The Watchman
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 896
- 1,427
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Lazaro Twange ameonyeshwa kukerwa na wasimamizi wa Ujenzi wa darasa katika Shule ya Msingi Golani B kwa kushindwa kutoa vizuri baadhi ya taarifa alizozihitaji kuzifahamu kuhusu mradi huo, baada ya kufika hapo kukagua maendeleo ya Ujenzi.
DC Twange alifika katika eneo hilo Machi 3, 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake aliyoifanya ya kukagua miradi mitano ya elimu msingi katika Shule mbalimbali ikiwemo Millenia 3, Golani B na Kilungule ambapo amebaini baadhi ya miradi kuchelewa kwa sababu mbalimbali ikiwemo wakandarasi wa kutekeleza miradi hiyo kuchelewa kupatikana, huku akiamuru kuondoka na viongozi hao kwa ajili ya kusaidia upatikanaji wa taarifa muhimu alizozihitaji.
DC Twange alifika katika eneo hilo Machi 3, 2025 ikiwa ni sehemu ya ziara yake aliyoifanya ya kukagua miradi mitano ya elimu msingi katika Shule mbalimbali ikiwemo Millenia 3, Golani B na Kilungule ambapo amebaini baadhi ya miradi kuchelewa kwa sababu mbalimbali ikiwemo wakandarasi wa kutekeleza miradi hiyo kuchelewa kupatikana, huku akiamuru kuondoka na viongozi hao kwa ajili ya kusaidia upatikanaji wa taarifa muhimu alizozihitaji.