DC Malenya wa Namtumbo: Msilalamike ajira hakuna, utajiri uko shambani

DC Malenya wa Namtumbo: Msilalamike ajira hakuna, utajiri uko shambani

ChoiceVariable

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2017
Posts
66,537
Reaction score
75,687
Huo ndio Ushauri wa DC Kwa Vijana wa Tanzania kwamba waache kulalamikia ugumu wa Maisha na kukosa Ajira badala yake wakalime maana huko ndiko Kuna utajiri.

My Take
Huyu Kwa nini asiache u DC aende kulima Ili awe Tajiri?

Bila kuwa Chawa hatoboi mtu

----

Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo, Ngollo Ng’waniduhu Malenya amewataka Wananchi hususani Vijana kutokaa vijiweni wakilalamika kuwa hakuna ajira na maisha magumu na badala yake wajiongeze kwa kujishughulisha na kilimo ambacho amesema kinalipa na wapo waliotajirika kupitia kilimo huku akisema Wilaya hiyo imepanga kufanya mapinduzi ya kilimo.

DC Ngollo amesema ili kuwafanya Wananchi washawishike kulima amenunua na kugawa bure majembe 500 kwa Wakazi wa Wilaya hiyo ikiwa pia ni sehemu ya kuunga mkono jitihada za Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuinua Sekta ya Kilimo nchini.

"Tunataka tufanye mapinduzi ya kilimo, Mh.Rais August 08,2023 alitangaza Mkoa wa Ruvuma kuwa tunaongoza kwa uzalishaji kwahiyo Mkoa wa Ruvuma ni Baba lao kwa uzalishaji wa chakula na Namtumbo tukiwemo”

Malenya ametoa majembe hayo wakati wa Kilele cha Jukwaa la Utambuzi wa Fursa za Kilimo, Biashara na Utalii (Namtumbo Kihenge) lililofanyika Namtumbo na kuhudhuria na Wadau mbalimbali akiwemo Naibu Waziri wa Kilimo, David Silinde aliyemwakilisha Waziri wa Kilimo, pia Benki ya NMB ni miongoni mwa Wadau walioshiriki, Wadau wengine ni TFS, TIC, ASA, Nyerere National Park, n.k

Chanzo: Millard
 
Hawa ma dc vijana waliokoma uwezo wa kubuni mipango ya kuwainua vijana na kufikiri sawasawa, wanafanya makosa yanayohatarisha ajira zao wenyewe lakini pia yanayoamsha hasira za vijana dhidi ya Serikali Yao.

anaweza kuwa sahihi lakini approach Lazima iwe very positive kwenye hiyo ajira yenyewe ili kusudi hilo kundi livutike na hiyo ajira yenyewe.

saa zingine afadhali wakae kimya tu
 
Aachie nafasi ashike mwingine halafu yeye aende akalime ili awe wa mfano kwa wengine.kuna watu hukalia kusema jiajiri ili Hali yeye hata biashara ndogo ya kuuza ubuyu hajawahi fanye Kama hawana vya kuongea Bora ukae kimya.
 
Ila acheni utani, moja ya Maamuzi magumu ni kuhamia kwenye kilimo kama njia ya kutoboa kiuchumi.
na pia inahitaji muda na subra sana. Mie mwaka huu nimelima ekari 10, bila mbolea wala mbegu za kisasa nimeambulia gunia chini ya gunia 20, alizeti gunia kadhaa, mahindi gunia kadhaa na mbaazi gunia kadhaa.

Mtu mwingine hawezi endelea na kilimo kwa matokeo haya. Inahitaji ustahimilivu mno.

Jukwaa la Kilimo wamenipa maarifa mwaka ujao wa kilimo zaidi nitusue. Nimeongeza ekari 10 nyingine zimekua 20. Hii yote ni matokeo ya kubeti. Saa zingine ubeti kunasaidia ila muhindi akinunua anakupiga mwaka mzima.
 
Hawa ma dc vijana waliokoma uwezo wa kubuni mipango ya kuwainua vijana na kufikiri sawasawa, wanafanya makosa yanayohatarisha ajira zao wenyewe lakini pia yanayoamsha hasira za vijana dhidi ya Serikali Yao.

anaweza kuwa sahihi lakini approach Lazima iwe very positive kwenye hiyo ajira yenyewe ili kusudi hilo kundi livutike na hiyo ajira yenyewe.

saa zingine afadhali wakae kimya tu
Hayo mashamba unalima bila kianzio si shida!
 
Hayo mashamba unalima bila kianzio si shida!
niko pori nafyeka msitu kila ekari 1 elfu 30 kakata miti na kung'oa visiki.

😜hadi nikwambie nilimpiga muhindi kiasi gani kwa kubeti nikaipeleka shamba, then hali ya hewa na Kilimo kilimo holela vikanipiga mweleka?

Mwaka ujao ntajuka kuotoa ushuhuda lakini Lazima ni tusue eka20 mwaka ujao wa Kilimo.
 
niko pori nafyeka msitu kila ekari 1 elfu 30 kakata miti na kung'oa visiki.

😜hadi nikwambie nilimpiga muhindi kiasi gani kwa kubeti nikaipeleka shamba, then hali ya hewa na Kilimo kilimo holela vikanipiga mweleka?

