Demokrasia katika ngazi ya Serikali za Mitaa huanza kwa ushirikishwaji wa Wananchi katika Mipango ya Maendeleo

Demokrasia katika ngazi ya Serikali za Mitaa huanza kwa ushirikishwaji wa Wananchi katika Mipango ya Maendeleo

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Joined
Aug 7, 2018
Posts
685
Reaction score
1,124
ijkk.png

Ushirikishwaji wa Wananchi katika upangaji na utekelezaji wa mipango mbalimbali ya maendeleo katika Mtaa, hupelekea Wananchi kuwa na dhamana ya;

Kudhibiti Matumizi ya Rasilimali Katika Serikali za Mtaa kwa:-

➢ Kupitia vikao mbalimbali kama Viongozi na Wananchi wa kawaida.
➢ Kuhoji utendaji wa Viongozi wao kupitia vikao mbalimbali.
➢ Kwa kuwataka Viongozi wao kuwa wawazi juu ya mapato na matumizi na katika kuamua juu ya rasilimali mbalimbali za Mtaa.

Kuwadhibiti Viongozi wa Serikali za Mtaa kwa:-

➢ Kutochagua Viongozi wasio waadilifu na kuchagua Viongozi waadilifu.
➢ Kuwaondoa madarakani Viongozi wasio waadilifu kwa njia ya vikao halali kabla ya uchaguzi.
➢ Kuhoji utendaji wa Viongozi wao katika vikao mbalimbali vya kisheria wao wenyewe au kupitia wawakilishi wao.
➢ Kuhakikisha kuwa kuna uwazi katika uendeshaji wa shughuli za Serikali ya Mtaa.
 
Upvote 0
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom