Dawa ya Kupunguza Hasira

Dawa ya Kupunguza Hasira

Mhafidhina

JF-Expert Member
Joined
Feb 6, 2008
Posts
549
Reaction score
23
Wanajamii habari za masiku?

Naomba mnisaidie hili tatizo ili niweze kumnusuru ndugu yangu.

Nina ndugu yangu ambae yeye ana hasira sana. Pia ni mtu ambaye huwa ni negative thinker, yaani endapo utamuomba ushauri yeye huwa anawazia negatively tu. Hivi karibuni alifanya vurugu na kupigana na watu matokeo yake aliumizwa sana. Huwa anajutia sana hizo hasira zake lakini anashindwa kuzi control.

Naomba mnishauri namna ya kuweza kumsaidia huyu ndugu yangu ili aondokane na hali hii.

Namna bora ya kudhibiti hasira

1. Tafuta chanzo cha hasira

Ni mambo gani yanakufanya kuwa na hasira? Ukishayajua tafuta namna ya kupata suluhisho la mambo hayo.

2.Epuka watu,maeneo, na mambo yanakufanya kupandwa na hasira

Pengine ni kwenye ushabiki wa mpira au labda ni kwenye majadiliano ya kisiasa, epuka mambo hayo.Si lazima ubishane kuhusu siasa au mpira,tafuta jambo lingine

3. Jifunze namna ya kudhibiti hisia zako
Hisia zinapaswa kuwa chini ya uwezo wako wa kuamua, si lazima kwa kuwa unahisi hasira basi ufanye mambo kwa hasira. Kwa kifupi tumia kichwa na sio fikara

4. Angalia/Tafuta namna bora za kutoa hisia za hasira

Wengi tumeshindwa hapa, si lazima ukiwa na hasira utoe matusi au maneno mabaya. Hamna haja ya kutaka kupigana au kutoa maneno ya kashfa,eleza kilichokuudhi bila kutumia hasira. '' When communicated respectfully and channeled effectively, anger can be a tremendous source of energy and inspiration for change.''

4. Jichunguze....

Jifanyie tathmini, je hasira zako zimetatua tatizo lolote? Je hasira inakufanya kuwa mtu bora mbele ya famlia yako, mke,mume na watoto.

Umeharibu urafiki mara ngapi kwa sababu ya hasira?

KIla la kheri mdau...
 
Nikutanishe nae tutafute dawa maana mie nina hasira kama zake kidogo tu nishakuja juu.
Hata sijui dawa yake nini mwenzenu labda leo tutapata dawa humu maana hali ni tete.
 
Mwambie hawe anasoma bible kuna mafundisho kibao juu ya Hasira ..
 
Anapata hasira akifanywa nini? Akibishiwa, akidanganywa au akitaniwa?
 
zako zilianza kupungua ila toka ujifiche ndo zimerudi!njoo kwa kanseling na maombi!nilikumissssss

Si kila aendaye hospitali kama Mirembe ni kichaa, you know due to hard ships in life discourse, our minds tend to adopt some madness, hivyo ni vyema baada ya kumwomba Mungu pia kuwapitia wataalamu wa mishipa na ufahamu kwa councelling na tiba.
 
Dawa yake rahisi sana. Ni mkono na sabuni tu (afu aitumie hiyo dawa akiwa amejificha)!!!!!!
 
Wanajamii habari za masiku?

Naomba mnisaidie hili tatizo ili niweze kumnusuru ndugu yangu.

Nina ndugu yangu ambae yeye ana hasira sana. Pia ni mtu ambaye huwa ni negative thinker, yaani endapo utamuomba ushauri yeye huwa anawazia negatively tu. Hivi karibuni alifanya vurugu na kupigana na watu matokeo yake aliumizwa sana. Huwa anajutia sana hizo hasira zake lakini anashindwa kuzi control.

Naomba mnishauri namna ya kuweza kumsaidia huyu ndugu yangu ili aondokane na hali hii.

