Debora Tluway Afika Tunguu, Chuo cha UVCCM

Debora Tluway Afika Tunguu, Chuo cha UVCCM

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

DEBORA TLUWAY AFIKA TUNGUU, CHUO CHA UVCCM

Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji UVCCM Mkoa, Komredi Debora Joseph Tluway tarehe 15 Desemba 2024 ametembelea Chuo cha Umoja wa Vijana wa CCM Tunguu Zanzibar na kuona miradi na mikakati mbalimbali inayotekelezwa ikiwemo Ufugaji wa Kuku wa Mayai na ujenzi wa majengo Chuoni hapo ambao unaendelea sasa hivi.

Debora Joseph Tluway ameweka jiwe la msingi la Ofisi ya Kundi la Umoja wa Vijana wa CCM K.K.V Kiomba - Mvua ambapo amechangia Matofali 500 na viongozi wengine pia Wabunge na Madiwani wamechangia K.K.V ili kusaidia ujenzi wa kisima cha maji

"Mwaka 2025 kuna uchaguzi mkuu wa Rais wa Zanzibar, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wabunge na Madiwani. Naomba tuwape nafasi wagombea wote wanaotokana na CCM. Muda ukiwadia twende Tukajiandikishe kwenye Daftari la Mpiga Kura ili tuwape nafasi viongozi wanaotokana na CCM" - Komredi Debora Joseph Tluway

Akiambatana na viongozi wengine UVCCM, Debora Joseph Tluway ametembelea Kaburi la aliyekuwa Rais wa Awamu ya Pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Ali Hassan Mwinyi Mangapwani. Pia, amezindua amsha amsha ya Upashikaji wa Bendera kwa Mabalozi; Ametembelea Bandari ya Mafuta Mangapwani

Vilevile, Debora Joseph Tluway amezindua Mashindano ya Vijana 50 ya Uendeshaji wa Baiskeli yanayoendelea katika Jimbo la Chaani na amempongeza Mbunge wa Jimbo la Chaani, Mhe. Juma Usonge kwani amekuwa Kiongozi anayefikika, anasikiliza Vijana na anafanya kazi kwa vitendo.
 

Attachments

  • KKV.mp4
    55 MB
  • BASKELI.mp4
    79.6 MB
  • AMSHA.mp4
    79 MB
  • WhatsApp Image 2024-12-15 at 16.25.27.jpeg
    WhatsApp Image 2024-12-15 at 16.25.27.jpeg
    264.7 KB · Views: 4
  • WhatsApp Image 2024-12-15 at 16.25.26.jpeg
    WhatsApp Image 2024-12-15 at 16.25.26.jpeg
    306.1 KB · Views: 4
  • WhatsApp Image 2024-12-15 at 16.25.30 (1).jpeg
    WhatsApp Image 2024-12-15 at 16.25.30 (1).jpeg
    259.2 KB · Views: 3
  • WhatsApp Image 2024-12-15 at 16.25.28 (1).jpeg
    WhatsApp Image 2024-12-15 at 16.25.28 (1).jpeg
    220.3 KB · Views: 4
  • WhatsApp Image 2024-12-15 at 16.25.30.jpeg
    WhatsApp Image 2024-12-15 at 16.25.30.jpeg
    303.5 KB · Views: 4
  • WhatsApp Image 2024-12-15 at 16.25.29.jpeg
    WhatsApp Image 2024-12-15 at 16.25.29.jpeg
    245.3 KB · Views: 6
  • WhatsApp Image 2024-12-15 at 16.25.36.jpeg
    WhatsApp Image 2024-12-15 at 16.25.36.jpeg
    274.2 KB · Views: 4
  • WhatsApp Image 2024-12-15 at 16.25.33.jpeg
    WhatsApp Image 2024-12-15 at 16.25.33.jpeg
    278.6 KB · Views: 5
  • WhatsApp Image 2024-12-15 at 21.16.02.jpeg
    WhatsApp Image 2024-12-15 at 21.16.02.jpeg
    144.3 KB · Views: 4
  • WhatsApp Image 2024-12-15 at 21.16.10.jpeg
    WhatsApp Image 2024-12-15 at 21.16.10.jpeg
    125.7 KB · Views: 6
  • WhatsApp Image 2024-12-15 at 21.16.17.jpeg
    WhatsApp Image 2024-12-15 at 21.16.17.jpeg
    245.3 KB · Views: 3
  • WhatsApp Image 2024-12-15 at 21.16.19.jpeg
    WhatsApp Image 2024-12-15 at 21.16.19.jpeg
    222.2 KB · Views: 3
Mnajaza seva tu kwani yale mabango ya uhuru nk yameporomoka?
 
Back
Top Bottom