Jpinduzi
Senior Member
- Feb 26, 2011
- 136
- 68
Ikiwa zimebaki wiki chache kabla ya kuanza sikukuu mfululizo, hatuna budi kumshukuru Mungu kwa uwezo wake na mapenzi yake kutuacha hai mpaka siku hii ya leo tunapoelekea mwisho wa mwaka. Hakika tuna kila sababu ya kumshukuru Mungu kwa hilo!
Katika mwezi Desemba wa kila mwaka, kuna mambo mengi ambayo hutokea hasa kwa wapendanao. Hakika ni mwezi mzuri sana kwa wale ambao ni waaminifu na wenye mapenzi ya kweli yasiyo na migogoro, lakini pia ni mwezi mbaya sana kwa wale ambao watahitilafiana na wapenzi wao.
Katika mwezi Desemba mambo mengi hutokea, kuna ambao huachana na wapenzi, kuna ambao hupata wapenzi wapya, lakini suala la msingi ni kuwa makini na kuhakikisha humuudhi mpenzi wako.
Katika hayo mengi ambayo hutokea mwezi huu, yakiwemo mabaya na mema ni vyema ukawa makini ili kuhakikisha kuwa yanayokufika mwezi huu ni mema zaidi kuliko mabaya! Hakika yote yanawezekana kama ukiwa makini. Lakini pia kuna ambao ni wapweke na waliochomwa mioyo yao na wapenzi wao, huwa ni mwezi mbaya zaidi kwao. Pamoja na hayo, hebu fuatilia vipengele vifuatavyo kwa makini ili ujue jinsi ya kusherehekea sikukuu zijazo vyema pasipo matatizo.
WAPWEKE
Huenda katika siku za karibuni uliachana na mpenzi wako na sasa upo katika hali ya upweke, usijali bado unaweza kusherehekea sikukuu zinazokuja bila kuwa na sononeko moyoni mwako. Elewa jambo moja rafiki/shemeji yangu mpenzi, katika kipindi cha sikukuu mambo mengi hutokea ambayo wakati mwingine huathiri kwa kiasi kikubwa maisha ya watu mbalimbali.
Usilazimishe kutafuta mpenzi mpya haraka kwa nia ya kupata mtu wa kutoka naye ‘OUT' mwezi huu ulio na sikukuu kibao. Hakika ni hatari kwa sababu ni lazima utakuwa na mtu ambaye huna mapenzi ya dhati kwake, hata kama utakuwa umempenda ni wazi kuwa utakuwa umeamua kuwa naye kwa nia ya kuziba ufa ili usijione mpweke.
Nakuhakikishia kuwa japokuwa unaweza ukatafuta mtu wa kuwa naye siku hiyo kwa nia ya kujiondolea upweke, lakini badala ya kuondokewa na upweke inaweza kuwa siku mbaya zaidi kwako na kukuachia historia mbaya katika maisha yako.
Utakapotoka na mpenzi mpya ambaye umeamua kuwa naye kwa nia ya kuziba ufa, lolote linaweza kutokea! Pengine unatumia kilevi, baada ya kilevi kukolea unaweza ukajikuta ukifanya mapenzi na patina mpya bila kinga na hata kama ukitumia kinga usitumie kwa njia inayofaa.
Usitake mwezi huu ukawa mwezi mbaya kuliko miezi yote katika maisha yako ya kimapenzi, achana na ulimbukeni, kubaliana na hali halisi kuwa sasa huna mpenzi, amini kuwa mwezi huu unaweza kuwa mzuri bila kuwa na mpenzi.
Kimsingi unachopaswa kufanya ni kumuomba Mungu wako akupe amani katika moyo wako ili mwezi huu na hekakeha zake zote usije kuwa ni wa majonzi katika maisha yako.
WENYE WAPENZI
Hakika ni mwezi mzuri sana kwa ajili yenu, lakini pia unaweza kuwa mbaya sana kwenu. Ni mwezi ambao uamnifu wa mtu huonekana, uongo huonekana na mambo mengine mengi yaliyokuwa nyuma ya pazia huonekana kutokana na msongamano wa sikukuu. Ni siku mbaya sana kwa wale wasio waaminifu!
Katika siku za sikukuu hasa za mwisho wa mwaka, lazima kunakuwa na ratiba za mtoko na mpenzi wako, sasa kama una mpenzi zaidi ya mmoja ndipo hapo mambo yatakapoanza kuharibika, kwa sababu utatoka na yupi hasa, sababu kila anayemdanganya kuwa yuko peke yake hukutegemea na kukuhitaji kutoka na wewe ‘out' mkasherehekee pamoja.
Sasa basi kitakachotokea hapo baada ya kutoka na mwingine, huyo mwingine ambaye hujatoka naye lazima atapiga simu kila wakati na kukuandikia sms akitaka kujua kulikoni! Ni hapo sasa balaa litakapoanzia hasa kama mpenzi uliyenaye atafuma sms hizo.
Uaminifu hauhitajiki mwezi huu pekee, uaminifu ni silaha madhubuti kwa ajili ya wapendanao na siku zote tunapaswa kuzingatia uaminifu kwa wapenzi wetu. Tambua kuwa dunia sio yako, fanya ufanyayo lakini elewa kuwa unafanya vibaya na mwisho wake hautakuwa mzuri.
Jitahidi kutomuumiza mwenzako mwezi huu, ni mwezi wa furaha kwako na kwa mpenzi wako, sasa ukimwumiza mpenzi wako na kumwachia doa katika moyo wake, elewa kuwa sio tabia nzuri na utakuwa mwanzo mbaya wa maisha mapya katika mwaka mpya ujao. Usiruhusu mtu akamwaga machozi kwa ajili yako siku hiyo! Kwa sababu machozi hayo lazima utayalipia, kwa bahati mbaya sana malipo yake sio madogo, yatakugharimu sana maisha yako na yanaweza kuathiri maisha yako yote!
