DC Kilakala: Ukusanyaji wa Mapato Kusaidia Morogoro Kuwa Jiji

DC Kilakala: Ukusanyaji wa Mapato Kusaidia Morogoro Kuwa Jiji

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

DC KILAKALA: UKUSANYAJI WA MAPATO KUSAIDIA MOROGORO KUWA JIJI

Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Musa Kilakala amesema kuwa Manispaa ya Morogoro haiwezi kufanikiwa kuwa jiji pasipo na mipango thabiti ya ukusanyaji wa mapato ya ndani kupitia vyanzo vyake vya kodi.

Ameeleza hayo wakati wa kikao maalum cha Kamati ya Ushauri ya Wilaya - DCC kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya kwa ajili ya kujadili mapendekezo ya mpango na bajeti ya mwaka wa fedha 2025/2026.

DC Kilakala amesema kuwa moja ya mipango waliyonayo ni kufunga mfumo wa kisasa wa ukusanyaji wa mapato katika kituo Kikuu cha Mabasi cha Msamvu mfumo ambao utafanana na ule wa Stendi ya Magufuli Mbezi jijini Dar es Salaam hatua hiyo inalenga kuhakikisha mapato yote yanakusanywa ipasavyo na kuzuia upotevu wa fedha.
 

Attachments

  • WhatsApp Video 2025-02-02 at 17.55.40.mp4
    36.2 MB
Back
Top Bottom