KERO DAWASA Kibaha nini tatizo? Hakuna Huduma ya Maji wiki ya pili, hayo mabomba mabovu hayatengenezeki?

KERO DAWASA Kibaha nini tatizo? Hakuna Huduma ya Maji wiki ya pili, hayo mabomba mabovu hayatengenezeki?

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Nyakijooga

JF-Expert Member
Joined
Dec 9, 2018
Posts
276
Reaction score
473
Wiki mbili zilizopita kulitokea changamoto ya bomba la maji kupasuka maeneo ya Maili Moja – Kibaha, hali hiyo ikasababisha maeneo mengi kukosa maji, tuliporipoti DAWASA – Kibaha kila siku wakawa wanatuambia wanarekebisha lakini bado huduma hazijarejea.

Hali hiyo inatupa changamoto kubwa Wakazi wa Maili Moja hasa maeneo ya Muheza na jirani, kuna watu wanauza maji kwenye magari kiasi kwamba tunajiuliza au kuna mchezo kati ya mamlaka na wanaofanya biashara hiyo?

Pia soma ~ DAWASA: Huduma ya Maji Muheza Maili Moja itarejea, mabomba yaliyoharibika yametengenezwa
 
Huwa najiuliza, hivi na sisi Tanzania tutafika wakati tutengeneze drones na Makombora ya masafa marefu?
ikiwa kama basic issues tuna struggle kwa miaka zaid ya sitini yaani (60)?
 
Back
Top Bottom