Mwaka ujao ntajuka kuotoa ushuhuda lakini Lazima ni tusue eka20 mwaka ujao wa Kilimo.
Kila la kheri mkuu
 
na pia inahitaji muda na subra sana. Mie mwaka huu nimelima ekari 10, bila mbolea wala mbegu za kisasa nimeambulia gunia chini ya gunia 20, alizeti gunia kadhaa, mahindi gunia kadhaa na mbaazi gunia kadhaa.

Mtu mwingine hawezi endelea na kilimo kwa matokeo haya. Inahitaji ustahimilivu mno.

Jukwaa la Kilimo wamenipa maarifa mwaka ujao wa kilimo zaidi nitusue. Nimeongeza ekari 10 nyingine zimekua 20. Hii yote ni matokeo ya kubeti. Saa zingine ubeti kunasaidia ila muhindi akinunua anakupiga mwaka mzima.
Mi nigekushauri uishi kizombi alafu izo gunia ulizopata ziwe mtaji ulime kisasa mbolea mbegu za kisasa ila usiongeze maana eneo kubwa mavuno kidogo.
Ukikomaa hapo hapo msimu unaofuata ndio uongeze baada ya kupata mavuno mazuri.
 
na pia inahitaji muda na subra sana. Mie mwaka huu nimelima ekari 10, bila mbolea wala mbegu za kisasa nimeambulia gunia chini ya gunia 20, alizeti gunia kadhaa, mahindi gunia kadhaa na mbaazi gunia kadhaa.

Mtu mwingine hawezi endelea na kilimo kwa matokeo haya. Inahitaji ustahimilivu mno.

Jukwaa la Kilimo wamenipa maarifa mwaka ujao wa kilimo zaidi nitusue. Nimeongeza ekari 10 nyingine zimekua 20. Hii yote ni matokeo ya kubeti. Saa zingine ubeti kunasaidia ila muhindi akinunua anakupiga mwaka mzima.
Mkuu Sasa ulitegemea muujiza gani kulima bila mbolea na mbegu za Kisasa? Bora ungelima.ekari 2
 
Aache yeye kazi ya udc aingie huko kwenye kilimo

Ova
 
Viongozi wa serikali wamekariri wakiwa wanaongea na raia points ni zile zile;
-Poor infrastructure
-Lack of capital
-cheap labor
-Lack of resources

Hizo points ilikuwa ukiwa nazo basi mtihani wa history, civics hupati O
 
Sio kwamba vijana hawataki kulima shida ya kwanza kabisa ni mtaji wa kupata shamba alafu kuna mbolea, mbegu zilizokua bora, dawa za kuulia wadudu na hapo hujawaza kuhusu mvua,

nadhani kama serikali itaongeza nguvu zaidi huku kwenye kilimo vijana na wasiokula vijana wata hamasika
tuu kulima,
kwa maana ya ijenge viwanda vya mbolea na madawa ya kuulia wadudu mashambani ili vipatikane kwa wingi Sana, iwekeze kwenye kufanya tafiti zaidi za kupata mbegu bora ili kuongeza uzalishaji na kupima ardhi za maeneo yote nchini ili wanaotaka kulima wajue kabisa zao fulani linashika vizuri eneo fulani, lakini pia serikali ije na mipango wezeshi ili kuhakikisha wakulima hawategemei mvua pekee kustawisha mazao
Na pia Yale maeneo ya serikali ambayo yapo tuu hayana shughuli zozote yawe kama mtaji kwa wanao hitaji kulima, wakifanya hayo yote watakua na nguvu ya kuwauliza watu kwa nini hawalimi
 
Badala awape tractor anawapa majembe!!!! . Solution pekee ya nchii hii kutajirika kupitia kilimo ni serikali kugawa ma tractor vijijini na kuchimba visima basi

Viongozi wangekuwa na akili wangefanya hivo
 
Huyu makende! Nae amekunywa mataputapu ya wapi sijuhi! Unanunua majembe 500 ya, Nikon, uwape vijana wakalime ili wapate ajira, na kuleta mapinduzi, ya kilimo?!
Hii nchi imeoza kuanzia kichwani!
Jaribu hata kuangalia na kuuliza wanaolima wanatumia mbinu gani sio kuleta story za kijinga!
Mzee Pinda analima sana Dodoma, anafuga na nyuki, unafikiri anatumia majembe ya mkono?
DC wa, zamani, Hapi, analima mpunga,pilipili, nk, unafikiri analima tu bila kuwa na uhakika wa soko? Unafikiri mie kapuku nikalime mahindi, nikishavuna Hilo soko nalipataje? Unafikiri ni rahisi kwangu kupata soko kama Hapi na Pinda,ambao wanaweza kutumia connections zao kuweka Mambo sawa!
Wewe kama DC toa mfano wa kilimo unachofanya!
U kweli mchungu, nchi haitaendelea kwa kuwa na wana nchi wengi wakulima, sasa hv80%ya wa bongo wanafanya kilimo! Inabidi 80 %wawe viwandani, na, 20%ndio wawe wakulima!
Mambo yq kilimo yameimbwa tangu awamu ya kikwete ya kilimo kwanza, wakaishia kununua magari na kujipa posho tu,
 
Back
Top Bottom