DC Mboni Mhita: Mkandarasi aliyeng'oa milango kisa deni aliirudisha na shughuli zinaendelea kama kawaida

DC Mboni Mhita: Mkandarasi aliyeng'oa milango kisa deni aliirudisha na shughuli zinaendelea kama kawaida

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
20240811_141638 (1).jpg
Imeelezwa kuwa milango ambayo iling’olewa na Mkandarasi katika Kituo cha Afya cha Bulige, Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga, ilirejeshwa na shughuli zinaendelea kama kawaida.

Awali Mkandarasi aling’oa milango kwa madai ya kuwa hajalipwa gharama za kazi yake kutoka kwa Ofisi ya Mkurugenzi, Mkuu wa Wilaya amefafanua.

Kuhusu kilichotokea bofya hapa ~ Mkandarasi ang'oa milango ya kituo cha afya cha Bulige akilalamika kutolipwa pesa zake

MKUU WA WILAYA
Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Mboni Mhita amesema suala hilo lilishamalizwa muda kidogo, kulitokea kutoelewana kati ya Mkandarasi na Mkurugenzi na hata wakati anang’oa milango kulikuwa na mazungumzo yanaendelea baina ya pande mbili.

Anasema “Mambo yaliwekwa sawa na mchakato wa malipo ukaendelea, milango ikarejeshwa na kila kitu kipo sawa.

“Sijui aliwaza nini huyo Mkandarasi, kwani walikuwa wameshakubaliana juu ya malipo, inawezekana alighafilika au labda kuna maneno alisikia, maana alikuwa anadai Ofisi ya Mkurugenzi, yeye anaenda kuondoa milango ambayo inatumiwa na watu wengi.

“Halikuwa jambo jema, tunachofurahia ni kuwa kila kitu kimekaa sawa na huduma zinaendelea kama kawaida.”
20240811_141400.jpg

20240811_140221.jpg

20240811_140654.jpg
 
Hizo kazi za halmashauri ni kama kamari tu, kuna mmoja nilimwona akimlilia mh makonda baada ya nyumba zake mbili pamoja na magari yake kupigwa mnada na bank baada ya kushindwa kulipa mkopo aliouchukua na kufanyia kazi ya kujenga madarasa ya shule huko wilayani monduli, hizo fedha amezidai kwa zaidi ya miaka miwili, alidai kuwa kwa sasa anaishi kwenye kijinyumbq kidogo yeye na familia yake, imagine,V8 lake pamoja na pick up jumlisha nyumba mbili kuuzwa kwa uzembe wa serikali, mtu hashindwi kujitoa roho.
 
Hao watu huwa Wana taka mazoea, Sasa hapa wame kutana na ngumu kumeza.

Ila huenda huo deal ilikuwa ya mkurugenzi aliye pita, Sasa huyu mpya naona kaona mtonyo mrefu?!
 
Hizo kazi za halmashauri ni kama kamari tu, kuna mmoja nilimwona akimlilia mh makonda baada ya nyumba zake mbili pamoja na magari yake kupigwa mnada na bank baada ya kushindwa kulipa mkopo aliouchukua na kufanyia kazi ya kujenga madarasa ya shule huko wilayani monduli, hizo fedha amezidai kwa zaidi ya miaka miwili, alidai kuwa kwa sasa anaishi kwenye kijinyumbq kidogo yeye na familia yake, imagine,V8 lake pamoja na pick up jumlisha nyumba mbili kuuzwa kwa uzembe wa serikali, mtu hashindwi kujitoa roho.
Haya wanawafanyia watanzania wenzao tu lakini wakikutana na mabeberu wanalipa na riba juu.
 
Hata ningekua mie, sijalipwa changu na blaah blaah nyingii, nang'oa, sitakiii utapelii mie. Lol
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hizo kazi za halmashauri ni kama kamari tu, kuna mmoja nilimwona akimlilia mh makonda baada ya nyumba zake mbili pamoja na magari yake kupigwa mnada na bank baada ya kushindwa kulipa mkopo aliouchukua na kufanyia kazi ya kujenga madarasa ya shule huko wilayani monduli, hizo fedha amezidai kwa zaidi ya miaka miwili, alidai kuwa kwa sasa anaishi kwenye kijinyumbq kidogo yeye na familia yake, imagine,V8 lake pamoja na pick up jumlisha nyumba mbili kuuzwa kwa uzembe wa serikali, mtu hashindwi kujitoa roho.
Hakuchizikaa kweliiii? Woiiiiiih
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom