KERO DAWASA Kisarawe bili zinatoka lakini maji hayatoki kwa miaka miwili

KERO DAWASA Kisarawe bili zinatoka lakini maji hayatoki kwa miaka miwili

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

upupu255

Senior Member
Joined
Sep 4, 2024
Posts
119
Reaction score
144
Wananchi wa mtaa wa Nyeburu uliopo kata ya Buyuni ILALA, Dar es salaam wameilalamikia mamlaka ya maji safi na mazingira DAWASA Kisarawe kwa kushindwa kufikisha huduma ya maji kwa zaidi ya miaka miwili sasa.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wamesema licha ya mamlaka hiyo kushindwa kufikisha huduma ya maji kwa zaidi ya miaka miwili lakini bado wananchi wanaendelea kupatiwa ankara kwaajili ya kulipia huduma hiyo.

Akiwa katika kikao cha kujadili kero mbalimbali zinazowakabili wananchi wa Nyeburu mwenyekiti wa mtaa huo SADATH RWETABURA akawaomba wananchi kuendelea kuwa wavumilivu katika kipindi hiki ambacho wataalamu wanaipatia ufumbuzi kero hiyo.

Soma Pia: Madiwani Chalinze wailalamikia DAWASA kushindwa kutoa huduma ya maji kwa wananchi

Kufuatia malalamiko hayo Mwakilishi wa meneja wa DAWASA Kisarawe Mhandisi ERASTO MWAKILULELE akatolea ufafanuzi na namna ambavyo wamejipanga kuhakikisha mamlaka hiyo inarejesha huduma hiyo hivi karibuni.

 
Baadae utasikia mama mama mama mama,yaan Pwani kuna mto Ruvu,mto Rufiji ni mito mikubwa tu,kams hiyo haitoshi serikali ingeweza kutengeneza lambo kubwa kama Mindu Morogoro lets say kila mkoa lakini 2025 hii watu bado wanalia shida ya maji tunashindwa hadi na nchi za majangwa kama Qatar na UAE.

Mtu yeyote anayefanikisha Ccm kuingia madarakan either kwa kupiga kura au kwa vyovyote vile akili yake inatakiwa ipimwe
 
Hivi DC wa mpweche mpweche yupo kweli?

USSR
 
Wachangiaji wakifika 20 niite confusion
IMG_0754.jpeg
 
Back
Top Bottom