Mhafidhina
JF-Expert Member
- Feb 6, 2008
- 549
- 23
Wanajamii habari za masiku?
Naomba mnisaidie hili tatizo ili niweze kumnusuru ndugu yangu.
Nina ndugu yangu ambae yeye ana hasira sana. Pia ni mtu ambaye huwa ni negative thinker, yaani endapo utamuomba ushauri yeye huwa anawazia negatively tu. Hivi karibuni alifanya vurugu na kupigana na watu matokeo yake aliumizwa sana. Huwa anajutia sana hizo hasira zake lakini anashindwa kuzi control.
Naomba mnishauri namna ya kuweza kumsaidia huyu ndugu yangu ili aondokane na hali hii.
Naomba mnisaidie hili tatizo ili niweze kumnusuru ndugu yangu.
Nina ndugu yangu ambae yeye ana hasira sana. Pia ni mtu ambaye huwa ni negative thinker, yaani endapo utamuomba ushauri yeye huwa anawazia negatively tu. Hivi karibuni alifanya vurugu na kupigana na watu matokeo yake aliumizwa sana. Huwa anajutia sana hizo hasira zake lakini anashindwa kuzi control.
Naomba mnishauri namna ya kuweza kumsaidia huyu ndugu yangu ili aondokane na hali hii.
Namna bora ya kudhibiti hasira
1. Tafuta chanzo cha hasira
Ni mambo gani yanakufanya kuwa na hasira? Ukishayajua tafuta namna ya kupata suluhisho la mambo hayo.
2.Epuka watu,maeneo, na mambo yanakufanya kupandwa na hasira
Pengine ni kwenye ushabiki wa mpira au labda ni kwenye majadiliano ya kisiasa, epuka mambo hayo.Si lazima ubishane kuhusu siasa au mpira,tafuta jambo lingine
3. Jifunze namna ya kudhibiti hisia zako
Hisia zinapaswa kuwa chini ya uwezo wako wa kuamua, si lazima kwa kuwa unahisi hasira basi ufanye mambo kwa hasira. Kwa kifupi tumia kichwa na sio fikara
4. Angalia/Tafuta namna bora za kutoa hisia za hasira
Wengi tumeshindwa hapa, si lazima ukiwa na hasira utoe matusi au maneno mabaya. Hamna haja ya kutaka kupigana au kutoa maneno ya kashfa,eleza kilichokuudhi bila kutumia hasira. '' When communicated respectfully and channeled effectively, anger can be a tremendous source of energy and inspiration for change.''
4. Jichunguze....
Jifanyie tathmini, je hasira zako zimetatua tatizo lolote? Je hasira inakufanya kuwa mtu bora mbele ya famlia yako, mke,mume na watoto.
Umeharibu urafiki mara ngapi kwa sababu ya hasira?
KIla la kheri mdau...