DC Ubungo akwepa kujibu swali la utekaji wa Sativa, asema “No Comment”

DC Ubungo akwepa kujibu swali la utekaji wa Sativa, asema “No Comment”

mwanamwana

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2011
Posts
1,309
Reaction score
4,798

Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Hassan Bomboko amekwepa kujibu swali kuhusu nani aliyehusika katika madai ya utekaji wa Edgar Mwakabela, maarufu Sativa.

Bomboka alikwepa swali hilo akiwa katika kipindi cha Medani za siasa cha runinga ya Star TV, huku akieleza kuwa wajibu wa Serikali ni kulinda raia na mali zao.

Msingi wa Bomboko kuulizwa swali hilo ni kwa sababu Sativa aliyedaiwa kupotea Dar es Salaam Juni 23, 2024 na kupatikana Alhamisi Juni 27, 2024 katika pori la Hifadhi ya Taifa ya Katavi akiwa na majeraha mwili ni mkazi wa Wilaya ya Ubungo.

“Jambo hili sasa hivi halipaswi kujadilika katika kipindi hiki,”amesema DC Bomboko, mtangazaji alipoendelea kumuuliza kuhusu muhusika wa kitendo hicho alisisitiza, “no coment (sina la kusema).”

Hata hivyo akizungumzia tukio la kupatikana Sativa mkoani Katavi, Juni, 2024, Kamanda wa Polisi wa mkoa huo, Kaster Ngonyanyi alisema jeshi hilo linafanya uchunguzi kuwabaini waliohusika.

Pia soma
 
Watesaji(serikali)wanabahati Kwa kuwa wanaoongozwa(wananchi wa tz)ni maiti kama alivyowahi kusema jomo kenyata.Tungekuwa kama wakenya (wanajitambua) ingekuwa maandamano Nchi nzima kupinga uonevu wa bibi kiziwi Kwa watu wasio na hatia
 
Ningelikuwa mtangazi walah HUYU DC ningemtandika makofi.

Unaalikwa kwenda studio unaenda ujafika na kuulizwa maswali unajibu no comment HAWA ni viongozi WA namna Gani?

Mkuu wa WILAYA anakataa kuitwa mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wilaya hivi HAWA watu wanateuliwa kutoka wapi?

Mkuu wa WILAYA unaulizwa raia kutoka ENEO lako la kiutawala je amani IPO ENEO lako unajibu no comment so so stupid.

Yaaani ni sawa sawa mtu anasema watu wanajiteka na kwenda kujitupa katavi kutokea DSM na Bado anawachangia fedha za matibabu je Nini hiki?

Nauliza Mh Rais haya maboya unayateua kutoka wapi?
 
Weka basi ka Clip Mkuu wetu mbona unatupa maneno matupu
 
Ningelikuwa mtangazi walah HUYU DC ningemtandika makofi.

Unaalikwa kwenda studio unaenda ujafika na kuulizwa maswali unajibu no comment HAWA ni viongozi WA namna Gani?

Mkuu wa WILAYA anakataa kuitwa mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wilaya hivi HAWA watu wanateuliwa kutoka wapi?

Mkuu wa WILAYA unaulizwa raia kutoka ENEO lako la kiutawala je amani IPO ENEO lako unajibu no comment so so stupid.

Yaaani ni sawa sawa mtu anasema watu wanajiteka na kwenda kujitupa katavi kutokea DSM na Bado anawachangia fedha za matibabu je Nini hiki?

Nauliza Mh Rais haya maboya unayateua kutoka wapi?

View: https://x.com/Twaha_Mwaipaya/status/1814898549286400402
 
Ww na huyo mkuu wa wilaya mnatakiwa mpigwe makofi maana hata ww unamtaja cheo chake tu jina lake na kituo chake cha kazi hujavitaja kwa hiyo tuote ni mkuu wa wilaya ipi...
 
Tunahitaji wakuu wa wilaya na mikoa walioiva kiakili na uzoefu wa maisha katika jamii.
Hawa vijana wenye mihemko, bila kujua wanayoyazungumza au kuyatenda yana athari gani kwa jamii ni changamoto.
 
Nadhani kwa sababu za kiusalama asingejibu maswali ya mwandishi hasa kama upelelezi unaendelea.
Hata hivyo DC angesema Vyombo vya ulinzi na usalama bado vinafuatilia bado angekuwa ametumia hekima kuliko kujibu kwa kujihami kwamba no comment.
 
Nadhani kwa sababu za kiusalama asingejibu maswali ya mwandishi hasa kama upelelezi unaendelea.
Hata hivyo DC angesema Vyombo vya ulinzi na usalama bado vinafuatilia bado angekuwa ametumia hekima kuliko kujibu kwa kujihami kwamba no comment.
Asingejibu au angejibu?
Majibu yanaweza kuwa upelelezi unaendelea, tutawasaka, tuwapeleke kwenye mkondo wa sheria. Usalama wa raia ndiyo kipaumbele cha serikali.
No comment siyo sawa hata kidogo.
 
Back
Top Bottom