Dawa ya corona yazinduliwa Uingereza

Dawa ya corona yazinduliwa Uingereza

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
1592508476766.png
Serikali ya Uingereza imesema kuwa dawa ya Dexamethasone itakayoanza kutumika mara moja kwa wagonjwa wa COVID 19 nchini humo ina uwezo wa kuokoa maisha ya waliopata maambukizi ya virusi hivyo.

Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson Jumanne Juni 16, amewashukuru wanasayansi wa Chuo Kikuu cha Oxford kwa kugundua dawa ambayo inaweza kupatikana kwa bei nafuu ya paundi tano za Uingereza na kupunguza vifo vya COVID kwa kiasi kikubwa.

Mganga Mkuu wa England Professor Chris Whitty amesema kuwa majaribio ya dawa hiyo yataokoa maisha ya watu duniani kote kwa kuwa Dexamethasone inapatikana katika kill nchi kwa bei nafuu zaidi ya bei ya Uingereza.

Ifahamike kuwa Chuo Kikuu cha Oxford hakijavumbua dawa ya Dexamethasone na kwamba wanasayansi wa chuo hicho wamegundua kuwa dawa hiyo ambayo ilivumbuliwa zaidi ya make 60 iliyopita na ambayo inatumika duniani nzima inaweza pia kutumika katika matibabu ya COVID-19. Wanasayansi wanasisitiza kuwa Dexamethasone inapunguza vifo kwa wagonjwa wa COVID-19 wanaopatiwa hewa ya oksijeni tu kwa kutumia mashine.

Profesa Peter Horby mwanasayansi aliyesimamia utafiti huo amesema kuwa dawa hiyo inapunguza hatari ya vifo kwa wagonjwa hao kwa asilimia 35. Na kwa wanaoongezewa oksijeni bila mashine maalum vifo vinapungua kwa asilimia 20.

Hata hivyo utafiti wa Oxford unaonesha kuwa Dexamethasone haiwasaidii wagonjwa ambao wana dalili tu za maambukizi ya virusi hivyo.

Dawa ya itagharimu dola 50 za Marekani ($50) kwa kuwatibia wagonjwa wanane.

Shirika la Afya Duniani (WHO) limeipongeza Uingereza kwa utafiti huo. Dr Tedros Adhanom Ghebreyesus, WHO Director-General amesema kuwa hii ni dawa ya kwanza inayoonesha kuwa itapunguza hatari ya vifo kwa wagonjwa wanaotumia oksijeni kwa mashine au bila mashine.

“Hizi ni taarifa muhimu na ninaipongeza serikali ya Uingereza na Chuo Kikuu cha Oxford, hospitali nyingi na wagonjwa ambao wameshiriki katika mafanikio makubwa ya kisayansi ya kuokoa maisha ya watu", amesema Dr, Tedros Adhanom Ghebreyesus wa WHO, Jumatano Juni 16, 2020.

Dexamethasone ni dawa gani?

Jambo la kwanza, ni muhimu kuwa kuwa dawa siyo mpya na kwamba ilivumbuliwa na wanasayansi mwaka 1957 baada ya majaribio kwa wagonjwa mbali mbali ikagundulika kuwa inaweza kutumika kwa ajili ya matibabu ya wagonjwa wenye aleji kali kama vile uvimbe unaotokana na maji yanayojaa kwenye misuli mwilini, ugonjwa wa tumbo na aina fulani za kiharusi.

Miaka minne badae ya najaribio mengi zaidi Dexamethasone iliruhusiwa na Shirika la Afya Duniani kutumika rasmi kwa matibabu ya changamoto hizo za kiafya katika mwaka wa 1961.

Sindano ya Dexamethasone ambayo ni jamii ya corticosteroids, inatumika kwa ajili ya kudhibiti magonjwa yanayotokana na aleji ya damu, ngozi, macho, tezi ya shingo (Thyroid), figo, mapafu na mfumo wa mishipa ya fahamu.

Jambo la pili ni muhimu kutambua kuwa Dexamethasone siyo tiba wala chanjo ya COVID-19. Na ndio mana haifai kutumiwa na watu ambao wana dalili tu za korona au wagonjwa ambao hawaongezewi hewa ya oksijeni kwa mashine au la.

Je, dawa hii ni kweli inapatikana katika nchi zote na hasa zile zinazoendelea kama Tanzania? Hili ni swali ambao litajibiwa na wataalamu ya dawa za binadamu, watafiti wa dawa, taasisi mbali mbali za dawa na utafiti wa tiba za magonjwa ya binadamu na hospitali zetu nchini.
 
