DC Kasesela:Serikali kuwashtaki wajasiriamali wenye mitaji inayozidi sh 4 milioni waliochukua Kitambulisho cha Mjasiriamali

DC Kasesela:Serikali kuwashtaki wajasiriamali wenye mitaji inayozidi sh 4 milioni waliochukua Kitambulisho cha Mjasiriamali

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Mkuu wa wilaya ya Iringa mjini Richard Kasesela amesema ni kosa la Uhujumu Uchumi kwa mtu yeyote mwenye mtaji unaozidi shilingi milioni 4 kutumia Kitambulisho cha mjasiriamali.

Kasesela amesema serikali mkoani Iringa itafanya ukaguzi kwa wajasiriamali wote na wale watakaobainika mitaji yao ni zaidi ya sh milioni 4 watapelekwa TRA wakalipe kodi yote waliokwepa.
Wale watakaoshindwa kulipa kodi watashtakiwa mahakamani kwa kosa la kukwepa kodi ambalo kimsingi ni uhujumu Uchumi amemalizia DC Kasesela.

Source Clouds tv habari!
 
Wameshakusanya tayari sasa waja kivingine
 
Sasa Mbona Serikali Inachanganya Wananchi Wake? Kwa Nini tangu mwanzo wa zoezi la kugawa hivyo vitambulisho haikuanisha ni kuanzia wajasiriamali wa kiwango gani hawastahili kupata hivyo vitambulisho. Basi ifahamike ni kina nani hasa ni wajasiriamali kuliko kujumuisha wafanyabiashara hao wenye hiyo mitaji ya milioni 4. Pengine neno mjasiriamali halieleweki vizuri maana yake, ndiyo maana mpaka wafanyabiasha wenye mitaji ya milioni 4 wamejitokeza kupewa vitambulisho wakijihesabu ni wajariamali
 
Mjasiriamali ni nani na mfanyabiashara ni nani? Tuwekane sawa kwanza kabla hatujajadili.
 
Back
Top Bottom