Kama world economic forum wanamkubali JPL kuwa amekuwa wa kwanza juu ya kuleta uchumi jumuishi alafu unasema eti mtoa mada aliangalia indicator moja.

Kwani wao WEF hawaajui kuwa hadi inclusive economy iwepo kwenye taifa fulani indicators zote zinakuwa zimekamilika!
Screenshot_20200905-042948.png
 
Kafulila bado kidogo ataha mm is CHAUMA, hapa anapiga debe huku anasikilizia uteuzi. Akiona hateuliwi anahamia chauma
 
Hivi huyu Kafulila anafikiri watu ni wajinga.
...wakati mwingine ni bora kukaa kimya..
Mambo yapo so obvious hivyo akae kwa kutulia...
 
Mfalme wa Genge,
[/QUOTE]
Hakika Magu ni kiongozi mwenye maono, mtekelezaji imara, na ana akili ya ubunifu, na ana kiu ya kuleta maendeleo ya watanzania wote
 
~Na David KAFULILA.
email: davidkafulila0@gmail.com

02 Septemba 2020.

Julai 1, 2020, ni tarehe itakayokumbukwa katika historia ya Tanzania. Ilikuwa tarehe ya kwanza ya utekelezaji wa Bajeti ya mwisho ya Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Utawala wa Rais JOHN MAGUFULI; na muhimu zaidi, ni siku ambayo Benki ya Dunia ilitambua na kuitangaza Tanzania kama Nchi ya kipato cha kati kabla ya matarajio iliyojiwekea kufikia 2025...
Hayo yote ni kwa yale mnayotaka ninyi watu waseme na wasikie tu. Kungekuwa na uhuru wa kutafuta, kupata na kutoa habari basi ningekuamini ngaa kwa asilimia moja.

Jamii ambayo hairuhusiwi hata kufanya tafiti huru za kisayansi, au hata kupiga na kuonesha picha halisia zisizikika maadili ya uandishi wa habari, huwezi sema ina habari isipokuwa zilizopikwa na walewale.

Sheria kandamizi za takwimu, habari na nyinginezo zinzfanya watu wawe mithili ya kasuku tu. Hongera kwa pambio zuri la kukuletea mkate mezani kwako ila ukweli haufishwi kwa chochote.
 
1.ajira zetu zipo wapi
2.biashara zetu zinakufa
3.Bei na soko la mazao ya kilimo
4.Haki za binadamu
5.Gharama za afya
 
Kafulila ni mchambuzi mzuri wa uchumi, ila alipoendeleza upotoshaji wa jiwe wakuwa tumeingia uchumi wa Kati kabla ya lengo la 2025 nimempuuza make hapo kaendeleza propaganda nahisi ni attention za kulamba miguu ili akumbukwe kwenye teuzi mapema!
 
Back
Top Bottom