DCs wapanguliwa na kustaafishwa

Kwa wilaya zilizopo mipakani nadhani kwa sababu za kuisalama na sometimes kuibabe,inabidi apewe mwanajeshi (hili nililishuhudia wilaya za Kigoma na kagera)

KWA SABABU WANASTAAFU NA UMRI MDOGO(57)na MAFAO YAO KIDOGO.PIA ALIKUA NAO JESHINI(kujuana).MWISHO SIJUI ni KWA USLAMA VILE.
 

Nsesi,

Sizijui hizo tuhuma zako na huenda ni za kweli ila mimi wacha nielezee upande wa pili wa DC wa Kyela. Huko nyuma niliwahi kuelezwa matendo mengi mabaya ya huyo DC na kuna wakati hata nilishaandika hapa JF. Kutokana na mambo ya kuelezwa na wengine, sikuona haja hata ya kuwasiliana naye kwa mambo yoyote ya maendeleo pale Kyela. Pia ninajua kuhusu kufamaniwa kwake na mkewe.

Lakini miezi kama minne iliyopita DC alinitafuta kwa ajili ya shughuli moja ya maendeleo Kyela. Nilishangaa lakini toka wakati huo nimekuwa nikiwasiliana naye mara kwa mara na nikashangaa kuona mambo niliyoambiwa na alivyo ni tofauti kabisa.

Kwa mimi naweza kusema katika viongozi wa Kyela ni mtu pekee ambaye mimi kama mwekezaji wilayani, alikuja kwetu na kutuuliza kama tuna shida ili atusaidie. Kwa kweli katika kipindi hicho cha miezi minne ametusaidia sana kwenye matatizo mbalimbali ya ufuatiliaji. Pia tumeshirikiana naye kwenye mambo mengine ya maendeleo ya wilaya.

Kwangu mimi Mashimba ni katika Watanzania wachache niliowahi kukutana nao maofisini ambao waliweza kusaidia bila kuombwa sana au kuahidiwa chochote.

Ningependa niseme kwa ukweli mtupu, pamoja na kutusaidia kote huko hajawahi kutuomba chochote wala hatujampatia chochote zaidi ya michango yetu kwenye maendeleo ya wilaya na ambayo imeenda moja kwa moja kwa walengwa.

Sikutaka kuandika haya ila baada ya kuona tuhuma zako, nimeona ni vizuri na mimi kueleza ninayoyajua.

Kinachonisikitisha mimi Kyela ni mgawanyiko wa watu na majungu mengi pembeni ambayo ndio yanakwamisha maendeleo.

Leo kuna watu wanasema kuondoka kwake ni kwasababu alikuwa haelewani na Mwakipesile. Mimi muda wote kabla ya kumfahamu nilikuwa najua haelewani na Dr. Mwakyembe.

Kitu ambacho Mashimba ameniambia mara nyingi kwa muda huo wa miezi minne niliyomfahamu ni kwamba wilaya ya Kyela ni ngumu sana kuongoza, watu wanachukiana mno, hawasahau hata chuki za miaka mitano iliyopita na alituomba sana sisi tukae katikati na kujiepusha na hayo makundi mawili.

Kama kuna mtu anamjua DC mpya, ni kumuambia mapema, kama kuna wilaya zinahitaji viboko basi Kyela ni mojawapo. Imejaa ujinga na majungu huku maendeleo zero. Inabidi toka mwanzo awaambie hawa waheshimiwa wawili kwamba vita vyao wasubiri 2010 na yeye achape kazi na viongozi wote. Sijui kama linawezekana lakini ndio ushauri pekee.
 
Ouwiii! Awe karibu zaidi na mkubwa. Maana kufungafunga safari za Korogwe kuna matatizo yake.

Mkuu Jasusi,

Inaelekea wewe na Mwawado kuna jambo mnajua zaidi lakini hamtaki kutuhabarisha.

Wakubwa wako wengi, ni nani huyo mkubwa wa Chamwino?
 
Mkuu Jasusi,

Inaelekea wewe na Mwawado kuna jambo mnajua zaidi lakini hamtaki kutuhabarisha.

Wakubwa wako wengi, ni nani huyo mkubwa wa Chimwano?

Mkubwa wa Chamwino ni mmoja tu. Ulishawahi kusikia Dr. Shein ana ofisi pale Chamwino? Mizengwe ofisi yake iko mjini Dodoma na pia ana makazi yake mjini Dodoma.

So by elimination anabaki mkubwa mmoja. Swali linakuja, je ndo kusema huyo Mama Mkwasa ni mali za huyo mkubwa? [samahani lakini sina nia ya udaku ama kuingilia maisha binafsi ya wakubwa wetu]
 
- Wakuu hivi kweli tunahitaji Wakuu wa wilaya Tanzania?FMES!
Unatutega?* si wewe unayejidai CCM damu sasa unamuuliza nani na nyie ndiyo mliandika katiba na hamtaki* katiba mpyaCCM ziiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii!
 