Ajiunge na kozi ya KARATE au KUNG FU kwa sababu zifuatazo. Kwanza itamsaidia hatakuwa akipigwa kizembe na kuumizwa mara anapokasirika. Pili ili kwenye hii michezo ya marshal arts kuna syllabus ya jinsi ya kudhibiti hasira yako hasa unapochokozwa na watu.
 
Mh hii dawa akipatikana, nitaiomba nina rafiki yangu mh dakika noja nyingi ukibadilishana naye tu sentensi mbili unaye!

Kila siku anaomba mungu ampunguzie hiyo hasira nadhani akipata na dawa mambo yatakuwa swafi sana
 
Si kila aendaye hospitali kama Mirembe ni kichaa, you know due to hard ships in life discourse, our minds tend to adopt some madness, hivyo ni vyema baada ya kumwomba Mungu pia kuwapitia wataalamu wa mishipa na ufahamu kwa councelling na tiba.

Pia ajaribu kuangalia family history,si unajua nazi haianguki mbali na mti,anaweza kupata pakuanzia.
 
Mkuu hasira za kupitiliza mara nyingi huletwa na sababu fulani, most of cases huwa ni faistration za kimaisha, mara nyingi watu ambao walikua na matarajio fulani na ikawa hawajafikia malengo yao kwa kiwango kikubwa huwa wanakuwa na hisia kali na kuona kila kitu kipo against na wao, ingawa hii si kwa wote.

Hakuna dawa as labda kidonge utameza ili kumaliza hilo tatizo, huyo anahitaji ushauri nasaha wa kisaikolojia toka kwa wataalamu muhimbili
 
Dawaa kubwaa ni kunywaa glass ya majiii pindi apandwapo na asiraaa.
 
Wanajamii habari za masiku?

Naomba mnisaidie hili tatizo ili niweze kumnusuru ndugu yangu.

Nina ndugu yangu ambae yeye ana hasira sana. Pia ni mtu ambaye huwa ni negative thinker, yaani endapo utamuomba ushauri yeye huwa anawazia negatively tu. Hivi karibuni alifanya vurugu na kupigana na watu matokeo yake aliumizwa sana. Huwa anajutia sana hizo hasira zake lakini anashindwa kuzi control.

Naomba mnishauri namna ya kuweza kumsaidia huyu ndugu yangu ili aondokane na hali hii.
Mshauri awe anakoga au kujimwagia maji kila anapopatwa na hasira.
 
Mkuu ktk hasira mwambie asitende chochote. Kila mtu ana hasira ila cha muhimu ni kutotenda bila maamuzi ya kina. Pia mshauri aone kuwa kila kitu kinawezekana. Mfano,mtu akitukanwa anakuja juu,ila kama angejua tusi lolote lifikiriwe kubeba ujumbe wa kawaida japo unauma.

Hasira hupungka ukichukulia vitu kwa uzito tofauti.
 
Wanajamii habari za masiku?

Naomba mnisaidie hili tatizo ili niweze kumnusuru ndugu yangu.

Nina ndugu yangu ambae yeye ana hasira sana. Pia ni mtu ambaye huwa ni negative thinker, yaani endapo utamuomba ushauri yeye huwa anawazia negatively tu. Hivi karibuni alifanya vurugu na kupigana na watu matokeo yake aliumizwa sana. Huwa anajutia sana hizo hasira zake lakini anashindwa kuzi control.

Naomba mnishauri namna ya kuweza kumsaidia huyu ndugu yangu ili aondokane na hali hii.

Ana mwili nyumba? :roll:
 
Kuna chanzo cha yeye kuwa na hasira ovyo,yapaswa kijulikane.....wengine huona wanadharauliwa yaani ana lo self esteem,hajiamini matokeo yaka kila kitu anahasira tu.....ni katika hali gani/mazingira gani hupata hasira,ya ubishi?:coffee:
 
Back
Top Bottom