Dawa Ya Kuongeza urefu (height)

silent lion

JF-Expert Member
Joined
Feb 28, 2012
Posts
1,278
Reaction score
1,794
Wakuu,

Leo ni kama mara ya tatu kuona tangazo kwenye channel mbalimbali za India zikitangaza kuwa kuna dawa ya kuongeza urefu inauzwa kwa pesa za Tanzania kama laki na ishirini. Yaani wanadai ukitumia dawa basi urefu wako utaongezeka.

Je, kisayansi inawezekana hivi hususan kwa watu ambao ni matured kuongeza urefu kwa dawa ?
 
Du!, kaka naomba unijulishe hiyo dawa wanasema inaitwaje?. nataka niitafute ili nimpe mwanangu anayependa sana kucheza basketball ili anywe awe mrefu kama hasheem Thabit.
 
Du!, kaka naomba unijulishe hiyo dawa wanasema inaitwaje?. nataka niitafute ili nimpe mwanangu anayependa sana kucheza basketball ili anywe awe mrefu kama hasheem Thabit.

inaitwa step up herbal growth formula
 
Urefu na ufupi ni mipango ya Mungu, ila unene na wembamba ni bidii yako yako tu ya kura au kufanya diet.
 
hizo hadithi tu bt km unataka kua tall fanya stretching exercises ambazo zinakuongeza urefu kwa kuongeza space ya intervertebral discs za uti wa mgongo. u can gain up to 3 inches bt mind u, lazima ue mvumilivu bcoz it takes time.
 
hii naitaka aisee maana kama inaweza kukurefusha mwili basi hata nonilihino inaweza kurefusha hizo ni fact za kisayansi tu..
 
Kumbe u-tall dili eeee ??
 
>HII DAWA NI KWELI IPO LAKINI SI KWA ADULT.
>Inachokifanya ni kustimulate pituitaly and thyroid gland zizarishe growth hormone iitwayo 'somatrophic hormone'
>Kwa watoto husaidia kurefuka kama wanavyo dai
>Lakini kwa watu wazima usababisha tatizo la 'acromegally'
yaani mtu harefuki ila baadhi ya viungo vyake vinaongezeka unene na upana
mf😛ua kuwa kubwa,miguu na mikono kuwa mipana, n.k
So MTU MZIMA HUSIJISUMBUE.
 
duu kwl dunia inamambo haya nielekezen wp ntaipata
 
Kuna rafiki yangu mwarabu tulisoma nae na alikuwa mfupi enzi hizo ila baada ya kumaliza tukakutana nae siku moja baada ya kupotezana nae aisee ni kweli jamaa alikuwa karefuka balaa anyway nilishangaa sana nikamuuliza akanijibu ni kwamba alipelekwa hospital akachomwa sindano ya kustimulate pituitary gland ndo ikawa hivyo ki ukweli nilishangaa lakini ni kweli hii kitu ipo.
 
ije na huku, hata miye ntanunua
 
Mmmmh jamani kama ipo na uchunguzi ukibaini inafaa bora tuitumie tu, maana hawa dada zetu wengine wanatuonea sana........!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…