DCEA: Wanawake waongoza kutumia Skanka, Mapenzi yanatajwa kuwa chanzo

DCEA: Wanawake waongoza kutumia Skanka, Mapenzi yanatajwa kuwa chanzo

The Watchman

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
896
Reaction score
1,427

Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), Aretas James Lyimo amesema wamefanikiwa kukamata Kilogramu 1066.105 za dawa za kulevya,mililita 447 za dawa tiba zenye asili ya kulevya, kuteketeza hekari 157.4 za mashamba ya bangi.

Akizungumza na wanahabari Jumanne Novemba 12, 2024, Dar es Salaam na kueleza kuwa kati ya mwezi Oktoba na Novemba mwaka huu zimekamatwa kilogramu 687.2 za skanka na kilogramu moja ya hashishi eneo la Goba jijini Dar es Salaam.

Kamishna Jenerali Lyimo amesema kumekuwa na ongezeko la watumiaji wakubwa wa dawa za kulevya aina ya skanka ikiwa wanaoongoza ni wanawake, huku sababu ya ongezeko hilo ikitajwa kuwa kupambana na msongo wa mawazo ambao umekuwa ukiwasumbua haswa ukitokana na udanganyifu wanaokutana nao kwenye uhusiano wa kimapenzi.

Kamishna Jenerali Lyimo amesema sambamba na kukamata dawa hizo, wamemkamata muuzaji maarufu wa dawa hizo kutokea mkoani Dodoma ajulikanaye kama Suleiman Mbaruku Suleiman maarufu kama Nyada(52) pamoja na Kimwaga Msobi Lazaro (37), ambapo Nyanda alikuwa ni kinara wa uuzaji wa dawa hizo, na kwamba hatua za kisheria zinaendelea dhidi yake.

Aidha Kamishna Jeneral Lyimo ametoa wito kwa Watanzania kuachana na utumiaji, pamoja na uuzaji wa dawa za kulevya kwani serikali chini ya Rais Samia Suluhu Hassan imeongeza umakini wa kufuatilia na kudhibiti dawa hizo.

Soma pia: DCEA yakamata kilo 767.2 za dawa za kulevya katika operesheni maalum, 21 mbaroni
 

Uchunguzi uliofanywa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) umebaini kuwa wanawake ndiyo wateja wakubwa na watumiaji wa bangi aina ya skanka kwa madai ya kupunguza msongo wa mawazo.

Hilo limebainika wakati wa operesheni iliyofanyika katika kipindi cha Oktoba na Novemba iliyowezesha kukamatwa kilo 687.32 za skanka na kilo moja ya hashishi eneo la Goba jijini Dar es Salaam zikiwa zimefichwa ndani ya nyumba ya mtuhumiwa.

Kamishna Jenerali wa DCEA Aretas Lyimo amesema hay oleo Novemba 12 2024 na kuongeza kuwa, uchunguzi umebaini kuwa, kuna ongezeko la matumizi ya dawa hizo za kulevya kufuatia udhibiti wa dawa zilizokuwa zikitumika hapo awali.

“Katika uchunguzi wetu ambao tulifanya kwenye vijiwe, saluni na maeneo mbalimbali tulibaini watumiaji wakubwa wa skanka ni wanawake. Kuna ambao tulizungumza nao na hata mimi binafsi nimezungumza na baadhi ya wanawake wanakiri wanatumia skanka kujiondolea mawazo.

“Ukisikiliza sababu zao wengi wanashindwa kuhimili misongo ya mawazo inayotonakana na changamoto za uhusiano, hivyo wanakimbilia kwenye ulevi huo kwa kile wanachoamini inasaidia kupunguza mawazo,” amesema Kamishna Jenerali Lyimo.
 
Back
Top Bottom