DC Meatu asitisha shughuli za Ibada Makanisa yasiyo na vyoo

DC Meatu asitisha shughuli za Ibada Makanisa yasiyo na vyoo

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760

Mkuu wa Wilaya ya Meatu Mkoani Simiyu Mhe.Faudhia Ngatumbura amesitisha shughuli za ibada katika baadhi ya makanisa Wilayani Meatu mpaka Makanisa hayo yatapokuwa yamejenga vyoo ili kuwanusuru Wananchi kuugua ugonjwa hatari wa Kipindupindu.

Amezitaka Taasisi Dini Wilayani Meatu kuwa Mfano wa kuigwa katika ujenzi wa vyoo Bora ili kuhamasisha Jamii kujenga vyoo Bora hatua itakayosaidia Wananchi kujihadhari na ugonjwa Hatari wa kipindupindu.

Ametoa maagizo na Rai hiyo alipofanya Ukaguzi wa usafi wa Mazingira katika Kaya na Taasisi mbalimbali ikiwemo Makanisa katika Kata ya Mbugayabanya katika kuadhimisha Siku ya Usafishaji Kimkoa Wilayani humo.

"Mtendaji nakuagiza shughuli za ibada katika makanisa haya zisimame mpaka watakapokuwa wamejenga vyoo Bora ili Wananchi wasipate magonjwa ya kipindupindu"

Watu 47 wameripotiwa kupata ugonjwa wa kipindupindu katika Kata ya Mbogayabanya huku 3 wakipoteza maisha tangu kuingia kwa ugonjwa huo katika Kata hiyo Wilayani Meatu.

Pia soma:
~
Katibu Tawala Simiyu: Elimu ya kujikinga na Kipindupindu kutolewa kwa Lugha ya Kisukuma na Kiswahili
~ Kipindupindu Simiyu kimeshamiri, kinaua ni hatari! Mbona Serikali haiweki wazi 'status' ipoje?
~ Wataalam wa Afya waingia mtaani kufanya jitihada za kudhibiti magonjwa ya kuhara Mkoani Simiyu
 
Mkuu wa Wilaya ya Meatu Mkoani Simiyu Mhe.Faudhia Ngatumbura amesitisha shughuli za ibada katika baadhi ya makanisa Wilayani Meatu mpaka Makanisa hayo yatapokuwa yamejenga vyoo ili kuwanusuru Wananchi kuugua ugonjwa hatari wa Kipindupindu.

Amezitaka Taasisi Dini Wilayani Meatu kuwa Mfano wa kuigwa katika ujenzi wa vyoo Bora ili kuhamasisha Jamii kujenga vyoo Bora hatua itakayosaidia Wananchi kujihadhari na ugonjwa Hatari wa kipindupindu.

Ametoa maagizo na Rai hiyo alipofanya Ukaguzi wa usafi wa Mazingira katika Kaya na Taasisi mbalimbali ikiwemo Makanisa katika Kata ya Mbugayabanya katika kuadhimisha Siku ya Usafishaji Kimkoa Wilayani humo.

"Mtendaji nakuagiza shughuli za ibada katika makanisa haya zisimame mpaka watakapokuwa wamejenga vyoo Bora ili Wananchi wasipate magonjwa ya kipindupindu"

Watu 47 wameripotiwa kupata ugonjwa wa kipindupindu katika Kata ya Mbogayabanya huku 3 wakipoteza maisha tangu kuingia kwa ugonjwa huo katika Kata hiyo Wilayani Meatu.

Pia soma:
~
Katibu Tawala Simiyu: Elimu ya kujikinga na Kipindupindu kutolewa kwa Lugha ya Kisukuma na Kiswahili
~ Kipindupindu Simiyu kimeshamiri, kinaua ni hatari! Mbona Serikali haiweki wazi 'status' ipoje?
~ Wataalam wa Afya waingia mtaani kufanya jitihada za kudhibiti magonjwa ya kuhara Mkoani Simiyu
I nashangaa wachungaji kujenga kanisa bila kuweka choo. Hii ni tabia ya baadhi ya watanzania kutokujali afya za watu. Unakuta mtu anauza chakula lakini haweki choo. Pia kuna mabasi ya baadhi ya mikoa yanapeleka abiria porini kuchimba dawa. Ajabu mabasi hayohayo hupita vituo vya mafuta ambavyo vina vyoo lakini hawawapeleki abiria kujisaidia huko. Hizi ni tabia za kishamba!
 
I nashangaa wachungaji kujenga kanisa bila kuweka choo. Hii ni tabia ya baadhi ya watanzania kutokujali afya za watu. Unakuta mtu anauza chakula lakini haweki choo. Pia kuna mabasi ya baadhi ya mikoa yanapeleka abiria porini kuchimba dawa. Ajabu mabasi hayohayo hupita vituo vya mafuta ambavyo vina vyoo lakini hawawapeleki abiria kujisaidia huko. Hizi ni tabia za kishamba!
 
Back
Top Bottom