Katika mwezi Desemba wa kila mwaka, kuna mambo mengi ambayo hutokea hasa kwa wapendanao. Hakika ni mwezi mzuri sana kwa wale ambao ni waaminifu na wenye mapenzi ya kweli yasiyo na migogoro, lakini pia ni mwezi mbaya sana kwa wale ambao watahitilafiana na wapenzi wao.
Katika mwezi Desemba mambo mengi hutokea, kuna ambao huachana na wapenzi, kuna ambao hupata wapenzi wapya, lakini suala la msingi ni kuwa makini na kuhakikisha humuudhi mpenzi wako.
Katika hayo mengi ambayo hutokea mwezi huu, yakiwemo mabaya na mema ni vyema ukawa makini ili kuhakikisha kuwa yanayokufika mwezi huu ni mema zaidi kuliko mabaya! Hakika yote yanawezekana kama ukiwa makini. Lakini pia kuna ambao ni wapweke na waliochomwa mioyo yao na wapenzi wao, huwa ni mwezi mbaya zaidi kwao. Pamoja na hayo, hebu fuatilia vipengele vifuatavyo kwa makini ili ujue jinsi ya kusherehekea sikukuu zijazo vyema pasipo matatizo.
WAPWEKE
Huenda katika siku za karibuni uliachana na mpenzi wako na sasa upo katika hali ya upweke, usijali bado unaweza kusherehekea sikukuu zinazokuja bila kuwa na sononeko moyoni mwako. Elewa jambo moja rafiki/shemeji yangu mpenzi, katika kipindi cha sikukuu mambo mengi hutokea ambayo wakati mwingine huathiri kwa kiasi kikubwa maisha ya watu mbalimbali.
Usilazimishe kutafuta mpenzi mpya haraka kwa nia ya kupata mtu wa kutoka naye ‘OUT' mwezi huu ulio na sikukuu kibao. Hakika ni hatari kwa sababu ni lazima utakuwa na mtu ambaye huna mapenzi ya dhati kwake, hata kama utakuwa umempenda ni wazi kuwa utakuwa umeamua kuwa naye kwa nia ya kuziba ufa ili usijione mpweke.
Nakuhakikishia kuwa japokuwa unaweza ukatafuta mtu wa kuwa naye siku hiyo kwa nia ya kujiondolea upweke, lakini badala ya kuondokewa na upweke inaweza kuwa siku mbaya zaidi kwako na kukuachia historia mbaya katika maisha yako.
Utakapotoka na mpenzi mpya ambaye umeamua kuwa naye kwa nia ya kuziba ufa, lolote linaweza kutokea! Pengine unatumia kilevi, baada ya kilevi kukolea unaweza ukajikuta ukifanya mapenzi na patina mpya bila kinga na hata kama ukitumia kinga usitumie kwa njia inayofaa.
Usitake mwezi huu ukawa mwezi mbaya kuliko miezi yote katika maisha yako ya kimapenzi, achana na ulimbukeni, kubaliana na hali halisi kuwa sasa huna mpenzi, amini kuwa mwezi huu unaweza kuwa mzuri bila kuwa na mpenzi.
Kimsingi unachopaswa kufanya ni kumuomba Mungu wako akupe amani katika moyo wako ili mwezi huu na hekakeha zake zote usije kuwa ni wa majonzi katika maisha yako.
WENYE WAPENZI
Hakika ni mwezi mzuri sana kwa ajili yenu, lakini pia unaweza kuwa mbaya sana kwenu. Ni mwezi ambao uamnifu wa mtu huonekana, uongo huonekana na mambo mengine mengi yaliyokuwa nyuma ya pazia huonekana kutokana na msongamano wa sikukuu. Ni siku mbaya sana kwa wale wasio waaminifu!
Katika siku za sikukuu hasa za mwisho wa mwaka, lazima kunakuwa na ratiba za mtoko na mpenzi wako, sasa kama una mpenzi zaidi ya mmoja ndipo hapo mambo yatakapoanza kuharibika, kwa sababu utatoka na yupi hasa, sababu kila anayemdanganya kuwa yuko peke yake hukutegemea na kukuhitaji kutoka na wewe ‘out' mkasherehekee pamoja.
Sasa basi kitakachotokea hapo baada ya kutoka na mwingine, huyo mwingine ambaye hujatoka naye lazima atapiga simu kila wakati na kukuandikia sms akitaka kujua kulikoni! Ni hapo sasa balaa litakapoanzia hasa kama mpenzi uliyenaye atafuma sms hizo.
Uaminifu hauhitajiki mwezi huu pekee, uaminifu ni silaha madhubuti kwa ajili ya wapendanao na siku zote tunapaswa kuzingatia uaminifu kwa wapenzi wetu. Tambua kuwa dunia sio yako, fanya ufanyayo lakini elewa kuwa unafanya vibaya na mwisho wake hautakuwa mzuri.
Jitahidi kutomuumiza mwenzako mwezi huu, ni mwezi wa furaha kwako na kwa mpenzi wako, sasa ukimwumiza mpenzi wako na kumwachia doa katika moyo wake, elewa kuwa sio tabia nzuri na utakuwa mwanzo mbaya wa maisha mapya katika mwaka mpya ujao. Usiruhusu mtu akamwaga machozi kwa ajili yako siku hiyo! Kwa sababu machozi hayo lazima utayalipia, kwa bahati mbaya sana malipo yake sio madogo, yatakugharimu sana maisha yako na yanaweza kuathiri maisha yako yote!