Dawa ya Malaria aina LUMERAX yapanda bei mara mbili

Dawa ya Malaria aina LUMERAX yapanda bei mara mbili

Brightg

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2013
Posts
372
Reaction score
662
Dawa aina ya Lumerax 80/480 mikoa ya Kaskazini ilikuwa inauzwa sh 5,000 haijapita miezi 5 toka ninunue dawa hiyo ili inisaidie kutibu malaria, leo hii nimeenda karibia maduka yote ya dawa nimeambiwa inauzwa sh 10,000, najiuliza kwanini dawa hii imepandishwa bei namna hii, kama mtu mwenye uwezo mdogo hawezi kumudu gharama hii serikali itamsaidiaje, hii ni dawa yenye uwezo mkubwa sana kutibu malaria.

Miaka ya nyuma serikali ilitoa ruzuku kwa dawa za malaria ili wananchi watibiwe kwa unafuu leo hii imekuwa ni dawa ghali sana. serikali iliangalie sana hili
 
Uchumi wa kati maana yake nyinyi ni vibopa , Sasa mnalia nini ?
 
Sio dawa tu sabun za mchi, sabun za b 29, mafuta ya kupikia vyote vipo juu sana bei imepanda
 
Dawa aina ya Lumerax 80/480 mikoa ya Kaskazini ilikuwa inauzwa sh 5,000 haijapita miezi 5 toka ninunue dawa hiyo ili inisaidie kutibu malaria, leo hii nimeenda karibia maduka yote ya dawa nimeambiwa inauzwa sh 10,000, najiuliza kwanini dawa hii imepandishwa bei namna hii, kama mtu mwenye uwezo mdogo hawezi kumudu gharama hii serikali itamsaidiaje, hii ni dawa yenye uwezo mkubwa sana kutibu malaria.

Miaka ya nyuma serikali ilitoa ruzuku kwa dawa za malaria ili wananchi watibiwe kwa unafuu leo hii imekuwa ni dawa ghali sana. serikali iliangalie sana hili
Alu ni alu tu, piga ya jani bei 3000 huko ulikoenda waachie wenyewe[emoji1][emoji1][emoji1][emoji1]
 
Mzee si ununue tu ALU ya vidonge vingi, LUMERAX wamepunguza drug burden tu ila ni ileile Artemether/Lumefantrine
Jamaa anahagaika na mambo ya starehe zake alfu aje kulalamika huku eti imepanda. Dawa za malaria ni 2500/- kwa zile vidonge Vinne. Dawa inayokuwa imeandaliwa kwa teknolojia kubwa na bei yake inakuwa imechangamka.! We kama mvivu wa kumeza vidonge vinne basi lipa hiyo 10k.
Viongozi wetu wapo busy na mambo ya msingi sio hilo kwa kwako.! Wewe ni sawa na mtu anayelalamika kununua marashi ya elfu themanini ili hali marashi ya elfu tano yapo pia.
Kula kulingana na urefu wa kamba yako.! Watu wengine bhana. Hapo napo mnataka kuisingizia serikali 😎😎
 
Mkuu tandika mseto achana nayo hiyo, Hiyo ni mahususi kwa walio uchumi wa kati wewe bado hujafikia wewe bado ni mnyonge na level yako ni mseto, mwaforty, vitungu saumu, mlonge au nyungu
 
Tatizo la hayo madawa ukinywa tu lazima usikilizie huwezi endelea na shughuli zako eti dawa zinafanya kazi.

Dawa za asili hazina huo ujinga unaendelea na shughuli zako kama kawaida.
 
Mkuu.tutakuja.uko.ngoja tumalizane na BEI za cement kwanza
 
Hahaha "kwani malaria nilireta mimi!? Anauliza rais wako.
 
Back
Top Bottom