Delaska Management mwenye A, B, C zake naomba mtujuze!

Delaska Management mwenye A, B, C zake naomba mtujuze!

FK21

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2019
Posts
8,600
Reaction score
10,760
Wakubwa nawasalimu kwa jina la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania!

Nmekuja hapa kuuliza kwenu juu ya hii kitu inayoitwa DELASKA AGENCY naona watu wanavuna pesa; je uhalisia upoje?

Naona pia nyingine inaitwa IDEABETA naona watu wanaweka laki 2 akikaa week ana toa laki 4?

Je, life imekuwa simple hivi nowdays?
 
Nimesita kujiunga nayo, si ndio ile unaweka elfu 13 alafu unapata faida ?
 
Hiyo Delaska wanatamba sana siku hizi kuna rafiki zangu wawili wapo ila mimi sina imani na pesa za mitandao kabisa
 
Nami kuna mtu ananisumbua sana kujiunga na hii kitu kama wiki tatu zilizopita, na hapa kanitumia ujumbe kunikumbushia juu ya kujiunga ...

Kanuni yangu ni kwamba hakuna pesa ya bure bure kirahisi dunia hii hivyo huwa sishawishiki na vitu kama hivi.

Nawahurumia sana wale wanao amini huko mafanikio yapo kirahisi. ..poleni saana ni suala la muda tuu mtaelewa juu ya hiyo delaska. (Delaska/sakadera sijui)
 
Nami kuna mtu ananisumbua sana kujiunga na hii kitu kama wiki tatu zilizopita, na hapa kanitumia ujumbe kunikumbushia juu ya kujiunga ...

Kanuni yangu ni kwamba hakuna pesa ya bure bure kirahisi dunia hii hivyo huwa sishawishiki na vitu kama hivi.

Nawahurumia sana wale wanao amini huko mafanikio yapo kirahisi. ..poleni saana ni suala la muda tuu mtaelewa juu ya hiyo delaska. (Delaska/sakadera sijui)
Hata namba zao ni za kawaida hizi,pia namba wanayokupa utume pesa Ina jina la mtu
 
walipotini mahali husika ili wakayatapike hayo mahela ya wajinga wanayoyakusanya
 
Watanzania wana akili za nyumbu. Wanapigwa wakikaa wiki mbili wameshasahau, akija mwingine anapiga tena... wanasahau, wanapigwa, wanasahau, wanapigwa......

Ukiwa mjinga halafu ukawa na tamaa ni janga kubwa sana kwa familia,ukoo, na taifa kwa ujumla.

Kanuni ya fedha huwa haiwi rahisi hivyo....eti weka 50,000/- halafu baada ya wiki unapata laki😛

Ila kwa ujinga na tamaa ya watanzania wengi, bado watatapeliwa na hao DELASKA
 
😂 😂 😂 😂 😂 😂 😂 😂 😂 😂 😂 😂 😂😂😂😂
Paaaaaaah! Jiwe hilo gizani
Kuna mdogo wangu mmoja niliona kaanza kupost hz mambo baadae akaja kunambia nijiunge nkamjibu ww si ushapata hela nikopeshe hyo elf 13 nijiunge sjamsikia tena mpka muda huu
 
Watanzania wajinga hawajawahi kukosekana tena kwa wingi,
Tuma kwenye namba hii jina litatokea Mamushka!
 
Back
Top Bottom