Exaud J. Makyao
JF-Expert Member
- Nov 30, 2008
- 1,518
- 24
Tafadhali nijulisheni dawa ya kuponya tatizo la NYONGO mwilini.
Je tatizo la nyongo ndilo heartburn kwa Kiingereza?
naomba msaada.
Heartburn.
Je nyongo inazidi au kupungua?
Inazidi mkuu.
Heart burn ni kiungulia, hali hii inatokana na nyongo kuzidi sana tumboni, na kuna sababu zake,
kwa vile umetaka kujua heart burn na nyongo, jibu ndio hilo, sababu zake utajulishwa siku nyngine.
Mtoa bandiko kabla sijachangia una tatizo la kuongezeka uzito? na umewahi kucheki cholestral level yako? Je wewe ni mlaji wa nyama sana red mt au kilaji? pilipili je?
Kule kwetu ikikupata hii tunakunywa magadi. Yale ya kutengeneza kiburu. Kwa huku naona wengine wanakulaga majivu. Mimi nikinywa maziwa fresh huwa namaliza kabisa. Au labda kwa kuwa cha kwangu kinasababishwa na mitungi.
Mkuu Ngulli,
Maswali yako yanaashiria mema katika kufikia suluhisho.
1. Mwenye tatizo hili hana tatizo la kuongezeka uzito.
2. Si mtumiaji sana wa red meat ila hutumia kwa uchache.
3. Hupenda sana pilipili japo hutumia mara chache sana.
4. Hajawahi kupima colestral level.
Tatizo la nyongo lisipozibitiwa linasababisha ulcers/vidonda vya tumbo kwa vile inakwangua ute ute pembeni mwa utumbo kwa jina la kitaalamu unaitwa mucus so kunabakia chubuko. Pia inaweza kusababisha stomach cancer.
Nyongo/bile inasabishwa na ulaji wa vitu vyenye acid kali kama pombe.
Inaweza kumwagika tumboni kwa wingi kutokana na mshituko wa hofu ya uoga wa situation yeyote ile. au hofu kwa mfano kufiwa etc.
Tafadhali nijulisheni dawa ya kuponya tatizo la NYONGO mwilini.
Je tatizo la nyongo ndilo heartburn kwa Kiingereza?
naomba msaada.
Apime pia bilurubin total & bilurubin level
Heartburn sio nyongo, ni kiungulia!!!! na tatizo hilo linatokana endapo mfumo wako wa usagaji chakula mwilini haufanyi kazi ipasavyo/vyema/sawia!!
"Heartburn is a painful burning sensation in your chest, caused by indigestion"
Asante Ngulli,
Huyu mhusika si mtumiaji wa pombe na wala haimpati kwa ajili ya hofu.
Nitatzo la zaidi ya miaka kumi sasa.
Awe katika hali ngumu au raha, hali hii hujitokeza tu.
Kama ni miaka 10 tayari ana ulcers na kama ana ulcers atibu ulcers kwanza na kutibu ulcers kunaanzia kichwani then ndio tumboni.