upupu255
Senior Member
- Sep 4, 2024
- 119
- 144
Wananchi wa mtaa wa Nyeburu uliopo kata ya Buyuni ILALA, Dar es salaam wameilalamikia mamlaka ya maji safi na mazingira DAWASA Kisarawe kwa kushindwa kufikisha huduma ya maji kwa zaidi ya miaka miwili sasa.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wamesema licha ya mamlaka hiyo kushindwa kufikisha huduma ya maji kwa zaidi ya miaka miwili lakini bado wananchi wanaendelea kupatiwa ankara kwaajili ya kulipia huduma hiyo.
Akiwa katika kikao cha kujadili kero mbalimbali zinazowakabili wananchi wa Nyeburu mwenyekiti wa mtaa huo SADATH RWETABURA akawaomba wananchi kuendelea kuwa wavumilivu katika kipindi hiki ambacho wataalamu wanaipatia ufumbuzi kero hiyo.
Soma Pia: Madiwani Chalinze wailalamikia DAWASA kushindwa kutoa huduma ya maji kwa wananchi
Kufuatia malalamiko hayo Mwakilishi wa meneja wa DAWASA Kisarawe Mhandisi ERASTO MWAKILULELE akatolea ufafanuzi na namna ambavyo wamejipanga kuhakikisha mamlaka hiyo inarejesha huduma hiyo hivi karibuni.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wamesema licha ya mamlaka hiyo kushindwa kufikisha huduma ya maji kwa zaidi ya miaka miwili lakini bado wananchi wanaendelea kupatiwa ankara kwaajili ya kulipia huduma hiyo.
Akiwa katika kikao cha kujadili kero mbalimbali zinazowakabili wananchi wa Nyeburu mwenyekiti wa mtaa huo SADATH RWETABURA akawaomba wananchi kuendelea kuwa wavumilivu katika kipindi hiki ambacho wataalamu wanaipatia ufumbuzi kero hiyo.
Soma Pia: Madiwani Chalinze wailalamikia DAWASA kushindwa kutoa huduma ya maji kwa wananchi
Kufuatia malalamiko hayo Mwakilishi wa meneja wa DAWASA Kisarawe Mhandisi ERASTO MWAKILULELE akatolea ufafanuzi na namna ambavyo wamejipanga kuhakikisha mamlaka hiyo inarejesha huduma hiyo hivi karibuni.