Pre GE2025 DAWASA inatekeleza ujenzi wa vituo nane (8) vya kisasa vya kuchakata majitaka kwa thamani ya Bilioni 16

Pre GE2025 DAWASA inatekeleza ujenzi wa vituo nane (8) vya kisasa vya kuchakata majitaka kwa thamani ya Bilioni 16

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

The Watchman

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
896
Reaction score
1,427
Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira DAWASA inatekeleza ujenzi wa vituo nane(8) vya kisasa vya kuchakata majitaka/takatope vyenye thamani ya Bilioni 16 katika jiji la Dar Es Salaam ambavyo itasaidia kupunguza gharama za kuzoa majitaka kutokana na ufinyu wa maeneo ya kuyahifadhi.

Akizungumza baada ya ziara ya kuwaonyesha Wenyeviti wa mitaa kutoka Wilaya ya Temeke miradi ya DAWASA iliyopo wilayani humo Kaimu Mkurugenzi Uzalishaji na Usambazaji Maji, Mhandisi Tyson Mkindi amesema lengo la ziara hiyo ni kuwaonyesha jitihada za serikali katika kuboresha huduma za afya ili waweze kuwaelewesha wananchi wao kwa sababu wao wapo karibu nao zaidi.

Pia soma: Pre GE2025 Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Kwa leo Wenyeviti hao walitembelea kituo cha kuchakata takatope cha Vikunai, kituo cha kuzalisha na kusambaza maji cha Mtoni Mtongani, na kisima cha maji cha Yombo.

Mhandisi Mkindi ameeleza kuwa miradi hiyo 8 ikikamilika itakuwa na faida nyingi ndani yake ikiwemo kupatikana kwa mbolea, maji safi ya kuweza kutumika kwa shughuli za kibinadamu, ajira za kudumu, pamoja na uzalishaji wa miche ya miti katika kila kituo ambayo itasambazwa katika wilaya zilizopo Dar Es Salaam.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa Wenyeviti wa mitaa ya Temeke Sharifu Mustafa Jumbe ameishukuru DAWASA kwa kuwajuza juu ya miradi hiyo na kueleza kuwa uelewa waliopata utawasaidia kwenda kuelimisha wananchi juu ya huduma ambazo DAWASA inatoa.

Naye Sara Shomari Mwenyekiti wa mtaa wa Jeshi la Wokovu pamoja na Yonathan Landa Mwenyekiti wa mtaa wa KekoMachungwa wamesema mradi wa Vikunai utawasaidia wananchi wake kupunguza gharama ambazo wao hulipa ili kupata huduma ya kunyonya takatope pamoja na kusaidia upatikanaji wa ajira kwa vijana.

DAWASA inatekeleza mpango wa kukutana na Wenyeviti wa mitaa katika wilaya zote za jiji la Dar Es Salaam kwa ajili ya kutembelea miradi iliyopo katika wilaya zao pamoja na kuwapa semina lengo likiwa kujenga mahusiano ya karibu na wenyeviti hao pamoja na kuwapa elimu juu ya huduma ambazo mamlaka hiyo inatoa.
20250219_212414.jpg
20250219_212408.jpg
20250219_212403.jpg
 
Nchi ya kijinga kabisa.ubungo karibu yote haijaungwa na huduma ya maji halafu wanatuletea upuuzi
 
Wenyeviti wa Serikali za Mitaa katika Wilaya ya Temeke wamepongeza na kuridhishwa na uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali kwa Wizara ya Maji kupitia Mamlaka ya majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) katika uboreshaji wa huduma ya Majisafi na Usafi wa Mazingira kwa wananchi katika Wilaya hiyo.

Hayo yamebainishwa katika ziara inayoendelea kwa siku ya pili ya Wenyeviti wa Serikali za mitaa kwenye vyanzo na miradi ya DAWASA inayolenga kujenga uelewa wa pamoja wa utoaji wa huduma ya Maji kwa Viongozi pamoja na kuweka mikakati ya namna ya kulinda miundombinu ya maji.