....kubadilishiwa vituo vya kazi madc 54 maana yake uhamisho.Gharama ya uhamisho hivi si kubwa sana?na ,je does it really worth it?
 
..nashangaa kanda2 na Chuma hawajaleta hoja zao za udini ktk teuzi hizi.

JokaKuu....Nilipoona post yako nikabaki kucheka tu...Tunahaja gani ya kuhoji wakati hakuna sababu hizo?...Mara nyingi wanaohoji ni wale ambao wanapoona tu teuzi zinapokwenda kwa waislam...!!!

Its Good watu wanahoji utendaji wa wahusika...

ES....kimsingi hatuna haja ya kuwa na wakuu wa Wilaya wala wakuu wa Mikoa...ni taratibu ambazo tumerithi kutoka kwa wakoloni...bahati mbaya pia hawa wakuu pamoja na kuteuliwa kwao kuwasaidia Rais na Wazir Mkuu, wamekuwa si wasaidizi makini zaid wamekuwa ma-opportnist fulani

Ipo Haja ya kureview mambo mengi ktk Cooperate Government studies. The same na utitiri aliousema Philimone Michael ktk mada fulani kuhusu znz...same na na Mainland tumejaza vyeo Lukuki sana. utendaji zero...

ktk Wakati huu wa Uchumi Legevu, wenzetu wa Kenya wameweka mkakati wa kutoajiri kwa nafasi ambazo hazina umuhim wa haraka...atleast tungeona GOT nayo inaanza na wakuu wa wilaya....i.e. Mfano DSM tuna wakuu wa wilaya 3 na Mkuu wa Mkoa 1,(total 4) tungeweza kabisa alau kuwa na wakuu wa wilaya 2, then mkuu wa Mkoa anakuwa pia mkuu wa wilaya ya Ilala....atleast tungepungza wakuu wengi sana...
 

Huyu wa mwisho amenikumbusha jambo na leo nataka kujaribu kuona yale ninayoyafikiria yapo humu ndani yaJF.
Katika hii orodha ya Wakuu wa Wilaya kuna Wislamu wangapi?
 

- Mkuu Chuma hapa tupo pamoja saafi sana yaani yako ni constructive argument inayotakwia kufikishwa kwa wahubwa wetu.

Respect.

FMES!
 
ES....kimsingi hatuna haja ya kuwa na wakuu wa Wilaya wala wakuu wa Mikoa...ni taratibu ambazo tumerithi kutoka kwa wakoloni

Hii ni kuwapakazia wakoloni! Hawakuwa na mikoa, walikuwa na Majimbo (Province) chini ya PC. Tanganyika nzima ilikuwa na Province kama saba tu.

We are very much overgoverned. Na angalau basi tungechagua sisi nani atutawale. DC na RC wachaguliwe na wananchi wa sehemu husika. It is done that way in all true democracies.

Obama katoa argument nzuri sana: You cannot do the same things over and over again and expect a different result!

Hawa ma DC wa kubandikwa na Rais ni Msalaba tu wanaobebeshwa wananchi.
 
Hatuhitaji wakuu wa wilaya kama tuna wakuu wa mikoa kuna wabunge kila pembe jimbo vichochoro wa nini hawa jamani. Hawa watu hawana moja wala mbili ni gharama tu zisizokuwa na msingi.Baada ya uchaguzi kutakuwa na reshufle nyingine si kuingiziana gharama zisizokuwa na msingi alikuwa wapi siku zote kufanya mabadiliko haya aje ayafanye leo. Hawa watu kwa kweli ni mzigo tu hakutakuwa na maendeleo yoyote. watu wa nchi za magharibi wanapunguza gharama zisizo na msingi bongo ndio kwanza tunaongeza gharama kila kukicha kweli bongo tambarareeeeeeziiiiiiiiii
 
Elizabeth Mkwasa kahamishiwa BAHI - Dodoma karibu na Ikulu ya Chamwino!!

Out of curiosity .... Chamwino ni Ikulu ndogo ya JK, kwa hiyo ndo kusema Elizabeth Mkwasa ni nanihiino ndogo ya Ikulu?

Mkuu Keil,

Umeniwahi, nilitaka kuuliza swali hilo hilo, anyway tuache tusije tukaambiwa tunadhalilisha dada zetu.

Ouwiii! Awe karibu zaidi na mkubwa. Maana kufungafunga safari za Korogwe kuna matatizo yake.

Udhalilishaji usio kifani, hivi kama Kocha anaingia humu si inaweza kumletea tatizo kichwani.
 
Hivi kocha bado ana chake pale??au kwisney???maana sielewi elewi....au imebakia mazoea tu??
 
Mhe rais amewastaafisha wakuu wa wilaya 7 na wengine kuwahamisha katika sehemu zao za kazi
 
Ipole upo wapi wewe?????hii sio habari mpya atii...imetoka jana mchana...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…