Mwande na Mndewa
JF-Expert Member
- Feb 26, 2021
- 1,117
- 3,153
Salaam!
Salaam toka Kinyerezi mtaa wa Sadani kwa Babu Ali,huu mtaa una miezi miwili hauna maji,ratiba ya kufungulia maji mara moja kwa mwezi mtaa huu inarukwa either kwa makusudi au wanatuona sisi manyani,kuna mitaa michache inapata maji kwa mwezi hata mara 3 kimpango mkakati ili itumike kama ngao na kuaminisha wakubwa majibu yao kuwa Kinyerezi maji yapo ila ukweli Mimi nipo hapa mtaa wa Sadani kwa Babu Ali huu ni mwezi wa pili maji hayajatoka.
Kwa sasa ili uweze kuagiza maji kwenye gari unatakiwa uwe na Shilingi 45,000. Na Kwa siku gari moja linaweza sambaza Maji kwa familia/kaya 30.
Kwa hesabu za haraka kwa siku moja gari moja linakusanya kiasi cha 1,350,000.
Bill yangu ya mwisho ilikuwa 13,000 ila mtandao mkubwa wa kuuza maji kwa njia ya magari Kinyerezi unafanya biashara kubwa,kwa hesabu za haraka kwa Siku 10 tu wanauhakika ya kuingiza 70,000,000..huku bill za maji za serikali zikiwa chini ya millioni 10.
Mtandao huu wa kuuza maji kwa njia ya magari huku Kinyerezi ni mkubwa na umeota mizizi pamoja na malalamiko ya wanachi kwa Dawasa Kinyerezi hakuna hatua zinazochukuliwa kuuwajibisha mtandao huu.
Wito kwa mamlaka nyingine za serikali kuingia Dawasa kinyerezi ili kuokoa mapato ya serikali yanayopotea,Dawasa Dar es salaam wanatakiwa kuondoa watumishi ya Dawasa kinyerezi ili kulinda heshima yao na Wizara ya Maji.
Salaam toka Kinyerezi mtaa wa Sadani kwa Babu Ali,huu mtaa una miezi miwili hauna maji,ratiba ya kufungulia maji mara moja kwa mwezi mtaa huu inarukwa either kwa makusudi au wanatuona sisi manyani,kuna mitaa michache inapata maji kwa mwezi hata mara 3 kimpango mkakati ili itumike kama ngao na kuaminisha wakubwa majibu yao kuwa Kinyerezi maji yapo ila ukweli Mimi nipo hapa mtaa wa Sadani kwa Babu Ali huu ni mwezi wa pili maji hayajatoka.
Kwa sasa ili uweze kuagiza maji kwenye gari unatakiwa uwe na Shilingi 45,000. Na Kwa siku gari moja linaweza sambaza Maji kwa familia/kaya 30.
Kwa hesabu za haraka kwa siku moja gari moja linakusanya kiasi cha 1,350,000.
Bill yangu ya mwisho ilikuwa 13,000 ila mtandao mkubwa wa kuuza maji kwa njia ya magari Kinyerezi unafanya biashara kubwa,kwa hesabu za haraka kwa Siku 10 tu wanauhakika ya kuingiza 70,000,000..huku bill za maji za serikali zikiwa chini ya millioni 10.
Mtandao huu wa kuuza maji kwa njia ya magari huku Kinyerezi ni mkubwa na umeota mizizi pamoja na malalamiko ya wanachi kwa Dawasa Kinyerezi hakuna hatua zinazochukuliwa kuuwajibisha mtandao huu.
Wito kwa mamlaka nyingine za serikali kuingia Dawasa kinyerezi ili kuokoa mapato ya serikali yanayopotea,Dawasa Dar es salaam wanatakiwa kuondoa watumishi ya Dawasa kinyerezi ili kulinda heshima yao na Wizara ya Maji.