Hii dawa ina suppress immunity,,sababu mtu. Anapopata corona ina trigger autoimmunity,,ambazo kinga za mwili zinago bersek na hivyo kusababisha inflamation katika mapafu na kupelekea tatizo wanaita,

Acute Respiratory Distress Syndrome (ARDS),hili ni tatizo baya sana ambalo huoelekea mapafu kuvimba na kujaa maji na mtu anapofika stage hii,asilimia chache sana hutoboa hata kama wataweka katika ventilators.

kwahiyo hii dawa inasaidia kushusha immunity ili ziache kureact against corona infection kwa kiasi kile,kwani inaonekana tatizo kubwa iko kwenye over reaction ya kinga za mwili against corona ndo zinasababisha complication
 
Ikiwa hiyo Dawa haimtibu mwenye Dalili ya ugonjwa feki wa Corona Virus bado kabisa hawaja weza kugunduwa dawa ya kuweza kutibu hayo maradhi feki ya Corona Virus.

The System is designed to Create Chronic Disease.
The's no money in being healthy.There's no money in being dead.All the money is being chronically ill.
Dr.Irvin Sahni, MD Lecturer & Scientist


Dr.Irvin Sahni, MD Lecturer & Scientist.jpg
 
View attachment 1482797Serikali ya Uingereza imesema kuwa dawa ya Dexamethasone itakayoanza kutumika mara moja kwa wagonjwa wa COVID 19 nchini humo ina uwezo wa kuokoa maisha ya waliopata maambukizi ya virusi hivyo.

Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson Jumanne Juni 16, amewashukuru wanasayansi wa Chuo Kikuu cha Oxford kwa kugundua dawa ambayo inaweza kupatikana kwa bei nafuu ya paundi tano za Uingereza na kupunguza vifo vya COVID kwa kiasi kikubwa...
Sky, ebu nisaidie kufanya homework kidogo. Dexamethasone inatumka kwenye ngombe kutibu mastitis, ndiyo hiyo unayoiongelea hapa?

Effect of dexamethasone on milk yield and composition in dairy cows

Avi SHAMAY, Fira SHAPIRO, Hanina BARASH, Israel BRUCKENTAL, Nissim SILANIKOVE*

Agricultural Research Organization (ARO), The Volcani Center, Institute of Animal Science,
PO Box 6, Bet Dagan 50250, Israel

(Received 1 September 1999; accepted 4 May 2000)

MASTITIS TREATMENT & CONTROL

15 march 2018
Mastitis is the inflammation of the mammary gland and udder tissue. It usually occurs as an immune response to bacterial invasion of the teat canal by variety of bacterial sources present on the farm, as a result of chemical, mechanical, or thermal injury to the cow’s udder.

1 mg of dexamethasone natrium phosphate....
 
Sky, ebu nisaidie kufanya homework kidogo. Dexamethasone inatumka kwenye ngombe kutibu mastitis, ndiyo hiyo unayoiongelea hapa?

Effect of dexamethasone on milk yield and composition in dairy cows

Avi SHAMAY, Fira SHAPIRO, Hanina BARASH, Israel BRUCKENTAL, Nissim SILANIKOVE*

Agricultural Research Organization (ARO), The Volcani Center, Institute of Animal Science...

Ni kweli dexamethasone ni anti inflammatory steroid na pia 2000 kuna research ilifanyika inayoonyesha kuwa inapunguza kiwango cha utoaji maziwa ikitumika kutibu inflammation ya matiti ya ng’ombe.


Effect of dexamethasone on milk yield and composition in dairy cows
Avi SHAMAY, Fira SHAPIRO, Hanina BARASH, Israel BRUCKENTAL, Nissim SILANIKOVE*
Agricultural Research Organization (ARO), The Volcani Center, Institute of Animal Science, PO Box 6, Bet Dagan 50250, Israel
(Received 1 September 1999; accepted 4 May 2000).

Abstract — Dexamethasone was injected in dairy cows in order to get a better insight into the effects of corticosteroids on milk secretion and composition. A single intramuscular dose of 40 mg dexamethasone caused a 45% reduction in milk yield after 24 h; full recovery took 5 d. The secretion of fat, casein and magnesium was not affected by the treatment.

Consequently, the concentration of fat, total protein, total casein, magnesium and phosphorus increased then decreased in direct proportion to the changes in milk yield. The secretion of total protein, calcium and phosphorus decreased as a result of the treatment.

The concentration of lactose and the monovalent ions (sodium, potassium, and chlorine) was unaffected, and as a result their secretion decreased and returned to pretreatment level in direct inverse proportion to the changes in milk yield. Whey protein secretion decreased for 48 h and was responsible for the decrease in total protein secretion for 48 h. The most profound effect of dexamethasone is the reduction in the secretion of the osmotic components.

milk yield / dairy cows / stress / corticosteroids
* Correspondence and reprints
Tel.: 972 8 9484419; fax: 972 8 9475075; e-mail: nsilanik@agri.huji.ac.il
 
Back
Top Bottom