DED Makete, William Makufwe awataka wakulima wa Ngano kuwa na imani na Serikali. Soko lipo kupitia kampuni ya Bakhresa

DED Makete, William Makufwe awataka wakulima wa Ngano kuwa na imani na Serikali. Soko lipo kupitia kampuni ya Bakhresa

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301
Wakulima wa zao la Ngano Wilayani Makete, wameshauriwa kutumia Mashine bora za kisasa katika Uvunaji wa zao hilo, ambao umeshanza rasmi katika baadhi ya Maeneo ikiwemo kijiji Cha Mlengu kilichopo Kata ya Kigala.

Ushauri huo umetolewa Julai 13, 2024, na Mkuu wa Wilaya ya Makete, Mhe. Juma Samwel Sweda, wakati wameongozana na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Makete, Ndg. William M. Makufwe, katika Ukaguzi wa shughuli za Uvunaji wa zao hilo katika mashamba hayo yenye ukubwa wa zaidi ya Ekari mia tatu.

Ikumbukwe kuwa, ni wiki Moja tu imepita tangu Mkurugenzi huyo, wa Halmashauri ya Wilaya ya Makete, alipotembelea mashamba hayo, ambapo aliwataka wakulima hao kuwa na Imani na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwakuwa soko la zao hilo lipo Kwa asilimia miamoja kupitia Kampuni ya Bakhiresa iliyopo Jijini Dar es Salaam.

Hata hivyo, Uvunaji wa zao la Ngano, umeanza rasmi Julai 13, 2024, katika Mashamba hayo yaliyopo kijiji cha Mlengu, Kata ya Kigala, Wilaya ya Makete, mkoani Njombe.

Screenshot 2024-07-15 at 10-50-15 Makete Dc Wakulima wa zao la Ngano Wilayani Makete wameshaur...png
Screenshot 2024-07-15 at 10-50-36 Makete Dc Wakulima wa zao la Ngano Wilayani Makete wameshaur...png
 
Wakulima wa zao la Ngano Wilayani Makete, wameshauriwa kutumia Mashine bora za kisasa katika Uvunaji wa zao hilo, ambao umeshanza rasmi katika baadhi ya Maeneo ikiwemo kijiji Cha Mlengu kilichopo Kata ya Kigala.

Ushauri huo umetolewa Julai 13, 2024, na Mkuu wa Wilaya ya Makete, Mhe. Juma Samwel Sweda, wakati wameongozana na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Makete, Ndg. William M. Makufwe, katika Ukaguzi wa shughuli za Uvunaji wa zao hilo katika mashamba hayo yenye ukubwa wa zaidi ya Ekari mia tatu.

Ikumbukwe kuwa, ni wiki Moja tu imepita tangu Mkurugenzi huyo, wa Halmashauri ya Wilaya ya Makete, alipotembelea mashamba hayo, ambapo aliwataka wakulima hao kuwa na Imani na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwakuwa soko la zao hilo lipo Kwa asilimia miamoja kupitia Kampuni ya Bakhiresa iliyopo Jijini Dar es Salaam.

Hata hivyo, Uvunaji wa zao la Ngano, umeanza rasmi Julai 13, 2024, katika Mashamba hayo yaliyopo kijiji cha Mlengu, Kata ya Kigala, Wilaya ya Makete, mkoani Njombe.

View attachment 3042809View attachment 3042810
Hatimaye ngano imeingia kwenye biashara rasmi sasa. Hongereni
 
Yaani Serikali ndio iwanunuliea mashine za kuvunia?Wanailimia Serikali? tuna safari ndefu mno
Kima wewe,upatikanaji sio maana yake serikali iwanunulie.Taarifa kuhusu hizo mashine kama bei na mahali zinakopatikana je wakulima wanafahamu?
Nchonyo wako huo.
 
Wakulima wengi walipewa Ngano wengine wakaenda kuibadilisha na Lita ya komoni . Na awajapanda
 
Kwa ufupi Ngano maandalizi yanaanza kuanzia mwezi February adi April mwanzoni ndo upandaji unafanyika na uvunaji unaanza July hadi agosti
 
Back
Top Bottom