Awali kabla ya ziara kwenye Mtambo wa kuzalisha maji Mtoni uliopo Wilayan Temeke, Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu DAWASA Mhandisi Mkama Bwire aliwashukuru viongozi hao kwa muitikkl mkubwa na kushiriki ziara hiyo itakayosaidia kuongeza tija ya utendaji kwa Mamlaka na kwa wananchi pia.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

"DAWASA tuna amini huduma endelevu ni ushirikishwaji wa watu na wenye watu ni nyinyi Wenyekiti wa Serikali za Mitaa, tunaamini katika kushirikiana ili kuimarisha huduma ya Majisafi na Usafi wa Mazingira katika maeneo yenu ya Wilaya ya Temeke," alisema Mhandisi Bwire.

Naye Mwenyekiti wa Wenyeviti katika Wilaya Temeke Ndugu Sharifu Jumbe ameipongeza DAWASA nakubainisha kuwa ni jambo la historia katika Wilaya ya Temeke kwa viongozi wa mitaa kupewa fursa ya ushirikishwaji katika mikakati mbalimbali kuboresha huduma za Maji kwa wananchi.

"Kwanza tunaishukuru DAWASA kwa kutambua umuhimu wa Viongozi wa Serikali za mitaa, kupitia ziara hii tumeridhika na uwekezaji unaoendelea kufanyika katika utekelezaji wa miradi yao," amesema.

"Pili tumejifunza mengi kuanzia utoaji wa huduma za Majisafu na Usafi wa Mazingira, hivyo tutasimamia vilivyo utoaji wa huduma kwa wananchi na kutoa ushirikiano wa kutosh kwa DAWASA ili lengo litimie," aliongeza Ndugu Jumbe.

Ziara hiyo iliyoongozwa na Kaimu Mkurugenzi wa uzalishaji na usambazaji Maji DAWASA, Mhandisi Tyson Mkindi, ilianzia katika mradi wa Usafi wa Mazingira Vikunai Kata ya Kijichi ukiwa ni sehemu ya mradi wa kimkakati unaohusisha ujenzi wa vituo nane vya huduma kwa Umma unaotekelezwa katika Wilaya tano za Mkoa wa Dar es Salaam utakaosaidia kupunguza adha ya uchafuzi wa Mazingira lakini utasaidia kuzalisha gesi pamoja na kupata mbolea kwa shughuli za kilimo ambao umetekelezwa kwa gharama ya shilingi bilioni 16.

Vilevile viongozi hao walitembelea Mtambo wa uzalishaji maji Mtoni ambao unahudumia kwa kiwango kikubwa Wakazi wa Wilaya Temeke na kuonesha hatua zote za kutibu maji hadi kumfikia mtumiaji na pia kutembelea Kisima cha Maji Makangarawe ikiwa ni sehemu ya kisima kati ya visima 31 vilivyopo na vinavyohudumia Wilaya Temeke.

Mamlaka inaendelea na ziara na mafunzo ua ushirikishwaji wa Viongozi wa Serikali za Mitaa katika Wilaya zote Tisa za kihuduma katika Mikoa ya Dar es salaam na Pwani.
IMG-20250219-WA0058.jpg
IMG-20250219-WA0059.jpg
IMG-20250219-WA0060.jpg
IMG-20250219-WA0061.jpg
IMG-20250219-WA0062.jpg
IMG-20250219-WA0063.jpg
 
Kwahio tatizo la maji limekwisha ? Au bado ? Naona tunajikita zaidi kwenye Mengineyo zaidi ya habari yenyewe (Kwamba Matatizo ya Maji kwenye Nchi yenye iliyozungukwa na Maziwa Makuu ni Uzuzu)

In abundance of Water, A fool is Thirsty....; Naona watu wanapiga Selfie tu....
 
Back
Top Bottom